Jabali la Siasa
JF-Expert Member
- Jul 10, 2020
- 2,557
- 2,188
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe Shaka Hamdu Shaka akimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa niaba ya Wananchi Wa Kilosa kwa kuwapatia daraja,
BILIONI 7 ZA DKT SAMIA SULUHU HASSAN KUTUMIKA UJENZI WA DARAJA LA BEREGA, KILOSA MKOANI MOROGORO
===
Wananchi wa Berega, wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro wamemshukuru sana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kufikia hatua nzuri daraja la Berega linalogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 7
Mradi wa huo unahusisha ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 140, upana mita 11, barabara mkaribio za daraja mite 600 na maboresho ya barabara kutoka Berega kwenda Dumbalume kilometa saba(km 7) katika halmashauri ya Wilaya ya Kilosa. Daraja hilo linaunganisha wilaya za Kilosa, Gairo na wilaya ya Kilindi mkoani Tanga.
Kadhalika mradi huu unatekelezwa na wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA). Mradi huu ni muhimu sana kwani utawezesha wananchi kufika hospitali ya Berega katika kupindi chote cha mwaka na utarahisisha shughuli za kiuchumi kama vile biashara na usafiriahaji wa mazao kufanyika kwa uhakika.
Kwa kweli acha wananchi wa Berega, Kilosa wampongeze Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo za ujenzi wa daraja hilo kama walivyofanya mbele ya mwenyekiti wa bodi TARURA, Mhandisi Florian Kabaka alipotembelea kukagua maendeleo ya mradi huo.
Kama Taifa hatuna budi kukiri kua katika miaka 2 ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan madarakani
AMEWEZA kutekeleza miradi mingi katika kila sekta, hivyo
ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu.
#Ameweza
#Anatosha
#TwendePamoja
#KwaMatokeoyaHaraka