Siyo kila maandamano na migomo huwa na lengo jema, mengine ni mabeberu huandaa watu kwa manufaa yao. Tafakar Libya waliandamana kwa sbb kipi kilipanda bei? Walikosa fedha za elimu? Walinyimwa matibabu?
Miundombinu ilikuwa duni? Lakini ukweli wa majawabu ya maswali haya na mengine mengi n Marekani wanataka kunyang'anya nchi ya Libya haki yake ya kumiliki rasilimali zake, hususan MAFUTA. Pia tukumbuke kuwa Uganda tayari ina mafuta, huenda MAREKANI wamegundua kuyapata kwa mikataba ya Buzwagi imeshindikana kwa Museven, sasa wamewatengeneza kina Besigye kwa malengo yaleyale ya Benghaz.
Kwa nini nasema hivi? Kwa sababu Museven hakukurupuka kuita wawekezaji wakati waganda hawajawa na ujuzi na taaluma ya mikataba ya malighafi hii, hivyo ilibidi akasomeshe vijana wa kignda kwa maandaliz ya faida ya taifa hilo.
Kwa mbinu hiyo wamarekani wamegundua kwa Museven mchana unageuka usiku kwao, cha msingi kumuondoa tuweke akina Besigye, kwani wao wanahitaji kutawala tu.
Chonde wanajamii migomo na maandamano ktk nchi zetu tuyapime kwa wigo mpana, nyuma yake kuna watu wana agenda tofauti. Tukishaanza chinjana wao huwa wako LONDON, NEW YORK, PARIS na kwingine kwa walowatuma kazi.