Mnyika: Sina mpango wa kuhama CHADEMA

Mnyika: Sina mpango wa kuhama CHADEMA

Title ya thread ingekuwa hivi:
Mwananchi yamsaidia Mnyika kukanusha tetesi za kuhama Chadema!!
 
Sidhani kama mnyika atakubali yamkute yaliyomkuta Machali!
 
Kwa Taifa la TANZANIA lilipo sasa hv ushabiki wa vyama si tija kwa nchi tena. Viongozi wa focus kwenye matatizo ya wananchi na waache ushabiki uchwara wa vyama.

Ushabiki wa vyama ndo unazidi kudidimiza Taifa la Tanzania. Watu hawaangalii tena ni hoja ipi yenye nguvu ikubalike kuivusha Tanzania kwenda mbele wamebakia kushabikia vyama tu.

Leo hii kiongozi wa CCM akitoa hoja yenye nguvu inayoweza kuvusha Tanzania kwenda mbele basi kwa kuwa kaitoa mtu wa CCM upinzani kwa nguvu zote watapinga. Leo kiongozi wa UPINZANI akitoa hoja yenye nguvu ya kuwezesha kuleta maendeleo kwa wananchi basi kwa kuwa imetolewa na UPINZANI viongozi wote wa CCM. wataipinga kwa nguvu zote kwa sababu tu imetolewa na UPINZANI.

Huu ni upofu wa akili, sijui wamelogwa🙁🙁. Sisi kama watanzania hatuhitaji kujua ni CCM au ni UKAWA wamefanya tunahitaji maendeleo kwa Watanzania. Ukisikiliza mijadala inayoendelea bungeni sometimes ungekuwa na uwezo unaweza chapa watu bakora.

Jamani tushikane kwa pamoja tuendeleze Taifa letu. Tuacheni ushabiki usio na maana wa kuleta siasa kwenye kazi. Taifa hili halitajengwa kwa migawanyiko ya kisiasa, tutapiga hatua na kusonga mbele tu kwa kushikana pamoja katika umoja wa kweli. Tukatae mabaya na yale mazuri ya kutuvusha mbele tuyashikilie kwa pamoja kama TAIFA tusonge mbele, tusibaguane kwa vyama, udini, ukanda au ukabila. Haya mambo yatalibomoa Taifa na hatutafika popote.

Chama changu ni UTANZANIA, kwa umoja tutafika.
Well said. ....
 
Title ya thread ingekuwa hivi:
Mwananchi yamsaidia Mnyika kukanusha tetesi za kuhama Chadema!!
Au

Ndugu Jingalao Alazimisha Kusikia Mnyika Anahama CDM.

Kwa sababu either of the two,hakuna lenye tija kwa Taifa!

Kila siku watu ni uvyama uvyama inakera sana. Maslahi mapsna ya Taifa, Sera za Taifa hazizungumzwi badala yake ni issue Personal, Itikadi za vyama na bla bla kibao.
 
Siasa zina "timing" zake mahakama ya mafisadi ndio itasababisha upepo wa Siasa ubadilike.

Subirini watu wapandishwe kizimbani ndio hapo mtajua mbivu na mbichi
 
Tunaomba akanushe na zile tetesi zinazosema hakubaliani na ujio wa Lowasa ili tumweke kwenye kundi la kina Msigwa.
 
Nilikuwa najiuliza kuwa angetokea mtu kuzusha kuwa John Pombe Joseph Magufuli ndiye "time bomb" linalosubiri kulipuka huko CCM kwa kuhama badala ya John Mnyika wa CHADEMA, nadhani ingeaminika zaidi eti kuliko huu uzushi unaoenea kumhusu JJM.....

I think, that makes more sense than this!

I don't get it kwa uzushi wa wazee wa propaganda wa CCM wakisaidiwa na wale wa "kitengo maalumu" wa serikali chini ya serikali, kwamba lengo lao ni nini hasa.....kuiua CHADEMA siyo?

Lakini binafsi, I hope watashindwa ile mbaya kwa sbb wakati wa J.K Mrisho nguvu iliyowekezwaga kukiua hiki chama ililuwa ni kubwa na iliyopangiliwa zaidi kuliko mbinu za hawa "washamba" wa sasa ambao mikakati yao wanaipanga wakati wa mchana wa jua kali huku kila mtu akiona!!
 
Naibu Katiba Mkuu wa Chadema, John Mnyika amekanusha taarifa zinazodai kuwa anataka kuachana na chama hicho.

Mnyika amesema hayo jana alipopigiwa simu ili azungumzie taarifa hizo. Mbunge huyo wa Kibamba amesisitiza kwamba huo ni uzushi.

“Hakuna kitu kama hicho na wala sina mpango wa kuhama,” amesema.

Habari za kujiuzulu kwa Mnyika zilianza kusambaa katika vyombo vya habari kwa mara ya kwanza mwaka 2013 baada ya aliyekuwa naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kufukuzwa uanachama.

Uvumi ulienea kwenye mitando kwamba amejivua nyadhifa zake zote na kwamba ameshakabidhi barua yake kwa katibu mkuu wakati huo, Dk Willibrod Slaa.

Chanzo:Mwananchi online

We ndugu kuna Uzi kule kuhusu tamko la Boss wenu Lowassa kuwataka muacheni issue za uhanarakati ili muwe chama cha siasa, wewe huonekani kumbe umejificha huku.

Haya nenda kule haraka,unahitajika
 
Kila jambo linaanza na tetesi
Nyie vijana wa lumumba hukumu yenu kutoka kwa mungu itakuwa kubwa sana,mnakaa na kumzushia mtu mambo ya ajabu?mtalaaniwa sana nyie
 
Hata Dr. Slaa na Prof. Lipumba hawakuhama vyama. Mnyika ni rafiki yangu. Ninachojua ni kwamba John Mnyika na Halima Mdee wanaenda ACT-Wazalendo ambapo anaenda kuwa GS. It's a matter of time.
Wana uhuru wao wa kuchagua,wacha kuwasemea unakuwa kama zuzu tu mitandaoni kwani wakihama wao ndio watakuwa wakwanza kuhama chama cha siasa?
 
Mnyika anaondoka
Na naunga mkono sababu CHADEMA imepoteza dira
Bali ccm ndio imeiokota hiyo dira siyo?dira ya kutuuzia sukari kilo moja sh 4000?dira ya kuyafanya mafuta ya taa kuwa ni almasi?dira ya kutuongezea kodi kwenye miamala ya fedha siyo?dira ya kununua vivuko vibovu kwa mabilioni siyo?
 
Back
Top Bottom