Mbwa dume
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 6,289
- 10,992
Ni kweli huwa natamani sana kuexport mzigo nje ya mipaka lakini tatizo ni uhakika wa masoko mkuu.Mkuu kwanini usipeleke hii fursa ubalozi wa Russia ili kuyauza majeneza Russia, watu wanapukutika saana huko.
Mfano kuna kipindi niliona hapa Dom biashara sio nzuri nikaamua kuvuta mkopo bank ili nikafungue brach Dar na Zanzibar lakini kilichonikuta sintokaa nisahau!
Biashara iligoma hasa Zanzibar misiba mingi ilikuwa ni ya waislamu tu yaani unakata miezi mitatu umeuza jeneza moja au mawili tu tena kwa kutumia madalali ilifika mahali pesa ya kodi na mshahara wa kumlipa kijana ikashindikana nikaamua kufunga kijiwe.
Mpaka sasa nimeamua nikomae tu na hii office ya Dom na Dar angalau nina uhakika wa soko hasa msimu huu wa mwisho wa mwaka huwa mambo sio mabaya