Mpenzi wako akifa ndani kwako utafanyaje?

Mpenzi wako akifa ndani kwako utafanyaje?

Wakuu kwema?

Huwa najiuliza sana mfano imetokea umekuwa na mahusiano na mwanamke halafu baada ya wiki akaja kwako kulala halafu asubuhi unamuamsha unataka uingie mishe mishe unashangaa haamki, unamtikisa unaona hatikisiki, unammwagia maji haamki. Unahamaki kuona anatokwa povu mdomoni, unamgusa unakuta wabaridi

Unagusa kifuani unashtuka mapigo ya moyo hayadundi. Je, utatoka nje uwajuze majirani? Wataamini vipi kama ni bahati mbaya

Je, utatoroka?? Hapa utakuwa umejivua utu na itaonekana kama ulikusudia

Ukibaki tena ni msala tena msala kwelikweli

Je, utafanyaje??
Jisalimishe polisi waeleze ukweli wote na km ni mtu wa church au Msikiti basi huko nako wape ukweli mtupu usiwafiche.For sure Mambo yatakaa sawa.
 
Back
Top Bottom