Oltung'anyi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 284
- 196
Ilitarajiwa ushindwe kumuelezea huyu Mungu wa level nyingine. Sasa unamuelezea kirahisi tu. Mungu ni wa level yetu kabisa. Tatizo linaanzia pale unapomuogopa. Mungu ni uwepo, na kumbuka usipokuwepo, hakuna kilichopo. Uwepo ni ukamilifu, hali nadhifu kabisa isiyo na doa. Ukamilifu ni upendo, unyenyekevu na kila tendo jema unalofikiri unapaswa kutendewa. Sasa ni ajabu kuu mno kuwaza kuwa Mungu ni level nyingine.Kuna mambo ya kufanyia mzaha lakini si Mungu. Naomba mwenye enzi Mungu akurehemu. Mungu si wa size yetu, yuko kwenye level nyingine, malumbano kuhusu Mungu yupo au hayupo sidhani kama ni sahii sana. Wote tutakufa alafu tutajua kama yupo au hayupo, usiwe na haraka.
Ni ajabu kuu pia kusema unaogopa upendo, unyenyekevu, unadhifu. Ni ajabu kabisa.