Sikilizeni, alichokifanya Zitto si sawa.
Kwanza, alishiriki tume ya Mkandara akijua kabisa ulikuwa ni ulaghai wa kutafuta namna ya kufuta maoni ya Tume ya Warioba. Zitto alijua hilo lakini akaingia katika mchakato haramu kwasababu binafasi. Yes ni binafasi kwakuwa;
1. Rasimu ya Warioba ndio ilibeba maoni halali ya Watanzania. Hii ya Mkandara ilikuwa ya nini?
2. Zitto anajua ACT ambayo ni CUF ilikuwa katika GNU na kuwa na Tume huru. Matokeo yake tunayajua na Marehemu Jecha ameondoka na kuwaachia majonzi. Sababu za Tume huru ya CUF a.k.a ACT ya wakati huo kufeli ni Katiba
3. Huwezi kubadilisha vifungu vya Tume ya Uchaguzi bila kufumua vifungu vya Katiba. Nilipomuona ameenda Bungeni kushangilia mswada nilimshangaa sana, yaani ni kama 'amateur' Huwezi kuwa na Tume huru wakati Rais akiwa na nguvu juu ya tume hiyo
Hata hivyo Zitto anasukumwa na ACT Wazalendo waliofeli mara nyingi Zanzibar na kukubali nusu mkate.
Lakini madhara yake ni makubwa, ushiriki wa Zitto tume ya Mkandara ulitoa uhalali wa haramu hiyo.
Laiti asingeshiriki tusingekuwa na haya ya leo, akaunga mkono kwasababu tusizozijua. Ni felia tu kama hawa akina Mnyika