Kwann alikubali kufanya nae kazi tena?!Mkuu..alisema kuwa aliwahi kucheza pambano na Mthailand ambapo Promota Siraji hakumalizia hela yake mpaka leo ndo maana alikosa imani naye
Kiufupi wanajuana watayamaliza tu ili wanawavuruga mashabiki..!
Uchochezi Wa kuni au?Kwa jinsi polisii walivyo sasa hawachelewi kusema jamaa anakabiliwa na kosa la uchochezi
Sio inagemea amei-frame kesi vipi? Anadai arudishiwe (madai)? Au anadai ametapeliwa/ibiwa (jinai)?Makosa ya kimkataba ...hayatatuliwi polisi
Breach of contract na polisi wapi na wapi...
Bondia Francis Cheka ashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro kwa kushindwa kulipa fidia ya shilingi milioni 28
Bondia huyo ambaye yuko rumande kwa sasa, anakabiliwa na kosa la kukataa kupanda ulingoni Desemba 25 dhidi ya Bondia Abdallah Pazi (Dulla Mbabe)
Kwa mujibu wa Promota wake, Kaiki Siraji, akifungua kesi katika Kituo cha polisi cha Kawe kwakuwa Cheka alimbadilikia dakika za mwisho wakati walikuwa na makubaliano kimkataba ulio kwa mujibu wa sheria za ngumi
Hata hivyo, Bondia Cheka atapelekwa Dar es salaam kesho akiwa chini ya ulinzi kwa ajili ya kesi hiyo katika kituo cha Kawe ambako kesi ilifunguliwa Desemba 25.
Chanzo: Mtanzania
Lakini mwisho wa siku hiyo ni contractual, ambapo upande mmoja umeshindwa ku comply na terms na hivyo mwisho wa siku atapaswa kulipa na riba, only kama akipata watetez wazuri watapangua hoja ya kujipatia pesa kwa udanganyifu.Wanachofanya wanabadilisha kesi. Inakua kujipatia hela kwa njia ya udanganyifu. Ukinyoosha mkono hata mdaiwa anafungwa. Only tz
Lakini mwisho wa siku hiyo ni contractual, ambapo upande mmoja umeshindwa ku comply na terms na hivyo mwisho wa siku atapaswa kulipa na riba, only kama akipata watetez wazuri watapangua hoja ya kujipatia pesa kwa udanganyifu.
Bado hiyo sio sababu ya kumpeleka polisi. Angemfungulia kesi ya madai. Cheka anachohitaji ni Mwanasheria tu. Tena akipelekwa mahakamani anaweza kushinda na aliyemshtaki akapoteza kila kitu.Kwa mujibu wa Promota Siraji ni kuwa alipewa pesa za mwanzo, ambapo zingine angemaliziwa kabla ya kupanda ulingoni kama inavyokuwa wameahidiana ambapo Cheka alionyesha kutokuwa na imani na mpango huo