Mmh sijui nimwambie! Naogopa atalipokeaje

Mmh sijui nimwambie! Naogopa atalipokeaje

Very simple, kama wewe umezipata kwa njia ya mtandao then fungua fake accounts, kisha mtumie huyo shoga yake mazagazaga yote. Kisha muachie aamue mwenyewe kusuka au kunyoa. Wewe utakuwa huna lawama tena mana taarifa atakuwa nazo .
NB Mahaba hayaingiliwi wala hayashauriki, kaa mbali utakuja kuumbuka huwezijua huyo shoga yako kafa kiasi gani kwa huyo jamaa. Unaweza ukaamua kujilipua kumwambia halafu yeye kwa jinsi alivyokolea akamwambia muhusika kuwa wewe ndio umemwambia, na pia shoga yako anaweza akaamua kuwa mchepuko wa huyo jamaa. Je hapo hujaumbuka?
 
Hapo ndo huwa nashangaa"unaenda kuzima moshi kwa jirani wakati kwako umeacha moto unawak" huu uzalendo naupenda kuliko.
 
Mambo ya kawaida saana mbona haya na ndio wanaume wetu siku hizi na tushawazoeya we kama rfk yako na wewe hamuyajui basi toaneni tongotongo...
 
Mimi naona busara zungumza na huyo shemeji mchepuko...mpe altimatum ya kuweka mambo yake sawa na rafiki yako. Lakini kama mmeshibana lipasue bwana.......The guy is time waster kwa kweli. Na huyo rafiki kilaza 3 years hata engagement au kupelekana kwa wazazi basi.
 
Um tune aangalie ulipoangalia ukaona hizo taarifa, ataamua yeye. Unaweza kuanza kwa kumuelezea umeona sehemu mtu anafanana na jamaa kisha muoneshe
Fanyia kazi ushauri huu wa PesaNdogo ni mzuri,usimweleze moja kwa moja ajionee yeye mwenyewe,
 
Mmh naona w'ume weng mmereact vbya sn hii ishu kwann? Maana naona weng mmemuona n mnoko. Maana yke n nini!? Na wakt anamuhurumia rafik yake jins alivyokalia kuti bovu.! N mtazamo tu

umbea mbona asiseme mazuri yake kama si unoko huo
 
Mimi ni mwanaume nakupa pole sana dada yangu kwa kutukwana na baadhi ya wanaume wezangu viumbe wasie jitambua, huyu dada kaleta uzi wake tumshauri kuwa amwambie rafiki yake au asimwambie mnaanza kumtolea matusi mnafikili nyie ndie kawachunguza. acheni tabia hizo za kumtukana binadamu mwenzako bila sababu ya msingi.....Mpaka dada kajuta kuleta uzi humu...watu wametokwa na povu kama wamechunguzwa....TABIA YA KUMTUKANA MTU BILA KUFIKIRI IKOME KABISA NA MICHEPUKO SIO DILI BAKI NJIA KUU UKIMWI UPO NA UNAUA.
 
Wana MMU habarini za leo,

Kuna jambo linanitatiza na kuniumi za nataka kusema lakinia naogopa mlengwa atalipokeaje jambo hilo mmh naogopa kuitwa mbeya mie maana wanawake hatunaga vifua vya kuvumilia maumivu.Nina rafiki yangu ambaye ana date na kaka flani hivi for more than a year now mkaka anaonyesha ana mcare na kujifanya yuko muwazi kwake kwa kila kitu.

Wakati wanaanza mahusiano mkaka alimwambia ukweli kuwa alikuwa anaishi na mwanamke na wamezaa ila hawakuoana na wametengana kwa muda huo kila mtu anaangalia maisha yake so my friend akaona sio mbaya coz hata yeye alikuwa single na mkaka ni kweli alimvutia wakaamua kuanza mahusiano.Shida imekuja juzi katika pekuapekua yangu ya kimitandao nimegundua yule kaka ameoa ndoa ya kanisani na still wanaishi na mkewe though mke yuko mkoa mwingine kikazi.

Evidence ninazo kuanzia picha za ndoa mpaka picha ambazo alikuwa anapiga na mkewe kipindi hiki ambacho alikuwa anaenda kumtembelea na kumuongopea shosty yuko safarini wana MMU hebu nisaidieni nifanyeje roho inaniuma coz naona kabisa shoga angu anapoteza muda ila je nikimwambia atalipokeajee? Hatoniona mimi mnafiki nataka kuwagombanisha na kuharibu furaha yao?

Maana shosti anamwamini vibaya sana huyu mkaka and kila mara anamsifia a guy is so muwazi and mkweli.

Tengeneza akunt feki ya fb au namba mpya ya watsapp then mtumie kila kitu humo either kwa watsapp au fb (kumbuka ziwe feki kuanzia majina na kila kitu)!! Meseji zikiwa delivered akaunt hizo usitumie tena!!!! Hapo utakua umemsave kila mtu!!
 
Wana MMU habarini za leo,

Kuna jambo linanitatiza na kuniumi za nataka kusema lakinia naogopa mlengwa atalipokeaje jambo hilo mmh naogopa kuitwa mbeya mie maana wanawake hatunaga vifua vya kuvumilia maumivu.Nina rafiki yangu ambaye ana date na kaka flani hivi for more than a year now mkaka anaonyesha ana mcare na kujifanya yuko muwazi kwake kwa kila kitu.

Wakati wanaanza mahusiano mkaka alimwambia ukweli kuwa alikuwa anaishi na mwanamke na wamezaa ila hawakuoana na wametengana kwa muda huo kila mtu anaangalia maisha yake so my friend akaona sio mbaya coz hata yeye alikuwa single na mkaka ni kweli alimvutia wakaamua kuanza mahusiano.Shida imekuja juzi katika pekuapekua yangu ya kimitandao nimegundua yule kaka ameoa ndoa ya kanisani na still wanaishi na mkewe though mke yuko mkoa mwingine kikazi.

Evidence ninazo kuanzia picha za ndoa mpaka picha ambazo alikuwa anapiga na mkewe kipindi hiki ambacho alikuwa anaenda kumtembelea na kumuongopea shosty yuko safarini wana MMU hebu nisaidieni nifanyeje roho inaniuma coz naona kabisa shoga angu anapoteza muda ila je nikimwambia atalipokeajee? Hatoniona mimi mnafiki nataka kuwagombanisha na kuharibu furaha yao?

Maana shosti anamwamini vibaya sana huyu mkaka and kila mara anamsifia a guy is so muwazi and mkweli.


umbea at work
 
let them fall into their destiny usiwe kikwazo,,,kama nikuachana wataachana tu ila dont be the reason
 
Siku hizi kuonyana imekuwa kufuatiliana maisha.
Unapaswa kumuonya huyo rafiki yako kwa kuingilia ndoa ya watu.

Ndoa ni ya mume na mke, tena hufanyika hadharani mbele ya mashahidi wengi. Hivyo wanandoa wanapaswa kuishi kwa uaminifu kwenye ndoa zao.

Haya mambo kuyaacha hivihivi ndiyo yanaharibu kizazi cha leo na kufanya ndoa kukosa thamani kwa kuendekeza uzinzi na uasherati kwenye jamii.
 
Nimegundua kitu hapo NA wewe unampenda huyo JAMAA ndo maana umeanza kumpekua kwenye mitandao
 
Muonyeshe huko ulikopata hizo habari mtandaoni. Ata jumlisha mwenyewe. Usizungumze chochote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom