Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,561
- 19,056
Juzi nimekutana na jamaa yangu mmoja mfanyakazi wa shirika moja la umma lenye ukwasi mkubwa huku na yeye akiwa ni mtu mwenye uwezo wake na anapenda kujirusha sana na mpenda totoz.
Rafiki yangu huyu alikuwa amepata matatizo kazini na akafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi iliyofanya akae ndani(mahabusu) karibu mwaka na nusu. Bahati nzuri ameshinda kesi na sasa yupo katika kufatilia taratibu za ama kurudishwa kazini au apewe chake asepe.
Katika maongezi yetu akaniusia "Mdogo wangu hakikisha wapenzi wako unawasaidia kwa kila hali. Ukiweza wafungulie biashara, usihonge sijui elfu ngapi, mpe mwanamke wako hela ya maana."
Akaniambia kama ukipata milioni 30 mpe hata milion kumi, wanawake wanakumbuka fadhila sana na wana msaada katika matatizo.
Anasema hata ndugu wanaweza wasikusaidie kwenye matatizo pamoja na kuwa umewahi kuwasaidia sana. Kanambia katika kipindi chote alichokaa ndani wanawake zake wamemsapoti sana kwa kumtia moyo, kumhurumia na kumhudumia kwa mambo mbalimbali na alikuwa anahisi kabisa hisia zao za huruma ni za kweli kabisa tofauti na marafiki zake wanaume.
Aliponichosha ni pale aliponitajia majina ya marafiki zetu kadhaa wanaume wenzetu kauli alizoambiwa kuwa walikuwa wanazitoa dhidi yake baada ya yeye kupata matatizo. Wengine walikua wanasema akome sasa anajifanya anazo, wengine walitamani afungwe kabisa eti mademu zao walikuwa wanamshobokea, na wapo waliofurahia tu yeye kupata matatizo.
Mimi nathibitisha kuwasikia jamaa tena aliokua nao karibu kwenye kula bata wakimsema kwa ubaya.
Hapa natafakari usia na kauli hii ya rafiki yangu na nahisi kama ina kaukweli fulani hivi ila naendelea kufanya utafiti wa kina nione kama naweza kuipitisha na mimi niitumie kama msimamo na mtazamo wangu rasmi.
Rafiki yangu huyu alikuwa amepata matatizo kazini na akafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi iliyofanya akae ndani(mahabusu) karibu mwaka na nusu. Bahati nzuri ameshinda kesi na sasa yupo katika kufatilia taratibu za ama kurudishwa kazini au apewe chake asepe.
Katika maongezi yetu akaniusia "Mdogo wangu hakikisha wapenzi wako unawasaidia kwa kila hali. Ukiweza wafungulie biashara, usihonge sijui elfu ngapi, mpe mwanamke wako hela ya maana."
Akaniambia kama ukipata milioni 30 mpe hata milion kumi, wanawake wanakumbuka fadhila sana na wana msaada katika matatizo.
Anasema hata ndugu wanaweza wasikusaidie kwenye matatizo pamoja na kuwa umewahi kuwasaidia sana. Kanambia katika kipindi chote alichokaa ndani wanawake zake wamemsapoti sana kwa kumtia moyo, kumhurumia na kumhudumia kwa mambo mbalimbali na alikuwa anahisi kabisa hisia zao za huruma ni za kweli kabisa tofauti na marafiki zake wanaume.
Aliponichosha ni pale aliponitajia majina ya marafiki zetu kadhaa wanaume wenzetu kauli alizoambiwa kuwa walikuwa wanazitoa dhidi yake baada ya yeye kupata matatizo. Wengine walikua wanasema akome sasa anajifanya anazo, wengine walitamani afungwe kabisa eti mademu zao walikuwa wanamshobokea, na wapo waliofurahia tu yeye kupata matatizo.
Mimi nathibitisha kuwasikia jamaa tena aliokua nao karibu kwenye kula bata wakimsema kwa ubaya.
Hapa natafakari usia na kauli hii ya rafiki yangu na nahisi kama ina kaukweli fulani hivi ila naendelea kufanya utafiti wa kina nione kama naweza kuipitisha na mimi niitumie kama msimamo na mtazamo wangu rasmi.
Last edited by a moderator: