LOTH HEMA
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 13,249
- 17,970
kuna Mungu na munguNyie mnao amini uwepo wa Mungu, Wakristo na waislam, na madhehebu mengine Je kila mmoja wenu mnamaanisha Mungu Mmoja?
Yani unavyomfikiria wewe na mwezio ni hivyohivyo? Je unauhakika Kiongozi wako wa dini, Rafiki yako, na yeyote yule Jinsi anavyomuwaza huyu Mungu alivyo ndivyo unavyomuwaza wewe? Yani picha uliyojijengea kichwani mwako Jinsi alivyo, tabia zake ndivyo wenzio wanavyomuwaza hivyo? Kama mnatofautiana hatima yake nini?
Je huyu Mungu wenu alivyokusudia mumuwaze alivyo ndivyo ilivyo?
Je mpaka sasa unauhakika na dini yako ndio sahihi kumweleza huyo Mungu? Au tangu upokee kutoka kwa wazazi wako dini hiyo ndio umejidhihirisha wazi kwamba upo sahihi?
Je umejifunza dini nyingine kujihakikishia upo sahihi mpaka sasa kwamba Mungu anaikubali dini yako? na upo sahihi?
Je Ni biblia na quran ndio references kuthibitisha Mungu yupo, na jinsi alivyo?
Unajidhihirishaje kwamba vitabu hivyo si maandiko ya watu kwa utashi wao?
Je Maswali yangu hapo Unaweza kuyajibu????