MNYIKA: Katiba mpya 2025 tumechelewa

MNYIKA: Katiba mpya 2025 tumechelewa

..tatizo mmewabwagia Cdm suala la Katiba Mpya mnasubiri wawafanyie.

..Ccm ina-behave vibaya kwasababu Watz hatujaamka.

..Watz wakiwaunga mkono kwa dhati wapinzani Ccm itajirekebisha.

..Tujiulize nchi ambazo zilidai mabadiliko na Katiba Mpya na wakafanikiwa, wananchi wake wali-behave kama tunavyo-behave Watanzania?
Mkuu umeuliza swali muhimu mno, kwa heshima naomba nimualike ndugu Pasko Mayalla kama mwana Habari nguli, mwanasheria mahiri na mchambuzi wa masuala ya kisiasa mzoefu aje watupe madini juu ya hili swali!
 
Hapana ,Mnyika hana hoja kabisa

Mwaka 2021 kulikuwa na pressure iliyozaa matunda ya kupatikana Katiba mpya.
In fact ilikuwa ni shinikizo Rasimu ya Warioba ianze kufanyiwa kazi na ingewezekana katika miaka 2

Chadema naweza kusema Vijana wao walikuwa active hata pale Mwenyekiti Mbowe alipokuwa magereza.
Tuliwaona Vijana wao wakiongoza jitihada za Katiba mpya hata ndani ya viunga vya Mahakama .

Alipoachiwa Mbowe na kwenda Ikulu kabla ya kukutana na yoyote akafungwa mdomo kwa ' Maridhiano'

Ni Mbowe aliyeeneza dhana ya Maridhiano bila kueleza na nani na kwa makosa gani.
CCM hawakuzungumzia Maridhiano hata kidogo, ni Mbowe tu aliyefungwa mdomo kitapeli , akakubali

Mbowe alionywa na kutahadharishwa hakuna maridhiano na CCM, haijawahi na haitatokea
Mbowe akapoteza mwaka mzima , mwisho wa siku CCM wakapata nafasi waliyoitaka wakamwaga Mbowe Mazima

Kwahiyo suala la muda ni tatizo la Chadema na Mwenyekiti Mbowe.

Nikisikia wanataka marekebisho nawashangaa . Hivi Wabunge walioingia Bungeni kwa wizi wa kura na wengine kubebwa kama wale 19 , wanawezaje kufanya mabadiliko yatakayohakikisha haki!
kwamba wao hawajitaki! Dhana ya marekebisho ni ya kitoto isiyo na chembe ya siasa, ni ujinga tu

Licha ya kuungwa mkono na Umma, CDM imeshindwa kuwa na mikakati ya maana ! ni sawa na ACT wanaoshangilia ule mswada wa kitapeli uliopelekwa mjengo. ACT wanafurahia kabisa kwamba ni ukombozi!

..Tatizo liko Ccm, sio Chadema au kwa vyama vya upinzani.

..Kilichokwamisha kupatikana kwa Katiba Mpya, au Tume huru, ni nia ovu ya Ccm, na sio Mbowe kutafuta maridhiano.

..Na kilichompeleka Mbowe kwenye meza ya maridhiano ni tabia ya Watanzania kutokuwa na muamko wa kutafuta haki kwa kuitia msukosuko Ccm.

..Raisi Samia alikuja na falsafa ya 4R. Tumejiuliza falsafa hiyo imeishia wapo? Au tumeridhishwa na utekelezaji wake?
 
Mkuu umeuliza swali muhimu mno, kwa heshima naomba nimualike ndugu Pasko Mayalla kama mwana Habari nguli, mwanasheria mahiri na mchambuzi wa masuala ya kisiasa mzoefu aje watupe madini juu ya hili swali!

..huyo hawezi kukupa majibu yoyote ya maana.

..amejielekeza zaidi ktk kupumbaza vijana na kuwalinda walioko ktk mfumo.
 
..Tatizo liko Ccm, sio Chadema au kwa vyama vya upinzani.

..Kilichokwamisha kupatikana kwa Katiba Mpya, au Tume huru, ni nia ovu ya Ccm, na sio Mbowe kutafuta maridhiano.

..Na kilichompeleka Mbowe kwenye meza ya maridhiano ni tabia ya Watanzania kutokuwa na muamko wa kutafuta haki kwa kuitia msukosuko Ccm.

..Raisi Samia alikuja na falsafa ya 4R. Tumejiuliza falsafa hiyo imeishia wapo? Au tumeridhishwa na utekelezaji wake?
Na kilichowafanya wananchi kupoteza Imani zaidi na kuachana na siasa, ni suala la Lowassa aliyekuwa akiitwa fisadi na CDM, Kisha hao hao kumfanya mgombea wao.
 
..huyo hawezi kukupa majibu yoyote ya maana.

..amejielekeza zaidi ktk kupumbaza vijana na kuwalinda walioko ktk mfumo.
Mkuu tumpe muda, usipre - empt! With all due respect to you do not speak for him!
 
Mkuu wangu Nguruvi3 umezungumza kana kwamba swala la Katiba mpya halikuhusu kabisa, kana kwamba unaishi nchi tofauti na hii hii Tanzania yetu.

Kana kwamba hitaji la katiba mpya na ni swala la Chadema tu. Kana kwamba wao ndio wanaotakiwa kuidai katiba, kana kwamba wao ndio wenye haja na katiba tu.

Sio kweli!

Mkuu kwa kweli umepotosha sana na kutudanganya mchana kweupe. Katiba mpya ni dai na haki ya kila mwananchi na wewe ukiwemo!
Suala la Katiba ni letu sote.
Kumbuka mchakato mzima ni 'political process'. Chadema ni chama arguably kinaungwa mkono na wengi baada ya CCM. Kiongozi wa CDM si sawa na mtu baki. Kauli ya CDM si kauli ya wana VICOBA etc.

Bungeni, Mbowe alikuwa na nafasi katika usawa na Waziri mkuu.
CDM wanapokea ruzuku kwa ajili ya mambo ya sisasa ikiwemo hili tunaloongelea.
CDM wana nguvu za kisheria kuitisha mikutano, raia mwingine hana haki hiyo.
Kwa kutambua hilo hata Serikali iliamua kukaa kitako nao kwa maridhiano si mtu baki.

Yes sote tuna wajibu, lakini '' with great power comes great responsibilities''.
Ikiwa watakimbia majukumu yao ya asili ' kama chama cha upinzani, watakuwa wamepoteza sifa ya kuungwa mkono. Huwezi kuongoza ukiwa umejificha! CDM wanatakiwa kujenga imani, ni mbadala wa CCM.
 
Suala la Katiba ni letu sote.
Kumbuka mchakato mzima ni 'political process'. Chadema ni chama arguably kinaungwa mkono na wengi baada ya CCM. Kiongozi wa CDM si sawa na mtu baki. Kauli ya CDM si kauli ya wana VICOBA etc.

Bungeni, Mbowe alikuwa na nafasi katika usawa na Waziri mkuu.
CDM wanapokea ruzuku kwa ajili ya mambo ya sisasa ikiwemo hili yunaloongelea.
CDM wana nguvu za kisheria kuitisha mikutano, raia mwingine hana haki hiyo.
Kwa kutambua hilo hata Serikali iliamua kukaa kitako nao kwa maridhiano si mtu baki.

Yes sote tuna wajibu, lakini '' with great power comes great responsibilities''.
Ikiwa watakimbia majukumu yao ya asili ' kama chama cha upinzani, watakuwa wamepoteza sifa ya kuungwa mkono. Huwezi kuongoza ukiwa umejificha! CDM wanatakiwa kujenga imani, ni mbadala wa CCM.
🙏🙏🆒
 
..Tatizo liko Ccm, sio Chadema au kwa vyama vya upinzani.

..Kilichokwamisha kupatikana kwa Katiba Mpya, au Tume huru, ni nia ovu ya Ccm, na sio Mbowe kutafuta maridhiano.

..Na kilichompeleka Mbowe kwenye meza ya maridhiano ni tabia ya Watanzania kutokuwa na muamko wa kutafuta haki kwa kuitia msukosuko Ccm.

..Raisi Samia alikuja na falsafa ya 4R. Tumejiuliza falsafa hiyo imeishia wapo? Au tumeridhishwa na utekelezaji wake?
Mkuu ni ukweli usio na kificho hujuma za Katiba ni tatizo kutoka CCM kwa kila kona na hali.
Rais na 4R ilikuwa ni 'slogan' tu, tulijua hana nguvu.
JK alipoanzisha mchakato alipingwa na wahafidhina wa CCM wakauhujumu licha ya kwamba alikuwa Rais

Ni kweli pia kwamba mwamko wa Watanzania kutafuta haki ni tatizo, lakini pia ni ukweli kwamba kama hakuna mtu wa kubadilisha mtazamo huo, tatizo si wananchi bali ni kufeli kwa Viongozi.

Kwa viongozi wanaoelewa utawala, unapofeli 'misheni' unaachi ngazi kuwapa wenye mtazamo na uwezo tofauti.

Ndani ya CDM, Mbowe alipingwa(alikiri hili akiwa USA), ilikuwa kuamua kuendelea na maridhiano au la.

Jibu lilikuwa wazi, aachie ngazi kwasababu alifanya maamuzi mengi bila mafanikio.
Mfano, kwenda Mwanza kwa maridhiano na Magufuli. Kubadilisha na kuchukua makapi ya CCM kugombea uongozi.

Nina uhakika CDM wasingekuwa na maridhiano hali ingalikuwa tofauti.

Niliwaeleza hapa jamvini CCM wanapitisha muda ili kikosi kazi kifanye kazi ya kufuta rasimu ya Warioba na ku prolong mchakato. Hicho ndicho kimetoa.

Jambo la kushangaza na kuudhi , CDM ndio wanatetea upungufu wa muda na si CCM.

Kwa vigezo vyote Mbowe hakupaswa kufanya maridhiano. Kama hilo lingalikuwa gumu alikuwa na option ya kujiuzulu. Kufeli kote ni kwasababu yeye kama sehemu muhimu ya 'political process' alifeli.
 
Mkuu ni ukweli usio na kificho hujuma za Katiba ni tatizo kutoka CCM kwa kila kona na hali.
Rais na 4R ilikuwa ni 'slogan' tu, tulijua hana nguvu.
JK alipoanzisha mchakato alipingwa na wahafidhina wa CCM wakauhujumu licha ya kwamba alikuwa Rais

Ni kweli pia kwamba mwamko wa Watanzania kutafuta haki ni tatizo, lakini pia ni ukweli kwamba kama hakuna mtu wa kubadilisha mtazamo huo, tatizo si wananchi bali ni kufeli kwa Viongozi.

Kwa viongozi wanaoelewa utawala, unapofeli 'misheni' unaachi ngazi kuwapa wenye mtazamo na uwezo tofauti.

Ndani ya CDM, Mbowe alipingwa(alikiri hili akiwa USA), ilikuwa kuamua kuendelea na maridhiano au la.

Jibu lilikuwa wazi, aachie ngazi kwasababu alifanya maamuzi mengi bila mafanikio.
Mfano, kwenda Mwanza kwa maridhiano na Magufuli. Kubadilisha na kuchukua makapi ya CCM kugombea uongozi.

Nina uhakika CDM wasingekuwa na maridhiano hali ingalikuwa tofauti.

Niliwaeleza hapa jamvini CCM wanapitisha muda ili kikosi kazi kifanye kazi ya kufuta rasimu ya Warioba na ku prolong mchakato. Hicho ndicho kimetoa.

Jambo la kushangaza na kuudhi , CDM ndio wanatetea upungufu wa muda na si CCM.

Kwa vigezo vyote Mbowe hakupaswa kufanya maridhiano. Kama hilo lingalikuwa gumu alikuwa na option ya kujiuzulu. Kufeli kote ni kwasababu yeye kama sehemu muhimu ya 'political process' alifeli.
🆒👍👌👏🙏💐🎁
 
Zitto alishawaambia mpiganie kwanza tume huru ya uchaguzi mkaishia kumtukana leo hii bila aibu mnakiri katiba kwa sasa haiwezekani!!... nani aliwaloga CHADEMA? Au mlidhani wabunge wenu 19 wa viti maalum na mmoja wa kuchaguliwa ndo wangeweza kuwasaidia kwenye kupata katiba mpya?
Sikilizeni, alichokifanya Zitto si sawa.

Kwanza, alishiriki tume ya Mkandara akijua kabisa ulikuwa ni ulaghai wa kutafuta namna ya kufuta maoni ya Tume ya Warioba. Zitto alijua hilo lakini akaingia katika mchakato haramu kwasababu binafasi. Yes ni binafasi kwakuwa;
1. Rasimu ya Warioba ndio ilibeba maoni halali ya Watanzania. Hii ya Mkandara ilikuwa ya nini?
2. Zitto anajua ACT ambayo ni CUF ilikuwa katika GNU na kuwa na Tume huru. Matokeo yake tunayajua na Marehemu Jecha ameondoka na kuwaachia majonzi. Sababu za Tume huru ya CUF a.k.a ACT ya wakati huo kufeli ni Katiba
3. Huwezi kubadilisha vifungu vya Tume ya Uchaguzi bila kufumua vifungu vya Katiba. Nilipomuona ameenda Bungeni kushangilia mswada nilimshangaa sana, yaani ni kama 'amateur' Huwezi kuwa na Tume huru wakati Rais akiwa na nguvu juu ya tume hiyo

Hata hivyo Zitto anasukumwa na ACT Wazalendo waliofeli mara nyingi Zanzibar na kukubali nusu mkate.
Lakini madhara yake ni makubwa, ushiriki wa Zitto tume ya Mkandara ulitoa uhalali wa haramu hiyo.
Laiti asingeshiriki tusingekuwa na haya ya leo, akaunga mkono kwasababu tusizozijua. Ni felia tu kama hawa akina Mnyika
 
Sikilizeni, alichokifanya Zitto si sawa.

Kwanza, alishiriki tume ya Mkandara akijua kabisa ulikuwa ni ulaghai wa kutafuta namna ya kufuta maoni ya Tume ya Warioba. Zitto alijua hilo lakini akaingia katika mchakato haramu kwasababu binafasi. Yes ni binafasi kwakuwa;
1. Rasimu ya Warioba ndio ilibeba maoni halali ya Watanzania. Hii ya Mkandara ilikuwa ya nini?
2. Zitto anajua ACT ambayo ni CUF ilikuwa katika GNU na kuwa na Tume huru. Matokeo yake tunayajua na Marehemu Jecha ameondoka na kuwaachia majonzi. Sababu za Tume huru ya CUF a.k.a ACT ya wakati huo kufeli ni Katiba
3. Huwezi kubadilisha vifungu vya Tume ya Uchaguzi bila kufumua vifungu vya Katiba. Nilipomuona ameenda Bungeni kushangilia mswada nilimshangaa sana, yaani ni kama 'amateur' Huwezi kuwa na Tume huru wakati Rais akiwa na nguvu juu ya tume hiyo

Hata hivyo Zitto anasukumwa na ACT Wazalendo waliofeli mara nyingi Zanzibar na kukubali nusu mkate.
Lakini madhara yake ni makubwa, ushiriki wa Zitto tume ya Mkandara ulitoa uhalali wa haramu hiyo.
Laiti asingeshiriki tusingekuwa na haya ya leo, akaunga mkono kwasababu tusizozijua. Ni felia tu kama hawa akina Mnyika
🆒👍👌👏🙏💐🎁
 
Mkuu ni ukweli usio na kificho hujuma za Katiba ni tatizo kutoka CCM kwa kila kona na hali.
Rais na 4R ilikuwa ni 'slogan' tu, tulijua hana nguvu.
JK alipoanzisha mchakato alipingwa na wahafidhina wa CCM wakauhujumu licha ya kwamba alikuwa Rais

Ni kweli pia kwamba mwamko wa Watanzania kutafuta haki ni tatizo, lakini pia ni ukweli kwamba kama hakuna mtu wa kubadilisha mtazamo huo, tatizo si wananchi bali ni kufeli kwa Viongozi.

Kwa viongozi wanaoelewa utawala, unapofeli 'misheni' unaachi ngazi kuwapa wenye mtazamo na uwezo tofauti.

Ndani ya CDM, Mbowe alipingwa(alikiri hili akiwa USA), ilikuwa kuamua kuendelea na maridhiano au la.

Jibu lilikuwa wazi, aachie ngazi kwasababu alifanya maamuzi mengi bila mafanikio.
Mfano, kwenda Mwanza kwa maridhiano na Magufuli. Kubadilisha na kuchukua makapi ya CCM kugombea uongozi.

Nina uhakika CDM wasingekuwa na maridhiano hali ingalikuwa tofauti.

Niliwaeleza hapa jamvini CCM wanapitisha muda ili kikosi kazi kifanye kazi ya kufuta rasimu ya Warioba na ku prolong mchakato. Hicho ndicho kimetoa.

Jambo la kushangaza na kuudhi , CDM ndio wanatetea upungufu wa muda na si CCM.

Kwa vigezo vyote Mbowe hakupaswa kufanya maridhiano. Kama hilo lingalikuwa gumu alikuwa na option ya kujiuzulu. Kufeli kote ni kwasababu yeye kama sehemu muhimu ya 'political process' alifeli.

..Mnamlaumu Mbowe na Chadema bila sababu na hamko kiuhalisia.

..Majority ya Kamati Kuu ya Chadema walifungwa jela na Magufuli.

..Kwenye nchi zenye wananchi wanaojitambua serikali haiwezi kufanya uhuni wa kufunga wapinzani na wananchi wakakubali kama ilivyotokea kwa Mbowe na wenzake.

..Mbowe alikwenda kwenye maridhiano kwasababu huku kitaa hakuna watu wa kukinukisha. Tusubiri kizazi kingine lakini sio hiki cha Watanzania wa sasa hivi.

..Sikubaliani na wewe kwamba tatizo ni uongozi ktk vyama vya upinzani. Mimi nadhani Watanzania bado hatujapigika kisawasawa kiasi cha kuamua kutaka mabadiliko.

..Vilevile sikubaliani na wewe kwamba Cdm ndio watetezi wa kukosekana kwa muda wa kuleta Katiba mpya btn now and 2025.

..Nadhani wanaoilaumu Cdm kuhusu kuchelewa kwa Katiba Mpya ni watu waoga wasiotaka kukabiliana na Ccm.

..Jambo lingine ni Watanzania kupenda kutengeneza our own fake reality na kujifanya hatuoni tatizo, au kusukumia lawama kwa wasiohusika na tatizo.

..Katiba imekwamishwa na Ccm. Kuwalaumu Chadema ni kujifanya vichwa maji.
 
Na kilichowafanya wananchi kupoteza Imani zaidi na kuachana na siasa, ni suala la Lowassa aliyekuwa akiitwa fisadi na CDM, Kisha hao hao kumfanya mgombea wao.

..Nakubali kwamba wapo waliokatishwa tamaa na Chadema kumchukua Lowassa.

..Lakini kuna mambo mabaya zaidi ya kumchukua Lowassa yamefanywa na Ccm na hakuna reaction ya kutosha kuleta mabadiliko.

..Ni vizuri Watanzania tukajiuliza kama tumeonyesha kwa dhati kwamba tunataka Katiba Mpya. Au kama tunataka Tume Huru.
 
.Kwenye nchi zenye wananchi wanaojitambua serikali haiwezi kufanya uhuni wa kufunga wapinzani na wananchi wakakubali kama ilivyotokea kwa Mbowe na wenzake.
Watanzania ni watu peace sana, tunakubali kila kitu
Mbowe alikwenda kwenye maridhiano kwasababu huku kitaa hakuna watu wa kukinukisha. Tusubiri kizazi kingine lakini sio hiki cha Watanzania wa sasa hivi.
Watu peace huwa hawa kinukishi!
Jambo lingine ni Watanzania kupenda kutengenezwa our own fake reality na kujifanya hatuoni tatizo, au kusukumia lawama kwa wasiohusika na tatizo.
Hivi ndivyo tulivyo.
P
 
Ni kweli pia kwamba mwamko wa Watanzania kutafuta haki ni tatizo,
Mkuu Nguruvi3 , naunga mkono hoja kwamba mwamko wa Watanzania kutafuta haki ni tatizo, na kwa utafiti wangu, tatizo kubwa sio Watanzania hawajui kutafuta haki, bali Watanzania hawazijui haki zao!. Hawazijui haki zao kwasababu hawaijui katiba yao, na hawazijui sheria zao!. Hivyo kitu cha kwanza cha kuwasaidia Watanzania ni kuwaelimisha, elimu ya Katiba, Sheria, na haki, ili sasa ndipo wahamasishwe na wapate mwamko wa kuzidai haki zao.

Kwenye hili mimi nimejitolea kusaidia
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=mk9eDysfE-QeSJRP

Naombeni mniunge mkono, na ikitokea fursa kuwaita kushiriki katika kipindi, jitokezeni bila mimi kusema huyu ndiye Nguruvi3 au huyu ndiye JokaKuu
P
 
Ie ya warioba veepee?
..Ukiacha mchakato ya kuandika Katiba mpya, kuna zoezi la KURA YA MAONI kukubali au kuikataa.

..Pia kuna kipindi cha mpito kati ya kukubaliana kwa Katiba Mpya, na kuanza rasmi kuitumia.

..Watu wengi wanadhani Katiba Mpya inaandikwa tu, halafu tunaarifiwa kuwa Tanzania imepata Katiba Mpya.


..Mchakato unaweza kuanza, lakini realistically sio rahisi kupata Katiba Mpya kabla ya uchaguzi wa 2025.
 
Katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo ametoa kauli Jana kuwa mchakato wa kupata katiba mpya tayari jambo Hilo haliwezekani ! Ameomba kufanyike marekebisho yenye tija kwenye tume ya uchaguzi.

Mimi nachojiuliza MNYIKA anaposema tumechelewa anamaanisha yeye ndiye aliyechelewesha mchakato huo mbona anatamka maneno ya jumlajumla.


Ndugu zangu hivi vyama vya upinzani tunavyoamini tuviangalie kwa undani Zaidi kuna watu wanaamini kwamba hivi vyama vinaweza kuiondoa ccm kwenye box la Kura la hasha Hilo halitokuja kuwezekana Kwani vyama hivi ni vivuli kuwa Tanzania kuna upinzani , upinzani wa Tanzania ni kiini macho kuna watu wananeemeka kwa kuhadaa wananchi kuwa wanakosoa serikali.huku mlango wa nyuma wakila donge Nono la keki ya taifa.

Mara Lissu anasema bila Katiba mpya hakuna uchaguzi, chama cha ajabu sana. Kila mmoja ni kambare!
 
..Mnamlaumu Mbowe na Chadema bila sababu na hamko kiuhalisia.
Simlaumu Mbowe na CDM kwa suala la Katiba kama jukumu lao, hapana! Sikubaliani nao kwa 'approach' yao
Wanachama wengi wa CDM ni ''political capital'.
Wakati wa kesi yao, Tsh Milioni 300+ zilichangwa katika masaa 24 ikiwa ni testimony kwamba wana Umma.
..Majority ya Kamati Kuu ya Chadema walifungwa jela na Magufuli.
Michango ilikuwa ni clear message kwa Watawala kwamba kuna 'resentment' katika sehemu ya Jami
..Mbowe alikwenda kwenye maridhiano kwasababu huku kitaa hakuna watu wa kukinukisha. Tusubiri kizazi kingine lakini sio hiki cha Watanzania wa sasa hivi.
Hapa ndipo ninapomuona Mbowe ana makosa. Akiwa mahabusu harakati ziliendelea tena Mahakamani.
Watu waliimba Katiba mpya mbele ya Mahakama na Polisi. Ilikuwa 'courage' isiyo ya kawaida.

Mbowe kutoka tu hata kabla ya kukutana na watu wake akaenda Ikulu, kuanzia hapo kila jambo likapooza

Mkutano wa BAWACHA Iringa Wanawake walikula mihogo chini ya miti na kuhudhira kwa gharama zao..
Siku ile Mbowe hakuwa na la kusema! kwanini alikikmbilia Ikulu kwanza. 'political blunder !

Mbowe akiwa Marekani akasema kuna 'wahafidhina' katika chama chake, hatoki katika mariadhiano
M/kiti alijua maridhiano na CCM ni ndoto. CUF na ACT wakajaribu, yeye akajaribu na Magufuli. Mara zote matokeo yalikuwa ya hovyo.

Hazikuwepo dalili za kufanikiwa, mwisho wa siku walimmwaga mzima bila chembe ya ridhiano,
Mbowe kapoteza muda kuaminisha CDM kuna jambo! hajifunzi kutokana na makosa?

2025 msimamo ni kususia chaguzi. Ghafla Mbowe anawaambia Wanachama wajiandae kwa chaguzi.
Ni kana kwamba hana kumbu kumbu za nini kilitokea 2020 au ana matumaini feki bila kujua ni feki.

Nililtegemea CDM waongoze jitihada za kususia katiba kama walivyosusia Tume ya Mkandara.
Moja ya sababu za Mbowe kutolewa ni kutaka CDM warejee katika majadiliano ya TCD.

Mara zote CDM wanaposusia Mwenyekiti wa CCM ana fura , maana yake CDM ni 'force to reckon with'
Muda uliopotea katika maridhiano ungetumika kushinikiza katiba na kueleza agenda ya kususia uchaguzi.

Inawezekana Mbowe hana mbinu mpya angejiuzulu waje wenye new ideas, ndani ya CDM wapo

Tuna mifano ya ACT na CUF walivyofeli Zanzibar, leo Mnyika anapita pale pale walipojikwaa wengine ili akaangukie pale pale. Na CCM wanajua hilo wanawasubiri waangukie pua tena. Wameleta mswada feki kama chambo
..Sikubaliani na wewe kwamba tatizo ni uongozi ktk vyama vya upinzani. Mimi nadhani Watanzania bado hatujapigika kisawasawa kiasi cha kuamua kutaka mabadiliko.
Yes ndio maana nasema CDM waache kuingia katika michakato ili Wananchi wajifunze.
Kinyume chake ni kuwapa CCM uhalali. Ni kama Zitto na ACT walivyotoa uhalali wa Tume feki ya Mkandara. iLaiti ACT, wenye nguvu visiwani wasingeshiriki Tume ya Mkandara, tungelikuwa pengine leo hii.

Hivyo, badala ya kwenda uchaguzi wa serikali za mitaa au uchaguzi mkuu na mabadiliko feki ni afadhali CDM wakatae ili wananchi wapigike na kupitia hilo watafunguka.

In fact haya tunayoyaona ya Bandari ni kutokana na ukweli kwamba 2020 ilikuwa dhahma , Wananchi wanajua hilo ndio maana wanaunga mkono makundi tofauti yenye misimamo mikali na si maridhiano feki
..Vilevile sikubaliani na wewe kwamba Cdm ndio watetezi wa kukosekana kwa muda wa kuleta Katiba mpya btn now and 2025.
Mnyika kasema muda hautoshi akiakisi kauli ya Mbowe ya siku za nyuma akiwa kanda ya Ziwa.
Waliopaswa kutumia 'muda' ni Wahuni wa CCM , siyo Chadema !
..Nadhani wanaoilaumu Cdm kuhusu kuchelewa kwa Katiba Mpya ni watu waoga wasiotaka kukabiliana na Ccm.
..Katiba imekwamishwa na Ccm. Kuwalaumu Chadema ni kujifanya vichwa maji.
Ni kweli CCM ilivuruga mchakato na haina nia njema, tulishangaa Mbowe kukaa nao meza moja.
Sijui Mbowe alitegemea maua ya aina gani. Hawa CCM ni Wahuni wazoefu haifai kukaa nao mezani.
Mkao na CCM ni haramu na kujI najisi, kama Mbowe alivyo '' jinajisi'' kwa maridhiano

CDM wana option, kwamba, wajifiche nyuma, mambo yatokee yenyewe kimiujiza au Watangulie ili kujenga imani kwamba ni mbadala. Kuchukua ruzuku za kazi za siasa halafu kukwepa majukumu ya siasa ni kujitweza.

Wananchi wanapokubaliana na sauti ya Watanzania badala ya Chama kikuu cha upinzani , ni wake up call.
 
Mzee Warioba amenukuliwa mara kadhaa akisema muda unatosha.

Kinachokosekana ni dhamira ya viongozi waliopo.

Hili jambo la Katiba mpya halizuiliki, limeruhusiwa,

Mbingu zitaamua mzozo!!

Tusubiri.
Naunga mkono hoja
 
Back
Top Bottom