Elias Msuya
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 175
- 681
Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amewataka viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama hicho kuandaa uchaguzi na kufanya uteuzi ili kuziba nafasi za viongozi waliojiondoa kwenye chama hicho, maarufu G55.
Kundi la G55 linahusisha viongozi na makada wa chama hicho wanaopinga kampeni ya chama hicho ya No Reforms No Election na sasa wamekuwa wakitangaz akujitoa kwenye chama hicho, lakini hawasemi wanajiunga na chama gani.
Soma zaidi: Deotha Minja aeleza sababu ya kuondoka Chadema
Miongoni mwa waliojitoa ni pamoja na Mwenyekiti wa Kanda ya Kati yenye mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida, Devotha Minja aliyesindikizwa na wanachama zaidi ya 200. Wamo pia wenyeviti wa mikoa, viongozi wa kanda na viongozi wastaafu.
Akizungumza leo Mei 16 wilayani Maswa Mkoa wa Simiyu, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema makada wanaojitoa katika chama hicho ni wasaliti wa mapambano.
Amesema kuondoka huko ni mkakati uliopangwa ili kuwahadaa makada na vuongozi ili wapate vyeo huko wanakotarajia kwenda.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
“Kwa kuwa tuko wengi natoa maelekezo kupitia mkutano huu wa Maswa, kwa viongozi wa Chadema Maswa kwa viongozi wa Chadema nchi nzima, kwa kuwa Chadema inaungwa mkono na wananchama wengi, akihama kiongozi pale pale, ingieni kwenye katiba ya chama ibara ya 6.3 na hapo hapo mtekeleze ibara ya (a) inayosema kamati ya utendaji ya kila ngazi au Baraza Kuu itaziba muda nafasi ya ya kiongozi aliyechaguliwa na mkutano mkuu wa ngazi husika.
“Tumieni vilevile kifungu (a) cha ibara hiyo hiyo ya 6.5 ya Katiba kinachosema, nafasi zilizo wazi za viongozi walioteuliwa, zitazibwa na vikao husika kwa kufanya uteuzi mpya. Tumieni Katiba kwa kuhakikisha kuwa akitoka kiongozi mmoja kwa kusaliti mapambano hapo hapo aingie mwingine tuendeleze mapambano,” amesema.
Huku akirejea aya za Biblia, Mnyika alitoa mfano wa Yuda Iskasiote aliyemsaliti Yesu kwa vipande 30mvya fedha.
“Lakini kusalitiwa kwa Yesu hakukuzuia kendelea na safari ya ukombozi, alipita mapito magumu, mateso mpaka msalabani, lakini usaliti ule haukuzuia ukombozi, bali ulitimiza na hatimaye nafasi ya Yuda Iskarioe ikazibwa kupitia uchaguzi. Uchaguzi hatukuanza sisi hapa Tanzania
“Ukisoma kitabu cha Matendo ya Mitume 1: 15 hadi 26, utakuta mitume wameongezeka sio tena 12. Wakakaa kikao cha watu 120, wakasali na wakapiga kura wakamchagua Mathias kuwa mtume kuziba nafasi Yuda Iskariote aliyesalit. Hivyo basi akisaliti mmoja zibeni nafasi tusonge mbele,” amesema.