Moyo Ulioonja Maumivu

Moyo Ulioonja Maumivu

SEHEMU YA 38

Violeth alikuwa akilia, Theo alivyomwangalia, alishindwa kuvumilia, akaenda pembeni na kuanza kulia.

Moyo ulimuuma mno, hakujua ni maneno gani ambayo alitakiwa kumwambia mke wake huyo aliyekuwa na kiu ya kuwaona watoto wake, alihisi kabisa angeumia mno lakini pamoja na hayo yote ilikuwa ni lazima aujue ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

“I want to see my twins...” (nataka kuwaona mapacha wangu...) alisema Violeth huku akilia.

Daktari na manesi walipata kazi kubwa kumtuliza mpaka kutulia. Baada ya kuona wamefanikiwa, akamfuata Theo na kumwambia sasa ulikuwa ni muda wa kumfuata mke wake na kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea, hakutakiwa kumficha kwani endapo angefanya hivyo lingekuwa kosa kubwa sana.

“Ila ninaumia sana...” alisema Theo.
“Najua! Jikaze, wewe ni mwanaume...” alisema daktari.

“Atalia sana...itakuwaje? Nitashindwa kuvumilia,” alisema Theo huku akiyafuta machozi yake.

“Unatakiwa kuvumilia...” alisema daktari.
Hakuwa na jinsi, akajifuta machozi na kumfuata mke wake pale kitandani.

Alipomwangalia, alihisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake, aliumia kupita kawaida kwani kwenye vitu ambavyo hakutaka kabisa kuviona katika maisha yake basi yalikuwa machozi ya mke wake.

Violeth alimwangalia mume wake, bado moyo wake ulimwambia kulikuwa na jambo kubwa lililokuwa likiendelea, alihitaji kujua, alitaka kuambiwa ukweli ili kama kulia, alie, ahuzunike lakini mwisho wa siku akubaliane na ukweli juu ya kile kilichotokea.
“Mke wangu...” aliita Theo huku akimwangalia Violeth.

“Niambie ukweli...niambie ukweli mume wangu...” alisema Violeth huku akilia.
Theo hakuwa na jinsi, alitakiwa kufanya kama alivyoambiwa, alimwambia mke wake ukweli kwamba alijifungua watoto wawili kama walivyotaka lakini mtoto wa kiume ambaye walipanga kumpa jina la Harry alifariki dunia.

“Mume wangu...mume wan...” alisema Violeth lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake akaanza kulia.
 
SEHEMU YA 38

Violeth alikuwa akilia, Theo alivyomwangalia, alishindwa kuvumilia, akaenda pembeni na kuanza kulia.

Moyo ulimuuma mno, hakujua ni maneno gani ambayo alitakiwa kumwambia mke wake huyo aliyekuwa na kiu ya kuwaona watoto wake, alihisi kabisa angeumia mno lakini pamoja na hayo yote ilikuwa ni lazima aujue ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

“I want to see my twins...” (nataka kuwaona mapacha wangu...) alisema Violeth huku akilia.

Daktari na manesi walipata kazi kubwa kumtuliza mpaka kutulia. Baada ya kuona wamefanikiwa, akamfuata Theo na kumwambia sasa ulikuwa ni muda wa kumfuata mke wake na kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea, hakutakiwa kumficha kwani endapo angefanya hivyo lingekuwa kosa kubwa sana.

“Ila ninaumia sana...” alisema Theo.
“Najua! Jikaze, wewe ni mwanaume...” alisema daktari.

“Atalia sana...itakuwaje? Nitashindwa kuvumilia,” alisema Theo huku akiyafuta machozi yake.

“Unatakiwa kuvumilia...” alisema daktari.
Hakuwa na jinsi, akajifuta machozi na kumfuata mke wake pale kitandani.

Alipomwangalia, alihisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake, aliumia kupita kawaida kwani kwenye vitu ambavyo hakutaka kabisa kuviona katika maisha yake basi yalikuwa machozi ya mke wake.

Violeth alimwangalia mume wake, bado moyo wake ulimwambia kulikuwa na jambo kubwa lililokuwa likiendelea, alihitaji kujua, alitaka kuambiwa ukweli ili kama kulia, alie, ahuzunike lakini mwisho wa siku akubaliane na ukweli juu ya kile kilichotokea.
“Mke wangu...” aliita Theo huku akimwangalia Violeth.

“Niambie ukweli...niambie ukweli mume wangu...” alisema Violeth huku akilia.
Theo hakuwa na jinsi, alitakiwa kufanya kama alivyoambiwa, alimwambia mke wake ukweli kwamba alijifungua watoto wawili kama walivyotaka lakini mtoto wa kiume ambaye walipanga kumpa jina la Harry alifariki dunia.

“Mume wangu...mume wan...” alisema Violeth lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake akaanza kulia.
Pole mama mzazi
Shunie asante sana
 
SEHEMU YA 39

Aliumia moyoni mwake, kile alichoambiwa hakutakiwa kukisikia kabisa, alikumbuka jinsi alivyoishi na mume wake, walivyokuwa na mipango mingi kuhusu watoto wao, walipanga mambo mengi, waliwafanyia shopping, waliwanunulia kila kitu mpaka kuwaandalia majina lakini mwisho wa siku, kila kitu kilionekana kwenda hovyo.
Theo ndiye alikuwa mfariji wake pekee, alilia sana lakini mwanaume huyo alikuwa pembeni yake na kuanza kumbembeleza kwa maneno mengi ya kutia moyo, maneno ambayo aliamini yangeweza kumsahaulisha mke wake juu ya watoto wake hao.
“Violeth! Usilie, hutakiwi kumkufuru Mungu. Kumbuka kila kitu kinachotokea ni mipango ya Mungu, kulia sana inamaanisha kwamba unakosoa kazi zake alizozifanya. Nyamaza, kama amemchukua mtoto wetu mmoja, ametuachia mmoja kwa sababu zake, naomba umshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema Theo kwa sauti ya chini, karibu kabisa na sikio la mke wake.
“Ninaumia sana...moyo wangu unaumaaaa....” alisema Violeth.
“Najua! Nimeumia pia kama wewe unavyoumia ila kuumia kwangu, machozi yangu hayawezi kumrudisha Harry! Naomba unyamaze mpenzi....” alisema Theo huku akimbembeleza mke wake huyo.
Mwisho wa siku Violeth alitakiwa kukubaliana na ukweli wa kile kilichotokea, kwamba mtoto wake mmoja alifariki dunia na kubaki mmoja.
Waliendelea kufarijiana mpaka pale walipokabidhiwa mwili wa mtoto wao na kwenda kuuzika katika makaburi yaliyokuwa nyuma ya hospitali hiyo.
Stori kuhusu kile kilichotokea zikaanza kusambaa kila kona, watu waliwaonea huruma, kila mmoja alisikitika mno kwani walikumbuka namna mwanamke huyo na mume wake walivyokuwa wakiwaambia kuhusu mapacha hao, jinsi watakavyotokea kuwapenda na kuwalea katika malezi mazuri lakini mwisho wa siku hawakufanikiwa kuwa na watoto wote wawili.
Watu wakawatumia salamu za pole, waliguswa na wengine kwenda kuwatembelea nyumbani kwao. Kwenye mitandao ya kijamii, ni stori kuhusu familia hiyo tu, ndiyo walikuwa watu maarufu kuliko mastaa wote nchini Tanzania hivyo hata viongozi wa serikalini na watu wengine wote waliwapa pole kwa kile kilichokuwa kimetokea.
 
SEHEMU YA 40

Kuhusu suala la ugonjwa wa Rachel, Theo hakutaka kumwambia mke wake, alijua kabisa angemchanganya zaidi hivyo aliamua kutulia kwa kubaki kimya mpaka pale ambapo tatizo hilo lingeanza kujitokeza.
Nyumbani, Violeth hakuwa na furaha, moyo wake ulimuuma mno, kila alipokuwa akimwangalia mtoto wake huyo alihisi maumivu makali, wakati mwingine alimlaumu Mungu kwa kumchukua mtoto wake ambaye alikuwa na mipango naye mingi lakini kuna kipindi alimuomba msamaha kwa kuwa kile kilichotokea, kilipangwa hata kabla ya yeye kuzaliwa.
Siku ziliendelea kwenda mbele, baada ya mwezi mmoja, Theo akarudi katika hali ya kawaida na kuendelea kufanya kazi zake za muziki. Alirudi na nguvu mpya, alitoa nyimbo mbili ambazo aliamini zingefanya vizuri kabisa.
Alichokitegemea ndicho kilichotokea, zilikuwa nyimbo kali sana ambazo zilipendwa na kila rika, kila mtu aliyezisikia aligundua kabisa kwamba Theo alirudi kivingine, alirudi na nguvu mpya ya kufanya ngoma kali zaidi.
Alichokifanya ni kufanya video zake, hakuzifanyia nchini Tanzania, aliamua kusafiri na kuelekea nchini Afrika Kusini na kuzifanyia huko. Kila mtu aliyeziona video hizo baada ya kuachiwa alichanganyikiwa, zilikuwa kali na zilizomfanya kuonekana kuwa mwanamuziki mwenye jina kubwa, hatari na aliyeiwakilisha vizuri Tanzania.
Alipokuwa huko, hakuacha kuwasiliana na mke wake, kila siku ilikuwa ni lazima kuzungumza naye kupitia video. Alimuona mtoto wake, alimsalimia, moyo wake ulikuwa na furaha mno kuiona familia yake ikiwa salama lakini kila alipokumbuka kwamba Rachel alikuwa na tatizo kwenye moyo wake, aliumia mno.
“Mbona umebadilika ghafla?’ aliuliza Violeth huku akimwangalia mume wake kwenye kompyuta yake kupitia mtandao wa Skype.
“Hapana! Nipo kawaida.”
“Kweli?”
“Yeah! Nipo kawaida. Nikuletee zawadi gani mpenzi?” aliuliza Theo, alijitahidi kumtoa mke wake katika suala la kutokuwa na furaha.
“Yoyote tu mpenzi!”
“Basi sawa, nitakufanyia sapraizi moja kubwa mno!”
“Kweli?”
“Niamini mpenzi!”
“Nakupenda sana!”
“Nakupenda pia.”
 
SEHEMU YA 41 “Iyanya...” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja kutoka kwenye gari moja la kifahari, Hummer nyekundu iliyokuwa imepaki pembeni ya duka moja la nguo lililokuwa Johannesberg nchini Afrika Kusini.
“Who are you?” (nani wewe?) aliuliza msichana aliyeitwa.
“Your Instagram friend! I liked your pictures yesterday and you connected me in you live video, do you remember me?” (Rafiki wako wa Instagram! Nilizipenda picha zako jana na uliniunganisha kwenye ile video ya moja kwa moja) alijibu mwanaume huyo.
Iyanya akasimama na kumwangalia mwanaume huyo, alikuwa chotara, mwenye asili ya Kiswahili na Kiarabu. Mwili wa Iyanya ukasisimka, alimwangalia mwanaume huyo, alikuwa mzuri wa asili.
Haraka sana akateremka kutoka ndani ya gari na kumsoegelea msichana huyo, alipomfikia, akamsalimia kwa kumpa mkono. Iyanya alipogusana naye tu akahisi mwili wake ukisisimka kupita kawaida.
Ni kweli aliwahi kukutana na wanaume wengi, alilala nao kitanda kimoja lakini wa siku hiyo alikuwa balaa, alikuwa mzuri kupita kawaida na kila alipomwangalia, moyo wake ulimwambia ni lazima kuzaa naye.
 
SEHEMU YA 42

Huyo aliitwa Iyanya Kobero, msichana wa Kizulu aliyekuwa na urembo wa kila namna. Alikuwa mwembamba, kiuno chake kilikuwa chembamba zaidi lakini kwa nyuma alifungashia.
Alikuwa mzuri, alijua kupendeza na kila alipokuwa akipiga picha, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuyaonyesha makalio yake kwanza huku lengo lake likiwa ni kuwadatisha wanaume wengi.
Iyanya alikuwa mfanyabishara mkubwa mitandaoni. Alifungua akaunti yake Instagram kwa ajili ya kujiuza. Aliweke picha nyingi zilizokuwa na mitego ya kila namna, mwanaume ambaye alimtaka, alimfuata sehemu ya meseji, waliwasiliana na kumpa namba ya simu.
Hiyo ndiyo ilikuwa biashara yake, alikuwa malaya, si wa kwenda klabu au barabarani, aliingiza pesa kupitia akaunti yake ya Insragram tu. Alikuwa mwanamke hatari, aliyezitetemesha ndoa za watu wengi, kulikuwa na wanawake waliolia sana kuibiwa wanaume zao, ilikuwa ni vigumu kuiona picha ya Iyanya kwenye akaunti yake halafu usibonyeze sehemu ya ‘like’
Shepu yake, jinsi kali lake lilivyokuwa ndiyo ilikuwa silaha yake kubwa, ya kuwateka wanaume wengi kiasi kwamba alikuwa na uhakika wa kulala na wanaume wanne tofauti ndani ya wiki moja kwa malipo makubwa tu.
Hiyo haikuwa kwa Iyanya tu, kulikuwa na wasichana wengi katika vyuo mbalimbali nchini Afrika Kusini ambao kazi yao ilikuwa ni kujiuza tu kwenye mitandao ya kijamii.
Ni kama mambo yalionekana kunoga kwani kila msichana ambaye aliamini kwamba alikuwa na makalio makubwa, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuingia kwenye mitandao ya kijamii, kupiga picha za kihasara na kuziweka huko, na kwa kufanya hivyo, walitengeneza pesa nyingi mno, na miongoni mwa watu hao alikuwa huyo Iyanya.
|
|
|
Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 43

Wakati Theo akijiandaa kwenda kufanya video nchini Afrika Kusini, kampuni ambayo ilikuwa ikitarajiwa kufanya video hiyo ikaanza kuandaa warembo kwa ajili ya kutumika. Miongoni mwa warembo hao alikuwepo Iyanya ambaye alitumia video nyingi kuwatega wanaume na kuwalia pesa zao.

Alipoambiwa kwamba video ambayo walitakiwa kushuti ilikuwa ni ya Theo, alichanganyikiwa mno, alimpenda mwanaume huyo kupita kiasi, kwake, masupastaa hawakuwa wakipindua, alipenda kuwa nao na kufanya uchafu wowote ule huku akilipwa kiasi kikubwa cha pesa.

Alihitaji kujiweka katika mazingira mazuri, ya kumtega mwanaume huyo ambaye aliamini piga ua ilikuwa ni lazima achanganyikiwe kwa jinsi atakavyokuwa. Siku ambayo waliambiwa waende location, akaenda huku akiwa na muonekano wa kuvutia kupita kawaida.

Wanaume ambao walikuwa mahali hapo wakaanza kumwangalia kwa macho ya uchu, japokuwa hapo kulikuwa na wanawake wengi lakini huyu Iyanya alionekana kuwa moto wa kuotea mbali, alikuwa ni mzuri zaidi ya wanawake wote waliokuwa hapo.

Mitego yake ilikuwa ni kwa Theo tu. Alimpenda mwanaume huyo, alitamani kulala naye kitanda kimoja. Alihitaji pesa zake pia, aliamini kwamba endapo angekuwa na mwanaume huyo ingekuwa rahisi sana kupata pesa kutoka kwake, hivyo alitaka kujaribu bahati yake.
Baada ya kukaa hapo kwa dakika kama thelathini ndipo Theo akaingia huku akiwa na wapambe wake.

Iyanya alipomuona tu, moyo wake ukapiga paaa, hakuamini kumuona mwanaume huyo mahali hapo, siku hiyo alipomwangalia, alionekana kuwa mzuri kupita kawaida.
Theo hakutakiwa kuongea na mtu yeyote, hasa wanawake hao ambao walipelekwa mahali pale kwa ajili ya kushuti kisha kuondoka zake.

Kwa Iyanya hilo likaonekana kuwa gumu, hakuwa tayari kufika sehemu ya tukio, amwangalie Theo na kuona mwanaume huyo akiondoka pasipo kuongea naye lolote lile.

“Ni lazima nitaongea naye! Siwezi kubaki kama sanamu,” alijisemea huku muda mwingi wa kushuti macho yake yalikuwa kwa mwanaume huyo tu.
 
SEHEMU YA 44

Theo hakuwa na habari, alifika mahali hapo kwa kazi moja tu. Aliwaona wanawake wote kuwa sawa, kichwa chake kilikuwa na mawazo juu ya familia yake na yale mambo yote ambayo walikuwa wakipitia.

Kushuti video hiyo ilichukua saa nne ndipo wakapumzika kwa ajili ya kupata chakula. Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya Iyanya kumfuata mwanaume huyo na kutaka kuongea naye. Haraka sana akasimama alipokuwa na kuanza kumsogelea.

Wapambe wake walipomuona, wakamzuia lakini Theo akawaambia wamuache kwani kusingekuwa na tatizo lolote lile kama angekaa na msichana huyo na kuzungumza naye.

Kwa Iyanya hiyo ikaonekana kuwa kama bahati, alikuwa na nafasi moja maishani mwake, nafasi ambayo ingempa hatma ya maisha yake kwa mwanaume huyo, hiyo nafasi alitakiwa kuitumia kwa umakini sana, yaani kama angeshindwa hiyo, basi asingeweza kupata tena.

Alimwangalia Theo, akamsogelea na kukaa karibu naye huku wakila. Moyo wake ulikuwa na furaha mno, alimpenda mwanaume huyo kupita kawaida, alitamani kumwambia kile kilichoujaza moyo wake muda huo lakini akaamua kutulia kwanza.

“Hii ni nafasi ya bahati sana kuwa katika video yako,” alisema Iyanya huku akimwangalia mwanaume huyo ambaye kwa mbali alionekana kutokuwa sawa.
“Kwa nini?”

“Wewe ni maarufu sana. Nadhani kupitia video yako nitakwenda kupata jina,” alisema Iyanya huku akiachia tabasamu pana, kwa jinsi alivyokuwa mzuri, uzuri wake ukaongezeka maradufu.
Theo hakujibu kitu zaidi ya kuachia tabasamu tu.

Alimwangalia msichana huyo, ni kweli alikuwa mrembo lakini hiyo haikuwa sababu ya kutaka kulala naye kwa sababu alijiheshimu sana, kubwa zaidi alimuheshimu mno mke wake.
“Theo! Ninahitaji msaada wako!” alisema Iyanya huku akimwangalia Theo.
“Msaada gani?”
 
SEHEMU YA 44

Theo hakuwa na habari, alifika mahali hapo kwa kazi moja tu. Aliwaona wanawake wote kuwa sawa, kichwa chake kilikuwa na mawazo juu ya familia yake na yale mambo yote ambayo walikuwa wakipitia.

Kushuti video hiyo ilichukua saa nne ndipo wakapumzika kwa ajili ya kupata chakula. Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya Iyanya kumfuata mwanaume huyo na kutaka kuongea naye. Haraka sana akasimama alipokuwa na kuanza kumsogelea.

Wapambe wake walipomuona, wakamzuia lakini Theo akawaambia wamuache kwani kusingekuwa na tatizo lolote lile kama angekaa na msichana huyo na kuzungumza naye.

Kwa Iyanya hiyo ikaonekana kuwa kama bahati, alikuwa na nafasi moja maishani mwake, nafasi ambayo ingempa hatma ya maisha yake kwa mwanaume huyo, hiyo nafasi alitakiwa kuitumia kwa umakini sana, yaani kama angeshindwa hiyo, basi asingeweza kupata tena.

Alimwangalia Theo, akamsogelea na kukaa karibu naye huku wakila. Moyo wake ulikuwa na furaha mno, alimpenda mwanaume huyo kupita kawaida, alitamani kumwambia kile kilichoujaza moyo wake muda huo lakini akaamua kutulia kwanza.

“Hii ni nafasi ya bahati sana kuwa katika video yako,” alisema Iyanya huku akimwangalia mwanaume huyo ambaye kwa mbali alionekana kutokuwa sawa.
“Kwa nini?”

“Wewe ni maarufu sana. Nadhani kupitia video yako nitakwenda kupata jina,” alisema Iyanya huku akiachia tabasamu pana, kwa jinsi alivyokuwa mzuri, uzuri wake ukaongezeka maradufu.
Theo hakujibu kitu zaidi ya kuachia tabasamu tu.

Alimwangalia msichana huyo, ni kweli alikuwa mrembo lakini hiyo haikuwa sababu ya kutaka kulala naye kwa sababu alijiheshimu sana, kubwa zaidi alimuheshimu mno mke wake.
“Theo! Ninahitaji msaada wako!” alisema Iyanya huku akimwangalia Theo.
“Msaada gani?”
mengi mengi kwako
 
SEHEMU YA 44

Theo hakuwa na habari, alifika mahali hapo kwa kazi moja tu. Aliwaona wanawake wote kuwa sawa, kichwa chake kilikuwa na mawazo juu ya familia yake na yale mambo yote ambayo walikuwa wakipitia.

Kushuti video hiyo ilichukua saa nne ndipo wakapumzika kwa ajili ya kupata chakula. Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya Iyanya kumfuata mwanaume huyo na kutaka kuongea naye. Haraka sana akasimama alipokuwa na kuanza kumsogelea.

Wapambe wake walipomuona, wakamzuia lakini Theo akawaambia wamuache kwani kusingekuwa na tatizo lolote lile kama angekaa na msichana huyo na kuzungumza naye.

Kwa Iyanya hiyo ikaonekana kuwa kama bahati, alikuwa na nafasi moja maishani mwake, nafasi ambayo ingempa hatma ya maisha yake kwa mwanaume huyo, hiyo nafasi alitakiwa kuitumia kwa umakini sana, yaani kama angeshindwa hiyo, basi asingeweza kupata tena.

Alimwangalia Theo, akamsogelea na kukaa karibu naye huku wakila. Moyo wake ulikuwa na furaha mno, alimpenda mwanaume huyo kupita kawaida, alitamani kumwambia kile kilichoujaza moyo wake muda huo lakini akaamua kutulia kwanza.

“Hii ni nafasi ya bahati sana kuwa katika video yako,” alisema Iyanya huku akimwangalia mwanaume huyo ambaye kwa mbali alionekana kutokuwa sawa.
“Kwa nini?”

“Wewe ni maarufu sana. Nadhani kupitia video yako nitakwenda kupata jina,” alisema Iyanya huku akiachia tabasamu pana, kwa jinsi alivyokuwa mzuri, uzuri wake ukaongezeka maradufu.
Theo hakujibu kitu zaidi ya kuachia tabasamu tu.

Alimwangalia msichana huyo, ni kweli alikuwa mrembo lakini hiyo haikuwa sababu ya kutaka kulala naye kwa sababu alijiheshimu sana, kubwa zaidi alimuheshimu mno mke wake.
“Theo! Ninahitaji msaada wako!” alisema Iyanya huku akimwangalia Theo.
“Msaada gani?”
Hapo ndipo ninapokupendea Shunie yaan ukiipata tu unatukumbuka ubarikiwe sana
 
Kahaba Iyanya katika mawindo yake sasa,,, shukran sana mkwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom