Moyo una mengi

:: Nitetee Mola Wangu


1 Nitetee Mola wangu
Wewe kimbilio langu
Duniani sina changu

2 Hali yangu vangu vangu
Nikulacho ni kichungu
Nimejawa naukungu

3 Siku ya tatu sijala
Na bado ni masajala
Nakesha kwenye jalala

4 Kuyaokota makopo
Ningeupata mkopo
Au ja kazi ya popo

5 Maisha yangu ni duni
Sina kitu mfukoni
Uzito upo kitwani

6 Muda wote ni majozi
Nacheka yaja machozi
Vitamu kwangu ni njozi

7 Njoo wangu muokozi
Nsije fanya udokozi
Kifo kiwe yangu dozi

[emoji2399] Abuuabdillah[emoji1607]
Ibn Kimweri
 
Ni utenzi ama kweli?
Nipa Neema Wadudi


1 Umenishika utungu, Matozi ndani ya maji
Menichoma nungunungu, ninakosa mfariji
Sijui ni lepi fungu, wala sinalo taraji

2 Yanisakama mawazo, usiku kesha silali
Kila yaumi vikwazo, mwisho ungali umbali
Lini nipate tulizo, hakunapo afadhali

3 Ati kukua ni huku, dunia mejaa tabu
Nakula kwa chukuchuku, ambwa natiwa adabu
Napeza kula makuku, ninenepe kama dubu

4 Naenda huku na kule, ila bado yale yale
Amara hii na ile, halitoshi lake bale
Sipati japo uwele, nifurahi nami nile

5 Madeni tele yan'zidi, ulimwengu masumbuko
Nipa neema Wadudi, fuadini machubuko
Mola sijamkaidi, ingali ni sokomoko

[emoji2399]Abuuabdillah[emoji3578]
0744883353
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ