Mnyika kinara bungeni

Mnyika kinara bungeni

Mnyika kinara wa Mwongozo spika, mpaka spika anamwambia kaa chini...Mnyika onyesha ukinara wako kwa kuleta maji Ubungo, Kimara njia mbovu njia azipitiki Kimara Bonyokwa, Kimara Temboni.
 
hiyo ndiyo CDM kila kona kuna jembe la ukweli, big sana ndg yetu Mnyika
 
sasa kumbe watu mnapenda kuongopewa eeh! manake mimi ni miongoni mwa watu ambao niliwah kusema mnyika anataka kudumaa kisaisa kwa hli jimbo. na wakati nasema nilionekana niviroba lkn wachambuzi wa siasa walisema ni kweli.hatuwez kumtegemea amalize haya yote kwa mara mja ila kule alikofanya apewe hongera zake na siyo kuonekana kana kwamba hajatend kabisa.
Kumbe kazi za mbunge ni kuleta maji, kuchimba barabara, kujenga hospitali? Rejeeni wajibu na majukumu ya Mbunge hakuna hayo mnayo jadili, Kazi yake ni kutungasheria na kuisimaamia serikakali kuelekeza rasilimali za jimbo na nchi katika kuwaletea maendeleao wananchi kwa kujenga barabara, hospitali, na shele badala ya kuzipeleka Uswisi.
 
big up Mnyika umejitahd sana. lakin je wafikiri ni kwanini hawa wabunge wa CDM wameweza kufikia hapo?
Simple.
Wanajali
Wanajua wajibu wao
Wana Kiu ya Maendeleo
Wana akili kuliko wabunge wa CCM
Bidii
Weredi wa Kujenga hoja
n.k
 
Kimbunga mbona unakuwa na roho ya kijicho dhidi ya Mnyika?
Mkuu mbona unachekesha walionuna, kwamba temeke iko juu ya ubungo, kwa kitu gani?
Unawezaje kulinganisha utumishi wa Mnyika wa miaka miwili na nusu dhidi ya miaka kumi ya keenja? Kitu gani alichofanya keenja unachoweza kukitaja kama mafanikio dhidi ya mnyika?
Mara moja moja ujitahidi kuficha chuki zako zisizo na msingi wowote. Kazi aliyoifanya Mnyika katika kipindi hiki kifupi hakuna mbunge yeyote wa ccm aliyemfikia.

Aliyofanya yapi ebu yaweke humu jamvini tuyaone sio maneno matupu.
 
Last edited by a moderator:
Barabara za Kilungule ni dhoflihali! Bonyokwa hakuendeki, King'ong'o hakuna njia, Ubungo Kibangu shida!

Serikali ya magamba haiwezi kuboresha huduma kwenye majimbo ya wapinzani mpaka wananchi msaidiane na mbunge wenu kuibana serikali hii ya dhaifu!

Hivi wewe kama mkazi wa maeneo hayo, kwenye yale maandamano ya kudai maji ulikuwepo? Au kazi yako ni kubofya baobonye hapa JF na kulalamika? Bila wananchi kushirikiana na mbunge wenu kuishinikiza serikali, mtamlaumu tu kijana japo anafanya kila lililo ndani ya uwezo wake laikini ccm kamwe hawawezi kufanya yale anayoyalalamikia mbunge wa upinzani!
 
Kigoma ikiwa Dubai itamsaidia nini Mnyika akija kuomba kura. Wakati anatuahidi kushughulikia kero ikiwemo hiyo bara bara alikuwa kalewa?

najua unajua unajidai hujui, kazi ya mbunge si kujenga barabara kwa sababu hana chanzo chochote cha mapato, kujenga barabara na huduma nyingine ni kazi ya serikali, na mnyika kama mbunge ni kuzifikisha kero kama hiyo ya kilungule kunako husika (serikalini) na ndio anachofanya na kama hawazifanyii kazi ni tatizo lao serikali.
 
humu jamvini watu wanajaribu kupotosha kazi za wabunge, hivi mnapotaka wabunge wafanye kazi za serikali, serikali itafanya nini, mnyika na baadhi ya wabunge wa cdm wanafanya kazi za kibunge sawasawa na hata baadhi ya wabunge wa ccm km mbina, filikunjombe wanafanya vizuri, kazi ya mbunge sio kujenga barabara au kuleta maji kazi yake ni kuzifikisha kero hizo kwa serikali ambao ndo watendaji coz ndo wanakusanya mapato!
 
Kazi ya mbunge ni kuwakilisha wananchi jimbo kwake na tz kwa ujumla ila la muhimu kabisa kuliko yote ni kuisimamia serikali na kutunga sheria
kwa sasa kazi ya kuisimamia serikali imeshapokwa na mafisadi hoja za muhimu zinaminywa mfano waziri kasema bungeni kwamba nguzo za tanesko walikuwa wanachakachuwa sio za south ingekuwa ni bunge kweli spika angehoji lakini wapi wamejimagamba kimyaaaaa.
pesa zipo uswis nilimuona ndugai tbc akisema ni vipesa vidogo tu eti watu wanakuza nyingi ni za kenya lakini takwimu zilizopo zinaonesha ni mahela mengi


hongera mnyika kaza uzi acha wabunge wa ccm waendelee kula rushwa kwenye kamati na uchaguzi
 
Anaonewa vipi wakati yeye kinara? Hivi vijisababu eti Keenja kakaa miaka mingapi ni vya kisengelema. Siku tukiwapa nchi CDM watakuja na majibu hayo hayo CCM imekaa miaka 50. Wakati anaomba kura Mnyika alisema ataondoa hizi kero na akirudi atapimwa kwa hilo sio idadi ya miongozo ya spika.

Kwani Mnyika ndio waziri wa Ujenzi muulize Magufuli akupe majibu, hizi barabara kila siku mnyika anapiga kelele na tunaona kama mnataka akachimbe mwenyewe mseme.
 
Hongera wabunge wa Chadema,Hongera wabunge wapambanaji....Tutafika tu!
 
Kumbe kazi za mbunge ni kuleta maji, kuchimba barabara, kujenga hospitali? Rejeeni wajibu na majukumu ya Mbunge hakuna hayo mnayo jadili, Kazi yake ni kutungasheria na kuisimaamia serikakali kuelekeza rasilimali za jimbo na nchi katika kuwaletea maendeleao wananchi kwa kujenga barabara, hospitali, na shele badala ya kuzipeleka Uswisi.

Tatizo ni ahadi. Kama siyo kazi yao kwa nini alitoa ahadi?
 
Serikali ya magamba haiwezi kuboresha huduma kwenye majimbo ya wapinzani mpaka wananchi msaidiane na mbunge wenu kuibana serikali hii ya dhaifu!

Hivi wewe kama mkazi wa maeneo hayo, kwenye yale maandamano ya kudai maji ulikuwepo? Au kazi yako ni kubofya baobonye hapa JF na kulalamika? Bila wananchi kushirikiana na mbunge wenu kuishinikiza serikali, mtamlaumu tu kijana japo anafanya kila lililo ndani ya uwezo wake laikini ccm kamwe hawawezi kufanya yale anayoyalalamikia mbunge wa upinzani!

Niandamane ili iweje badala ya Mbunge wangu kuwabana Bungeni kama anavyofanya kwenye miongozo na jinsi alivyobadili kile kifungu kwenye mambo ya bandari. Kwani Ukinara wake Bungeni ni kwa kuandamana au kwa hoja? Kwa nini useme niandamane badala ya kutumia hoja hadi kieleweke kama anavyotumia hoja bungeni?
 
Back
Top Bottom