Mpango wa vyakula shuleni usigeuzwe dili.

MWAKIGOBE

Member
Nov 1, 2010
65
2
Hivi karibuni serikali imeanza mpango wa kutoa vyakula kwa wanafunzi mashuleni lengo ni pamoja na kuwavutia watoto kwenda shule. mpango huu umekuwa ukidhaminiwa na watu binafsi pamoja na mashirika mbalimbali. lakini huko mbeya wilaya ya rungwe katika vijiji vya rungwe walimu wamekuwa wakiwaagiza kila mwanafunzi apeleke debe moja la mahindi kila mwezi. kwa mzazi mwenye watoto wanne, anatakiwa kupeleka debe nne. hii inaleta usumbufu na malalamiko kwa wazazi. jamani naomba tusitafsiri vibaya mpango huu,
 
Back
Top Bottom