Morogoro Mjini: Abood atawasaidia nini bungeni?

charity begins at home ukitaka kujua abood atawasaidia wana moro nenda viwandani mwake wafanyakazi manyanyaso hayakomi! nafikiri hoja ya msingi hapo si waluguru ni udini umeshamiri sana morogoro so walisahau manyanyaso ya ndugu abood kiwandani kwa wafanyakazi wake na kutazama anaabudu wapi msikitini au kanisani? siasa za udini morogoro hazitatufikisha popote!
 
Mimi nimesikitishwa sana na wananchi na wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa kuchagua mwarabu (Aziz Abood) awe mbunge ili hali tunajua kabisa walitutesa wakati wa ukoloni, wametuibia sana na hawalipi kodi.

Warguru mnamatatizo gani??? au ni kutokuwa na elimu????

CHA KUSIKITISHA NI KWAMBA BADO KUNA WATU WABAGUZI KAMA WEWE. Yani wewe unam assess mtu kwa skin color?. kwa tarrifa yako hii nchi ya watanzania wote bila kujali uarabu, uhindi au uzungu. inabidi uelimike na uachane na racism. ni watanzania wangapi weusi wanalipa kodi kati ya watz milioni 40? au wanaoiibia nchi yao hata leo?. ukoloni?!!!!! tufike nmahali tuache visingizio, sawa ukoloni ulikuwepo .

Sasa miaka 40 bila ukoloni mmefanya nini? ulishawahi kusikia waisrael wakilalamika wao ni masikini kwa sasabu hitler aliwaua wenzao milioni sita?

Uchochezi huo si mzuri.
 
Actually mimi sifagilii huu ubaguzi ila kwenye ukweli uongo hujitenga. Ni bora mwarabu kuliko muhindi mara dufu. Waarabu wengi wana kitu kinaitwa altruism - is selfless concern for the welfare of others, mfano pale Tabora alikuwepo mtu anaitwa S M Said, nafikiri alifirisiwa baada ya kuwa anawaunga mkono CUF wakampiga tax mpaka ya kuvuta hewa, huyu jamaa alikuwa na roho ya pekee yaani ukifika mfungo pale dukani kwake utakuta kuna msururu wa watu wanasubiri hela ya futari.

Yaani hawa wanafanya kazi kwa misingi ya kutoa zaka, Ila wahindi sijui kama wana hiyo kitu. Sasa ukija kwenye suala hili utaona kuwa Mikoa yote yenye majority ya watu wenye dini ya kiislam wanakuwa connected na hii kitu, hivyo wao kumpatia kura mtu kama huyo ni sehemu ya utamaduni wao wa dini yao ambayo inatamka wazi kuwa thamani ya mtu si rangi yake wala fedha zake bali ni uchamungu wake.

Kwa hiyo tusiziangalie kura hizi kwa misingi ya uarabu, ubantu na uhindi bali kuna mambo mengi sana yanawafanya watu kumchagua mtu kama nilivyoeleza hapo juu.

Marehemu bibi alikuwa na usemi mmoja kuwa ukiwa na roho ya kitumwa basi hata haki yako wewe utaiona ni hisani, ninahisi watu wengi wa mikoa hii pia wanaangukia kwenye usemi huu, hawa wahindi na waarabu wanachowafanyia watu kwenye mikoa hii ni kujifanya na wao ni sehemu yao kwa ama kuhudhuria misiba au kutoa misaada kwa kutumia hela walizokwepea kodi
 
Mwandishi wa thread hii anaonyesha madhaifu makubwa sana. kwanza aidha ni mjinga wa historia au ni mdini au ana chuki zake na Azizi Abood.

ukiwa ni mtaalamu wa historia huhitaji kufahamu kuwa wakoloni wa awali east africa walikuwa wareno ambao walitutawala baina ya karne ya 14 mpaka ya 16 kabla ya wareno hawa kufurushwa na waarabu. lakini je waarabu pekee ndio walihusika na biashara ya utumwa? jibu si kweli, wareno walihusika kwa kiwango kikubwa na utumwa ule wa trans-atlantic trade, vilevile kumbuka waarabu hawa walikuwa wakinunua watumwa kutoka kwa viongozi wa kiafrika ambao leo hii sisi huwa tunawaita mashujaa, je wafahamu kuwa mirambo alihusika sana na biashara ya utumwa?

Alikuwa mwarabu huyu? Biashara ya utumwa inaonekana katika biblia ambayo ninyi mwaona kuwa ni kiongozo chenu, yusufu aliuzwa na nduguze huko mosri vipi hawa nduguze walikuwa waarabu? Ibrahimu hakumiliki watumwa? mbona biblia tena agano jipya waefeso 6:5 inatetea utumwa?je wakristo hawa na huyu paulo ni mwarabu?basi twaweza semawaarabu hawa walikuwa wakinunua watumwa kuwapelekea wakristo walioruhusiwa kumiliki watumwa

lakini kwa kuwa hayo yote ni upuuzi sikupata kufikiria kuwa wananchi wa mpanda kati waliomchagua said amour arfi wa chadema awe mbunge wao kumbe walikuwa wajinga sana. vipi kuhusu yule gulam wa nccr aliyekuwa mbunge kule kigoma alichaguliwa na majuha?vilevile halmashauri kuu yote ya chadema iliyomchgua said amour arfi awe makamu wa chama hicho ni wajinga na majuha makubwa? vipi wananchi kutoka wilaya zinazosadikiwa kuwa ndizo zenye wasomi kuliko wote tanzania(vigezo?) za ilala , kinondoni na kawe zilizopata kuwachagua adamjee, mussa azzan na idd azzan ,je wananchi hawa ni wajinga ? mifano inaendelea na kuendelea

Muhimu tuweke ubaguzi kando, ila tuweke utanzania mbele, nani aliyekwambia kuwa watu weusi ndio wana upendo zaidi kwetu?huyu chenge anayelalamikiwa ni mwarabu?vipi lowasa, mramba , mkapa, anna mkapa, na mafisadi kadha wa kadha wenye rangi nyeusi na majina ya kikristo unayoyajua hawa wote ni waarabu? it is very pathetic kuona mtu anakaa kwenye kompyuta na kuanza kuandika threads zenye mwelekeo wa kibaguzi halafu anajiita yeye ana roho njema moyoni

I'm very dissapointed with the thread writer lakini siwezi kumlaumu ni upeo finyu alionao ndio unaomsababishia kuandika up[uzi huu
 
Mimi nimesikitishwa sana na wananchi na wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa kuchagua mwarabu (Aziz Abood) awe mbunge ili hali tunajua kabisa walitutesa wakati wa ukoloni, wametuibia sana na hawalipi kodi.

Warguru mnamatatizo gani??? au ni kutokuwa na elimu????

Na hao waliokuwa wakiwamata na kuwauza kwa hao waarabu ni kina nani kama sio mababu zenu waliokuwa machifu na vibaraka vyao? Na hao weusi waliojaa marekani wameuzwa na waarabu?

Au una ubia na yule aliyeshindwa ubunge ambaye nadhani ni Professa vile! Jee ingekuwa huko kwenu kagera mtu kama Mruguru au Mpogoro nae angeweza kushinda huo uchaguzi wakati mumejaa ubaguzi na nyinyi?

Suali la utumwa lina historia ndefu ambayo mtu hutoa sentensi moja na kuichakachua halafu akajifanya yeye ndiye mtaalamu wa kuanza kulaumu wenzake.

Kuunganisha uarabu na biashara ya utumwa iliyofanyika miaka mia moja nyuma hamumtendei haki huyo Abood. Kwa hivyo uwachukie hata hao mababu zako waliokuwa wanauza hao watu. Si ajabu na yeye alikuwa mmoja wa vibaraka wa machifu aliyekuwa anakamata hao wenzake.

Vile vile suali la kunyanyasa watu huko viwandani jee muna uhakika na hilo? Na huko viwandani naona hata hao waafrika weusi pia wananyanyasa wenzao kwani mfanya biashara ye yote lengo lake ni kupata faida kubwa kila penye upenyo.

Wacheni chuki zisizokuwa na msingi.
 
Kunawatu wameumbwa na roho za kibaguzi na chuki zisizo na msingi. Hii Tanzania ina watu wa aina mbali mbali kurokana na ukoloni na inter marriages kati ya Wabantu wa TZ na Wahindi na Waarabu ambao wengiwao wapo mikoa ya Pwani ya Tanzania, Tabora(RA), Singida, Shinyanga, Kigoma n.k. Jamani wote hawa ni wa TZ tusiwape lebo za kibaguzi mf. mafisadi, Jee, kuna weusi wangapi wanatuhumiwa kwa ufisadi?
 
Asante bwana magezi kwa kuwakumbusha wananchi wa morogoro,kimsingi jimbo la morogoro mjini kwa mara ya kwanza limemchagua mbunge aliyepata ziro forest,asiye na uwezo wa kujenga na kutetea hoja,wamevunja historia,ni aibu kubwa
 
Tanzania si nchi ya kibaguzi lakini wapo watu wanaowabagua watanzania,dhambi ya ubaguzi haiwezi kuisha kwa kuinyamazia,kama kuna watanzania wenzetu ambao wameamua kuwa na shule zao,hospitali zao,wanapanda mabasi yao,hawachanganyiki na watanzania wenzao,hawajengi nyumba zao maeneo ya waswahili na wanapata huduma zao kutokana na rangi zao, lazima tuwakemee waziwazi,tunahitaji kuona wahindi na waarabu wa kitanzania wakinunua viwanja,wakijenga na kupanga nyumba moja na waswahili
 
Wakazi wa moro wamemlipa fadhila kisa huwa anawasaidia misibani! ki ukweli huyu bwana hata yeye mwenyewe kujieleza hajui sijui kama atafanya lolote huko bungeni
 
Atatusaidia sana, mwe... Mjomba, huoni mwenzio katusadia mabasi ya kwenda kuzika... kila tukifiwa basi... kila tukifiwa basi, sasa we wataka tumtose, kha...
 
Back
Top Bottom