Ni Asset? Unajua ilisemwa anakuja na Wabunge wangapi? Mpaka sasa hata wale wa kufa kupona wanagombea huko CCM ....unajua nguvu kubwa inayotumika kupangua hoja za ufisadi kuliko kunadi ilani ya Chadema? Hivi nyie mashabiki mnaijua hata hiyo ilani japo kidogo? Bora hata magufuli anatembea nayo na kuinadi .....Hivi unaamini idadi ya mahudhurio kwenye mikutano ndio kura? Pengine hukujua nini kilitokea kwa Mrema na hata Dr Slaa mwaka 2010 .....huu uchaguzi tunapoteza vibaya hadi level ya ubunge (mark my word) ....hatuna hoja nzito zaidi ya kuaminisha watu kuichoka tu CCM tena kazi hiyo ikifanywa na akina Sumaye ......Aibu tu ....
mkuu siasa ni watu, kama ilani ndo ushindi chadema au Cuf wamekuwa na ilani nzuri tu lakini hawajahi kufikisha asilimia 30 ya kura za urais, mwaka huu hali ilikuwa inaelekea kuwa mbaya zaidi lakini kwa sasa nchi ina mwamko mpya, unataka asset ipi zaidi ya hii ya chama kupata nguvu kwenye mioyo ya wananchi?