Tripo9
JF-Expert Member
- Sep 9, 2009
- 4,366
- 3,561
Nashukuru wote mlionipokea hapo Moshi December,kwa kweli nilijidai sana na wageni wangu walifurahi sana baada ya kula mtori na gali nyama choma vitu ambavyo havipo kabisa mitaa hii!!!
Kilichonishangaza ni jinsi mji wa Moshi ulivyobadilika sana sana,kwa kweli nilipoondoka niliacha maduka karibu yote makubwa yanaendeshwa na Wahindi,kusema kweli sikuona Mhindi hata mmoja,sijui wako wapi,,wamekimbia competition??]
Nimeshangaa kuona msururu wa magari na kuna traffic kubwa ya magari kitu ambacho hakikuwepo,pale soku kuu Moshi zamani tulikuwa tunapita na speed ya 120 lakini sasa hivi kutoka soko kuu kwenda stand ya mabasi utatumia dakika 20 na gari jambo la kushangaza sana
Vilevile tulishangaa kuona jinsi watu wa Moshi walivyobadilika na kutumia magari yao kwenda nyumbani,tulitoka moshi tarehe 23 kwenda dar,tulipishana na magari binafsi sio mabasi kuanzia Moshi mpaka Dar,magari mengi sana kitu ambacho hakikuwepo,
naona watanzania wameamka sana sasa hivi,hongereni sana wandugu.
Hapo kwenye nyekundu, wewe na mh Jakaya Kikwete munamitazamo sawa ktk hilo swala ie ni maendeleo kumiliki miguu mi4