Mpenzi anataka nibebe mimba ndio aende kwetu

Mpenzi anataka nibebe mimba ndio aende kwetu

Wengi walikokosea hapo. Hata wewe mwenyewe mwanzoni ulikosea hapo hapo. Na sasa unataka kukosea tena hapo hapo? Unataka ujifunze mara ngapi? Hata hivyo sitamlaumu huyo bwana maana baadhi yenu wanamichezo ya hatari mno siku hizi!
 
Achana naye huyo, kwani wanao oa na kuolewa wote wanapata watoto? Kwanza wewe unamtoto tayari embu fanya shughuli zako punguza stress za kuolewa, muoaji anajulikanaga tu mapema, wewe beba kama utamuona hataki kukuona ukipendeza anataka kukufanya kipozeo watoto 2 anajua hapo hutakuwa na ujanja utamwabudu yeye huyo panya road mkubwa
 
STUKA!! Ukipata mimba anaingia mitini! Usiuingie huo mkenge. Wengi wameshaadhirika na kuishia kuwa single mothers.

Habari wana Jf. Mimi nina miaka 33 nina mtoto wa miaka miwili na nusu. Baba wa mtoto nilipozaa mtoto tuliendelea na mahusiano nilimsihi aende kwetu hakwenda nikaamua niachane nae kwa sababu niliona anadharau wazazi wangu kwa kutokwenda nyumbani. Mwaka huu katika mawasiliano na mpenzi wangu wa zamani tukaanza mahusiano ila anataka nibebe mimba ndio aende kwetu. Na nyumbani hawataki nibebe mimba kabla mtu hajaenda. Anasema nampa masharti wakati niliezaa nae sikumpa masharti ya kwenda kwetu kabla ya kunipa ujauzito. Naombeni Ushauri hapa kuna muoaji kweli au anataka alipize kisasi. Nahisi kuchanganyikiwa.
 
Unamtoto huyo pili nini tena si ajabu tayari anamchumba kitendo cha wewe kubeba mimba tu utakuwa mwendo wa mateka, halafu kwanini wanawake wengine mnapenda kurudiaga matapishi? Ndiyo nyie mnaishiaga kundungwa mavifu ya usoni
 
Pole,hapo hakuna muoaji ila kama utabahatika kutafta mtoto kwa yule wa mwanzo niafadhali ili watoto wawe wa baba mmoja.kuzaa watoto wa baba tofauti si nzuri sana...niushauri tu lakini
 
Upumbavu was sisi wa bongo baadhi ndo huu. Kasi kusambaza mayai hovyo Kama kunguni eti mapenzi ya kweli mpaka mimba pole dadangu mpendwa usikubali upumbavu Kama huo wa kutelekezwa kidzining.alafu wanaume mda mwingine tuwe na huruma na mbegu zetu tunazosambaza hovyo Kama kuku mwishowe mtoto wa watu akienda kutoa was Kwanza kumharibia sifa ni wewe hivi ungetegemea aleaje mtu mwenyewe pengine beki tatu aisee inaniumaga Sana hatua ya kujaga KUOA ndio umakini wangu tuuuu!!alafu mda mwingine mapenzi yasio ya ndoa tue makin nao
Subiri ukue mkuu....
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mambo mawili ya kijinga nilioyaona.

Jamaa kuachana na jamaa yako alokuzalisha sababu tu alikataa kuja kwenu... Maana ulupaswa kutafuta njia nyinginr ya kuhakikisha mko pamoja.


Unajiona hufai, na unaish kwabahat..najamaa keshajua unataman ndoa na yy unamwona km Mtu pekee. Nasababu umezaa, basi huna lakufanya.


Kama unajiamin ,,, kataa katakata kubeba mimba kabla ya kujitambulisha kwenu.


Hiyo ndo sehem yakujua km anania naww au...... Ukibeba mimba ,ndo umepata mtoto wapili asokua nababa.


Kataa...asupokukubali....njoo unitafute, mimi tutaenda wote kwenu, nijitambulishe, nikubebe mzima mzima .
 
Unataka ufanye kosa LA pili tena?? Sitaki kuamini kwamba tusipo kushauri hapa ungefanya hivo jamaa anachotaka?? Mungu atusaidie kwenye maamuzi yetu
 
Eehe kwa Huo umri naona unachanganyikiwa kabisaa...Ila usibebe aisee anaweza kukubebesha akakuacha huyoo!!
Kumbe wewe ndiye hutaki nipatiwe mtoto na huyo Kipenzi changu eeeh!...?

Sasa subiri mziki wake utakapokatiza pale mtaani kwangu ukitokea mazoezini nikufundishe adabu ili usiingilie mahusiano yangu na Kipenzi changu cha roho.
 
Achana na huyo mwanaume. Atakuumiza tena.

Mwanamke kama ulimuacha mwanaume, kurudiana nae tena unatafta matatizo.

Utashika mimba yake alafu abaki kukuzodoa kua huna jipya ulikosa soko ndio maana umerudi kwake. Utapoteza thamani yako. Pamoja na hilo hakuna mwanaume anaekataa K zinazojileta zenyewe hata kama hakuhitaji tena.

Hapo hakuna muoaji.

Kwa nini unahofu kua anataka kulipa kisasi? Ulimfanyaje?

Huu ni ushauri wangu wa bure kwa wanawake. Ukimuacha mwanaume kwa sababu yoyote ile usirudiane nae, ukirudiana nae kwake unakua umekosa thamani, maana anakuona kama mtu uliekosa soko huko umerudi.
Ukweli mtupu, japo ni mchungu lakini ni bora sana kuuanika hapa ili uokoe madhara watayopatwa nayo Dada na Mama zetu wakithubutu kutenda hivi.
 
Habari wana Jf. Mimi nina miaka 33 nina mtoto wa miaka miwili na nusu. Baba wa mtoto nilipozaa mtoto tuliendelea na mahusiano nilimsihi aende kwetu hakwenda nikaamua niachane nae kwa sababu niliona anadharau wazazi wangu kwa kutokwenda nyumbani. Mwaka huu katika mawasiliano na mpenzi wangu wa zamani tukaanza mahusiano ila anataka nibebe mimba ndio aende kwetu. Na nyumbani hawataki nibebe mimba kabla mtu hajaenda. Anasema nampa masharti wakati niliezaa nae sikumpa masharti ya kwenda kwetu kabla ya kunipa ujauzito. Naombeni Ushauri hapa kuna muoaji kweli au anataka alipize kisasi. Nahisi kuchanganyikiwa.
Unamtoto huyo pili nini tena si ajabu tayari anamchumba kitendo cha wewe kubeba mimba tu utakuwa mwendo wa mateka, halafu kwanini wanawake wengine mnapenda kurudiaga matapishi? Ndiyo nyie mnaishiaga kundungwa mavifu ya usoni
Pole pole Mama, usiwaharibie Wanaume bahati zao maana wakati mwingine mapenzi ni upofu.
 
Umri huo bado unakili za kushikiwa,ukija kustuka utajikuta umezalishwa watoto kadhaa bila ndoa
Habari wana Jf. Mimi nina miaka 33 nina mtoto wa miaka miwili na nusu. Baba wa mtoto nilipozaa mtoto tuliendelea na mahusiano nilimsihi aende kwetu hakwenda nikaamua niachane nae kwa sababu niliona anadharau wazazi wangu kwa kutokwenda nyumbani. Mwaka huu katika mawasiliano na mpenzi wangu wa zamani tukaanza mahusiano ila anataka nibebe mimba ndio aende kwetu. Na nyumbani hawataki nibebe mimba kabla mtu hajaenda. Anasema nampa masharti wakati niliezaa nae sikumpa masharti ya kwenda kwetu kabla ya kunipa ujauzito. Naombeni Ushauri hapa kuna muoaji kweli au anataka alipize kisasi. Nahisi kuchanganyikiwa.
 
Nashauri mwambie Nina mimba yako uone malengo yake
 
Pole pole Mama, usiwaharibie Wanaume bahati zao maana wakati mwingine mapenzi ni upofu.
Ni ushauri tu baba [emoji23] [emoji23] [emoji23] sio lazima kuupokea maana maamuzi yapo kwake na changamoto ni zake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom