Morogoro: Mkuu wa Mkoa asitisha mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuwabeba walanguzi

nokwenumuya

JF-Expert Member
Jun 29, 2019
810
2,851
Hii ni habari ya kusikitisha kwa Wakulima na hujuma kubwa toka kwa Mkuu wa Mkoa, mtu aliyetegemewa kuwasaidia wananchi sasa amekuwa mkandamizaji kwa wananchi.

Kwa takribani mwezi sasa kumekuwa na juhudi toka kwa wafanyabiashara wahindi na madalali wao wa kuzuia mfumo wa stakabadhi ghalani kutumika katika Mkoa wa Morogoro katika zao la Ufuta.

Bodi ya Maghala Tanzania ilishaandaa mfumo kwa ajili ya kuanza kufanya kazi katika msimu huu. Lakini leo mkuu wa mkoa kasitisha mfumo huo kutumika akisingizia kuwa eti Elimu kwa Mkulima haijamfikia hivyo mfumo uanze mwakani.

Mwaka jana alisitisha mfumo kuanza katika wilaya za mlimba na Malinyi. Lakini mfumo ulifanyika na kufanikiwa sana katika wilaya ya Ulanga.

Cha ajabu Mkuu wa Mkoa, Ndugu Martin Shigela kasitisha zoezi kwa sababu eti wakulima hawajapata taarifa na elimu ya kutosha. Sasa kama mwaka jana Ulanga walifanya? Na wakafanikiwa? Nao Elimu yao sio ya kutosha kweli?

Katika mnada uliofanyika mkoa wa Songwe 1st June, kilo moja iliuzwa kwa bei ya shilingi 2877.

Lakini madalali wa wahindi hununua ufuta kati ya shilingi 800 hadi 1600.

Mkuu wa Mkoa kusitisha zoezi hili kwa kisingizio Wakulima hawako tayari sio za kweli bali tuamini amefika bei kwa wahindi na kaamua kumuuza mkulima.

Mkuu huyo huyo wa Mkoa ndio alituma barua kwa wakuu wa Wilaya waandae mfumo ambako katima hizo wilaya tatu tayari Bodi ya Maghala ilishatafuta watunza maghala na kuyaandaa kwa muda mrefu ili kazi ianze.

Kweli hii awamu ya 6 ndio imeamua kurudisha nyuma juhudi zote za wakulima na kuruhusu wanyonyaji wachache waendelee kufaidika kupitia jasho la watanzania wanyonge?

Tunakuomba Rais Samia haya mambo uyaangalie. Itavunja moyo watu kulima. Bei za pembejeo ziko juu sana na bado wakuu wa mikoa wanatumika wakulima wasipate bei nzuri za mazao?

Ni lini huyo Mkuu wa Mkoa amekaa na Wakulima na akagundua hawana elimu ya kutosha? Inahitaji elimu gani kujua wauzie wapi?

Kama wamekuwa wanalima na kuja kuwauzia wahindi Dar, je watashindwa kupeleka mzigo kwenye ghala hapo hapo na uuzwe? Hizi ni hujuma za kipumbavu kabisa.

Huyu Mkuu wa Mkoa awajibishwe. Bodi ya Maghala imezunguka huko pamoja na TMX kutoa elimu kwa magari na gharama ya Serikali. Leo mtu mmoja sababu ya kupewa hongo anakuja kusitisha mfumo na wakati katika ghala la Ulanga, Mlimba na Malinyi tayari wameshaanza kukusanya Ufuta?

Mama Samia tunakuomba uwasaidie hawa Watanzania masikini wanaoonewa. Tutatoa namba kwa vyombo husika vya madalali wa wahindi ili kupitia TCRA mawasiliano yao yachunguzwe maana wao ndio wamekuwa wakimpigia simu ili aue huo mfumo. Aibu kubwa sana kwa Taifa letu.

Chini ni attachment ya tangazo lililotolewa na ofisi ya Mkurugenzi juzi. Ambalo leo Ndugu Shigella kasisitsha. Sasa serikali moja kila mtu anafanya yake. Wengine kwa maslahi ya wananchi. Wengine kwa maslahi ya wanyonyaji.

UPDATES:

MKUU WA MKOA WA MOROGORO KAFIKA LEO KATIKA GETI AMBALO MKUU WA WILAYA ALITOA MAAGIZO KUWA UFUTA USIOPITIA KATIKA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI USIVUKE KWA MUJIBU WA MAAGIZO YA SERIKALI.

LAKINI MKUU WA MKOA KAFIKA LEO NA KURUHUSU UENDELEE KUPITA HAPO. HIVYO KATENGUA MAAGIZO YA SERIKALI YALIYOTOLEWA KWA MAANDISHI KWA MDOMO WALA SIO OFFICIAL DOCUMENT TOKA OFISI YA MKUU WA MKOA.

SHIGELLA ACHUNGUZWE KATIKA HILI. KWANZA ALIKUWA NA DHARURA GANI HADI KUWAHI KUFANYA HAYO SIKU YA WEEKEND?
 

Attachments

  • STAKABADHI ZA GHALA.pdf
    367.8 KB · Views: 11
Waziri wa Kilimo hayupo? Bashe yupo mpigie simu au nenda ukurasa wao rasmi katoe malalamiko..
Taarifa hizi zitamfikia. Ila jua Bashe pia ni mfanyabiashara wa mazao. Mwaka jana alipiga maarufu uuzaji wa choroko mkoa wa Tabora kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na akatuma watu wake wamnunulie hizo choroko na kahifadhi katika Maghala ya mtu mmoja huko Tabora.
 
Taarifa hizi zitamfikia. Ila jua Bashe pia ni mfanyabiashara wa mazao. Mwaka jana alipiga maarufu uuzaji wa choroko mkoa wa Tabora kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na akatuma watu wake wamnunulie hizo choroko na kahifadhi katika Maghala ya mtu mmoja huko Tabora.
Tuhuma hazina ushahidi
 
Songwe Ufuta umeuzwa kwa 2877 kwa kilo. Walanguzi 800 hadi 1600. Bila shaka wewe ni dalali wa wahindi unayefaidika na hizi hujuma.
Ungekuwa unajua maana yake usingeandika huu ugolo.
1. Mfumo unahitaji ushirika wa hiari. Je wakulima hao wamejiunga kwa hiari?
2. Mfumo unataka wanaushirika wakusanye mazao yao ili wauze. Je wakulima wote wanaolazimishwa ni wanaushirika?.
3. Kama ni mwanaushirika nani amekuzuia kukusanya wewe na wenzako mliojiunga kwenye amcos yenu na kuuza?
4. Kwanini unalazimisha mkulima asiye mwanaushirika wenu naye auze mtakavyo nyinyi?
Wewe utakuwa kiongozi wa amcos madalali waliojisajili kununua kwa wakulima na kuuza kwa makampuni kwa kisingizio cha ushirika. Kwa taarifa yako cheza vzr utaenda na maji.
(i) Tutasajili wakulima mashamba yao na kiasi cha mazao ambacho kila mkulima anategemea kupata kwa msimu. Wewe nunua mwakani uje na mazao ya heka 10 wakati una heka moja tutapita na ongezeko maana umemlangua mkulima fulani hizo heka 9.
Nenda usome mwongozo wa ushirika na stakabadhi ghalani

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Ungekuwa unajua maana yake usingeandika huu ugolo.
1. Mfumo unahitaji ushirika wa hiari. Je wakulima hao wamejiunga kwa hiari?
2. Mfumo unataka wanaushirika wakusanye mazao yao ili wauze. Je wakulima wote wanaolazimishwa ni wanaushirika?.
3. Kama ni mwanaushirika nani amekuzuia kukusanya wewe na wenzako mliojiunga kwenye amcos yenu na kuuza?
4. Kwanini unalazimisha mkulima asiye mwanaushirika wenu naye auze mtakavyo nyinyi?
Wewe utakuwa kiongozi wa amcos madalali waliojisajili kununua kwa wakulima na kuuza kwa makampuni kwa kisingizio cha ushirika. Kwa taarifa yako cheza vzr utaenda na maji.
(i) Tutasajili wakulima mashamba yao na kiasi cha mazao ambacho kila mkulima anategemea kupata kwa msimu. Wewe nunua mwakani uje na mazao ya heka 10 wakati una heka moja tutapita na ongezeko maana umemlangua mkulima fulani hizo heka 9.
Nenda usome mwongozo wa ushirika na stakabadhi ghalani

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
Wakulima hawana tatizo. Kuna mtu ana tatizo na kupata bei kubwa ya mazao yake. Muongozo naujua.

Basi nikuulize wewe unayejua sana. Kama Ulanga na Morogoro Municipal wamekuwa wakiuza since 2019 je mwaka huu ndio hawana elimu?
 
Kweli hii awamu ya 6 ndio imeamua kurudisha nyuma juhudi zote za wakulima na kuruhusu wanyonyaji wachache waendelee kufaidika kupitia jasho la watanzania wanyonge?
Hivi wewe mleta mada unaumwa ugonjwa gani kichwani? Angalia usije kuwa na homa ya ngedere.

Hujui kuwa stakabadhi gharamni ni kuingilia uhuru wa mkulima wa kufanya biashara?

Mkulima anapaswa kusaidiwa kutunza shamba lkn siyo mazao. Yaani shamba atunze peke yake lkn mazao atunziwe kusubiri soko?
 
Hivi wewe mleta mada unaumwa ugonjwa gani kichwani? Angalia usike kuwa na homa ya ngedere.

Hujui kuwa stakabadhi gharamni ni kuingilia uhuru wa mkulima wa kufanya biashara?

Mkulima anapaswa kusaidiwa kutunza shamba lkn siyo mazao. Yaani shamba atunze peke yake lkn mazao atunziwe kusubiri soko?
Nafikiri uelewa wako ni mdogo sana. Maana ya huu mfumo ni kumsaidia mkulima apate soko la uhakika na kwa bei nzuri.

Mfano zao la kakao. Kabla ya ushirika mkulima alikuwa anauza kati ya 1000 hadi 2500 top. Hivi sasa kupitia stakabadhi ghalani bei elekezi ya Serikali ni 4200 na katika hiyo minada hufikia hadi 5000
 
Hivi wewe mleta mada unaumwa ugonjwa gani kichwani? Angalia usije kuwa na homa ya ngedere.

Hujui kuwa stakabadhi gharamni ni kuingilia uhuru wa mkulima wa kufanya biashara?

Mkulima anapaswa kusaidiwa kutunza shamba lkn siyo mazao. Yaani shamba atunze peke yake lkn mazao atunziwe kusubiri soko?
Huenda haujui maana ya stakabadhi ghalani. Unaachosema wewe kifanyike ndio kitamuuza zaidi mkulima maana walanguzi wataingilia soko na watakubaliana kununua kwa bei ya chini sana
 
Huenda haujui maana ya stakabadhi ghalani. Unaachosema wewe kifanyike ndio kitamuuza zaidi mkulima maana walanguzi wataingilia soko na watakubaliana kununua kwa bei ya chini sana
Ni kweli ulichomjibu. Wanunuzi wanakaa chini kwa pamoja wanakubaliana tutanunua kwa bei hii kisha hawapandishi bei . Wakulima mtakaza baadae mtauza maana wanakuwa hawana wa kuwatetea. Mtetezi ambaye ni serikali kupitia watumishi wasio jali maslahi ya wakulima wanachukua rushwa na kumuumiza mkulima. Na matokeo yake watu wanapunguza uzalishaji maana hawajapata faida.
 
Maagizo ya Mkurugenzi ambayo leo yametenguliwa na Mkuu wa Mkoa.
 

Attachments

  • STAKABADHI ZA GHALA.pdf
    367.8 KB · Views: 4
UPDATES:

MKUU WA MKOA WA MOROGORO KAFIKA LEO KATIKA GETI AMBALO MKUU WA WILAYA ALITOA MAAGIZO KUWA UFUTA USIOPITIA KATIKA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI USIVUKE KWA MUJIBU WA MAAGIZO YA SERIKALI.

LAKINI MKUU WA MKOA KAFIKA LEO NA KURUHUSU UENDELEE KUPITA HAPO. HIVYO KATENGUA MAAGIZO YA SERIKALI YALIYOTOLEWA KWA MAANDISHI KWA MDOMO WALA SIO OFFICIAL DOCUMENT TOKA OFISI YA MKUU WA MKOA.

SHIGELLA ACHUNGUZWE KATIKA HILI. KWANZA ALIKUWA NA DHARURA GANI HADI KUWAHI KUFANYA HAYO SIKU YA WEEKEND?
 
Stakabadhi gharani ni udalali yaani ingekua inatoka cash sawa, lakini mtu anashida hadi akukopeshe wewe chama cha ushirika unaesimama kama dalali hapana big no huko tulishatoka kalima apate chake chapchap mambo yaishe
 
Hiyo stakabadhi ghalani ina manufaa gani kwa mkulima??
UPDATES:

MKUU WA MKOA WA MOROGORO KAFIKA LEO KATIKA GETI AMBALO MKUU WA WILAYA ALITOA MAAGIZO KUWA UFUTA USIOPITIA KATIKA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI USIVUKE KWA MUJIBU WA MAAGIZO YA SERIKALI.

LAKINI MKUU WA MKOA KAFIKA LEO NA KURUHUSU UENDELEE KUPITA HAPO. HIVYO KATENGUA MAAGIZO YA SERIKALI YALIYOTOLEWA KWA MAANDISHI KWA MDOMO WALA SIO OFFICIAL DOCUMENT TOKA OFISI YA MKUU WA MKOA.

SHIGELLA ACHUNGUZWE KATIKA HILI. KWANZA ALIKUWA NA DHARURA GANI HADI KUWAHI KUFANYA HAYO SIKU YA WEEKEND?
 
Ninyi watu wa ushirika limeni mazao yenu ndio muweke huo mfumo wenu kwenye mazao yenu mnajifanya kutetea mkulima ilihali nanyi wapigaji tu maana ni madalali ambao toka mtu anaandaa shamba, anapanda, parizi hampo mnajifokeza kwenye kuuza huo ujinga haupo dunia ya leo
 
Back
Top Bottom