Babu yangu aliwahi kunisimulia kuhusu kabila lililoitwa Abatwa ....
Kabila hilo lilikuwa dogo lenye nguvu za ushirikina apahapa Africa.
Kabila hilo la kichawi ilisemekana lilikuwa na tabia ya kuwafungia watoto kwenye ulimwengu wa giza au kunywa damu zao ili waongeze umri wa kuishi duniani .
Ipo hivi hii ni 2025 , hiyo hadithi nilipewa na babu, niliona kama hadithi ya mafikirio tu na sogeza muda ili viazi vya kuchoma viive pale Asante Nyerere....
Top story kwenye ulimwengu wa filamu ni kuhusu filamu inayoitwa "WEAPONS "yani SILAHA...
Filamu hii inamuhusu kijana Alex na familia yake ,Alex alikuwa ni mtoto wa pekee kwenye familia ya Mr Lily na Mme Lily...
Ilikuwa ni familia inayoishi kwa furaha, Alex alikuwa mwanafunzi, lakini ghafla furaha yao ilingia doa baada ya kuja Gladys ambaye ni shangazi wa mama yake Alex akiwa mgonjwa mno ....
Walianza kuishi naye fresh, lakini siku moja Alex ametoka Shule alimkuta bibi yupo imara lakini wazazi wake tayari ni misukule...
Dogo alivyohoji alipewa vitisho vingi na kuambiwa akae kimya la sivyo wazazi wake watauwawa...
Bibi bado alikuwa dhaifu, bibi ili awe imara alihitaji watoto.
Kwahiyo Ale aliambiwa " mjukuu hebu kalete kifaa chochote kile cha kila mwanafunzi wa darasani kwenu alafu mimi taondoka hapa na kuwaachia hii nyumba".....
Alex alienda shule kuiba kifaa cha kila classmate na kumletea bibi mzaa mama..
Alex bila kujua kumbe anaenda kuzalisha tatizo kubwa kwenye mji wake...
Oya hii filamu inaitwa...
WEAPONS YANI SILAHA...
C&P