hatimaye imekubali kwenye laptop! Nilichofanya nimetumia dashboard ya airtel. nilichomeka modem ya airtel huawei e153, na nikachomoa na kuchomeka ya ttcl. Sikuamini macho yangu nilipoona maandishi ''cdma'' pale kwenye sehemu ya kuonesha signal ambako siku zote palikuwa plain. Kwa kuwa hii imtokea kwenye d'board ya airttel, niliamua kurestart na kuclick icon ya ttcl. dashboard ya ttcl ikadisplay na yale maandishi ya ''cdma'' yakajitokeza kuashiria sasa signal inapatikana, na nilipojaribu kuconnect ikakubali.
Nakushukuru wewe na wote mlionisaidia katika kutatua tatizo hili. Nimejifunza mengi pia.
Modem ni ya ttcl, huawei ec 122; os ni windows xp; location: kigamboni-dar.
Asanteni sana.