Moyo Ulioonja Maumivu

Moyo Ulioonja Maumivu


Jinga wewe
Sitarudia tena, nilijisahau nikajua nipo kule chini...

Hakyamungu nikibakwa sitalia, sitachukia, sitasikitika, sitashitaki mahala popote zaidi nitafurahi na nitajipitisha kila siku ili nibakwe....
 
SEHEMU YA 34

Aliishika, aliibeba kana kwamba alikuwa mtoto mzima, alilia huku ikiendelea kuwa mikononi mwake.

Hakujua ni kwa namna gani Mungu aliruhusu maumivu hayo katika maisha yake, alitamani arudishe mishale ya saa nyuma ili kila kitu kianze upya lakini si kupitia maumivu makali aliyokuwa akiyapitia.

“Nitakupenda maisha yangu yote Harry!” alisema Theo huku mwili wa mtoto wake ukiwa mikononi mwake.

Alikaa humo kwa dakika kadhaa, alipomaliza, madaktari wakamwambia kuhusu kumzika mtoto huyo. Hakutaka kufanya hivyo mpaka pale ambapo mke wake angerudiwa na fahamu. Hilo halikuwa tatizo, kulikuwa na jambo jingine ambalo dokta alihitaji sana kuzungumza naye.

Moyo wa Theo ukapiga paa! Hakuamini kama kulikuwa na jambo jingine tena, lilikuwa nini? Kuhusu hali ya mke wake ama?

Hakuwa na jinsi, akaondoka na marafiki zake na kuelekea katika ofisi ya daktari yule na kukaa pamoja.

Alijua kabisa kwamba Theo aliumia moyoni mwake, hakuwa na jinsi, alitakiwa kumwambia ukweli kuhusu jambo jingine, yaani kama kulia, alitakiwa kulia tena lakini si kumruhusu aondoke na siku nyingine amwambie kuhusu tatizo jingine, kilio kingeanza upya.

“Niambie kuna nini? Ni kuhusu mke wangu? Dokta, naomba usinifiche kitu, kama kuumia, nimeumia sana, na kama kulia nimelia sana, naomba uniambie, mimi mwanaume,” alisema Theo japokuwa moyoni mwake alijua hakuwa na moyo wa kuvumilia maumivu makali.
“Ni kuhusu mtoto wako!” alisema dokta.
“Nani? Rachel?”
“Ndiyo!”

“Amefanyaje?” aliuliza Theo, akaishiwa pozi, akabaki pale kwenye kiti huku akili yake ikizidi kuchanganyikiwa.

“Ana tatizo pia!”
“Tatizo gani?”
“Moyo wake umevimba, mishipa yake haina nguvu ya kusukuma damu vizuri,” alijibu daktari kitu kilichoanzisha kilio kingine kabisa ndani ya ofisi ile.

Hilo likawa jambo jingine jipya! Theo alilia sana, aliumia zaidi, hakuamini kile alichokisikia, yaani mtoto wake aliyebaki alikuwa na tatizo jingine tena, moyo wake kuvimba na mishipa yake haikuwa na nguvu ya kusukuma damu.
😢😢😢 hapa nimetoa chozi
 
Mtunzi Nyemo Chilongani sehemu ya 01


Gari aina ya Lamborghini Centenario LP 770 nyekundu yenye thamani ya zaidi ya dola laki tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni moja lilisimama nje ya Ukumbi wa Mlimani City uliokuwa jijini Dar es Salaam.

Waandishi wa habari waliokuwa mahali hapo kwa ajili ya kuripoti Mashindano ya Miss Tanzania wakaanza kulisogelea gari hilo huku wakiwa na kamera zao mikononi mwao.

Walimfahamu mtu aliyekuwa ndani ya gari hilo, walihitaji kupata picha kadhaa kwa ajili ya magazeti yao, tovuti na hata mitandao ya kijamii.

Hata kabla ya mtu kuteremka, wakaanza kupiga picha mfululizo, hakukuwa na mwandishi aliyekuwa radhi kuondoka mahali hapo, kila mmoja alihitaji kupata japo picha moja tu ya sura yake.

Baada ya kukaa kwenye gari kwa sekunde zaidi ya hamsini, hatimaye mlango ukafunguliwa na msichana mrembo, mwenye sura nyembamba, mrefu na kidoti pembeni ya pua yake, akateremka na kutoa tabasamu pana.

Alivalia gauni refu jekundu la kumeremeta mpaka chini, viatu vilivyokuwa na visigino virefu, shingoni alikuwa na cheni ya kike iliyoonekana kuwa ya dhahabu kabisa huku kwenye mkono wake wa kushoto akiwa na saa ya thamani aina ya Rolex aliyoinunua nchini Ufaransa alipokuwa akiishi.

Msichana huyu aliitwa kwa jina la Violeth Joseph Zilikana. Alikuwa mmoja wa wanawake waliokuwa na uzuri wa ajabu nchini Tanzania.

Alikuwa maarufu na aliyekuwa na pesa nyingi, alikwenda sehemu yoyote aliyotaka duniani, alipewa mialiko mingi kutoka sehemu mbalimbali kutokana na kazi ya mitindo aliyokuwa akiifanya.

Umaarufu wake ulikuwa mkubwa mno, alijua kupendeza, watu wengi walimpenda na kutamani sana kuwa naye lakini kwa sababu mume wake alifariki dunia, hakuwa tayari kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwanaume yeyote yule.


View attachment 944998


Vitabu hivyo....Moyo Ulioonja Maumivu.
Kopi 10,000 tu kwa Dar...mikoani ni 15,000 nakutumia.
Namba ya mawasiliano ni 0718069269 na namba ya malipo ni 0763986156.
Muda wa kuzurura kama kawaida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom