Mpenzi wako akifa ndani kwako utafanyaje?

Mpenzi wako akifa ndani kwako utafanyaje?

Ita mjumbe, nendeni kutoa taarifa police.
Utaswekwa ndani kama wiki mbili uchunguzi ukiisha you are free to go. Ila jua selo kuingia ni bure ila kutoka si bure so usiwe na mkono mfupi.....
Sidhani kama unajua kuhusu kesi za mtu kufa mzee usiombe hata kidogo hasa kwa nchi zetu ambazo mifumo ya kisheria na haki haipo vzr ukikaa muda mchache ndani bhasi ni miaka 3 kwa kesi za hvyo naongea kwa uzoefu si hisia
 
Sidhani kama polisi wanafanya kazi namna hiyo. Wamuweke tu rumande mtu aliyeenda kutoa taarifa kwa sababu mtu amefia kwake!
Mfano wewe ni askari mpelelezi.

Mimi ninaleta taarifa ndani kwangu kuna maiti ya mwanamke.

Usiku mzima kabla ya mauti kumkuta alikua na mimi tu.

Mshukiwa namba moja anatakiwa awe nani?
 
Ni vyema kuthibitisha afya ya demu kabla ya kumualika kulala gheto. Kama ikitokea ni kuripoti polisi na kupeleka mwili mortuary. Kama kutakuwa na kesi, basi utajitetea. Na kama ikishindwa kesi, basi unakubali matokeo, ndio dunia hiyo!

Hahaha ni rahisi kusema tuu eti kuthibitisha afya kwanza ya mtu hahaha hivi unajua kweli unacho kiongea? Kwa mazingira ya kitanzania inawezekana? Ni mara ngapi wewe umeweza kujiridhisha juu ya afya ya wapenzi wanao kuja kwako?

Haya mambo huwa hata kuyajadili yanaogopesha maana sio mchezo kabisa omba hilo jambo lisikukute kabisa acha kabisa!
 
Unasubiri usiku kamlaze barabarani rudi home jifukize ujiepushe na maambukizi yakorona.AACHE KWAO AKAFIE KWANGU....so bure ni Korona.
 
Wakuu kwema?

Huwa najiuliza sana mfano imetokea umekuwa na mahusiano na mwanamke halafu baada ya wiki akaja kwako kulala halafu asubuhi unamuamsha unataka uingie mishe mishe unashangaa haamki, unamtikisa unaona hatikisiki, unammwagia maji haamki. Unahamaki kuona anatokwa povu mdomoni, unamgusa unakuta wabaridi

Unagusa kifuani unashtuka mapigo ya moyo hayadundi. Je, utatoka nje uwajuze majirani? Wataamini vipi kama ni bahati mbaya

Je, utatoroka?? Hapa utakuwa umejivua utu na itaonekana kama ulikusudia

Ukibaki tena ni msala tena msala kwelikweli

Je, utafanyaje??
bora ufate utaratibi wa kawaida kuita majirani, polisi na kuendelea ili kuku toa kwenye hatia
 
Kama chai vile, ila acha ninywe tu .. binadamu tuna hatari sana. Kulala na mtu chumbani na sio mkeo na kwao hawana information ni hatari sana

Hii sio chai mkuu huu mkasa ni wakweli kabisa. Mtu akishazima hata kama mlikua mmependana sana bila kutambulika kwao tayari ni tatzo hilo lazima uisome namba.
 
Nenda kwa mjumbe mpe taarifa.

Wewe na mjumbe mtaenda polisi kutoa taarifa.

Maiti itapelekwa hospitali. Wewe utakuwa mshukiwa namba moja hivyo utawekwa rumande na kuchukuliwa maelezo.

Mwili utafanyiwa autopsy ili kujua chanzo cha kifo. Lengo ni kujua kama ni natural death au kuna foul play.

Kama ni natural death hiyo kesi inakua haina locus standi kufunguliwa mahakamani so utaachiwa. Ikionekana kuna foul play mfano sumu hapa sasa show itakua ndefu.

NB. Usione naandika hivi ukadhani na askari wataenda step by step kama mimi unaweza shangaa upo gerezani kutumikia adhabu na mahakamani hukuwahi kwenda.

So you can just throw the whole ghetto away and elope to the nearest forest while figuring your next move.
Na ukute hiyo sumu kapewa kwingine kaja kufia kwako

Zaidi ya mume si busara kulala na hawara mpaka asubuhi asee
 
Nilikuwa Tanga demu akaanza kuumwa tumbo usiku hadi analia hapo mie wala sijamgusa. Kusema kweli niliogopa sana na nilikuwa najiuliza huyu akifa hapa ndiyo nafanyaje?
Yule mrembo tulipendana sana na nilijua atakuwa mke wangu. Penzi letu lilisababisha ugomvi mkubwa kati ya dada yake na shemeji yake. Dada mtu ambaye alikuwa akiniona mimi kijana wa maana sana hadi kunisifia kwa wadogo zake wa kike baada ya kujua tu mdogo wake ni mpenzi wangu akanichukia vibaya sana hadi akaanza vitisho kwangu kwamba ataniroga wakati mie nimeweka pamba masikioni. Shemeji alikuwa ananifagilia kwamba atuache na penzi letu hatimaye nao wakaanza kugombana kisa penzi letu. Dada mtu ndiyo akaamua kumhamishia binti Tanga kama vile Tanga na Dar umbali wake ni mbingu na ardhi
Endelea bitoz wa USA, Atlanta
 
Wakuu kwema?

Huwa najiuliza sana mfano imetokea umekuwa na mahusiano na mwanamke halafu baada ya wiki akaja kwako kulala halafu asubuhi unamuamsha unataka uingie mishe mishe unashangaa haamki, unamtikisa unaona hatikisiki, unammwagia maji haamki. Unahamaki kuona anatokwa povu mdomoni, unamgusa unakuta wabaridi

Unagusa kifuani unashtuka mapigo ya moyo hayadundi. Je, utatoka nje uwajuze majirani? Wataamini vipi kama ni bahati mbaya

Je, utatoroka?? Hapa utakuwa umejivua utu na itaonekana kama ulikusudia

Ukibaki tena ni msala tena msala kwelikweli

Je, utafanyaje??
Ndio maana mnaambiwa msiwe mnakaa na watoto wa watu hata hamuwajui vizuri na history zao. Unaweza kuta mtu ana conditions za kiafya, akizinguliwa kidogo tu anapata shida.....
 
Katika hio situation njia salama ,
Nikuchukua hio maiti ( mgonjwa)maana ww uwezi sibitisha
Kama mtu kafa;

peleka hospital Kama mgonjwa wakabidhi madoctor ;Andikisha nmba za ndugu zake;

Afu akishapokelewa majibu Kama kafa watachukua ndugu zake ;

Usije ukajichanganya eti utupe au uzike au utelekeze maiti gheto ;
 
Sidhani kama unajua kuhusu kesi za mtu kufa mzee usiombe hata kidogo hasa kwa nchi zetu ambazo mifumo ya kisheria na haki haipo vzr ukikaa muda mchache ndani bhasi ni miaka 3 kwa kesi za hvyo naongea kwa uzoefu si hisia
Mimi nishashuhudia kabsa na nikashughulikia hiyo kesi. Demu alikufa mchezoni. Postmortem ilipotoka ilionekana demu alikua na matatzo ya mapafu. Ilituchukua week mbili na nusu kutatua hili swala la liliisha kabsa......

Follow procedure na usiongeze wasiwasi kwa kukimbia......

Halafu mtindo wa kuandika majina ya uongo guest mbaya sana.....
 
Kiukweli kusema mtu usipanick ilo haliwezekani ,Ila ukiona imekukuta hali kma iyo Kodi taxi au bajaji haraka sna mpeleke hospital then mengine mtajua huko huko mbeleni ,japo kesi kma hizi maamuzi na majibu yatakuja hapo hapo siku ya tukio ... finally usiombe hii kitu ikukute yni utumbo mpaka mapumbu lazima yaweweseke
 
Back
Top Bottom