Mlipuko wa ugonjwa usiofahamika mkoani Geita

Mlipuko wa ugonjwa usiofahamika mkoani Geita

Habari,

Nipo Geita kumekuwa na hali ambayo inatia shaka kidogo.

Kumekuwa na ka mlipuko ka ugonjwa ambao unatembelea kila familia na kila mtu.

Dalili kubwa ni homa...mafua na kikohozi.

Ukienda kupima unaambiwa ni malaria au UTI unapewa na dawa za kikohozi na mafua.

Ni takribani mwezi sasa hii hali nimeiona na familia yangu mwenyewe imetukumba.

Ni familia nyingi sana zimekumbwa na hii hali.

Nimejaribu kupita katk vituo vya afya (zahanati) wagonjwa ni wengi...shuleni nako ruhusa za wagonjwa ni nyingi sana

Kwenye maduka ya dawa mauzo yamepanda sana kutoka 20,000 kwa siku hadi 50,000-70,000 kwa siku.
Ila hakuna vifo vilivyo ripotiwa.

Naomba mamlaka husika iangalie hili swala isijekuwa tumevamiwa kirusi kipya.
Asante kugutuka na kuhisi huenda kukawa na tatizo nyuma ya haya. Lakini, zaidi ya kuandika humu kwenye JF ingekuwa na maana zaidi kama utalifikisha suala hili kwenye vyombo husika; ikiwemo ofisi ya Mkuu wa Wilaya au kwingineko ili walifuatilie kwa undani zaidi. Haitoshi kuomba vyombo husika vifuatilie. Kwani una uhakika watu wa kwenye vyombo husika pia wamo humu kwenye JF? Kuna malalamiko mingine huwa yanaandikwa mitandaoni kwamba uhalifu fulani unaendelea mahali fulani na polisi hawachukui hatua. Sasa polisi watachukuaje hatua kama hawajaarifiwa? Ni juu yetu wananchi tukiona kitu tutoe taarifa panapohusika. Vivyo hivyo ni suala hili la ugonjwa. Wewe una ushahidi wa ndugu zako kadhaa waliodhurika. Ukitoa ushahidi huo uchunguzi utafanyika kuanzia na ndugu zako na labda watu zaidi watagundulika na tatizo kuthibitiwa. Hivi sasa wahusika hata kama wameiona mada yako hawaezi wala kujua waanzie wapi kwani hukujitambulisha.
 
Habari,

Nipo Geita kumekuwa na hali ambayo inatia shaka kidogo.

Kumekuwa na ka mlipuko ka ugonjwa ambao unatembelea kila familia na kila mtu.

Dalili kubwa ni homa...mafua na kikohozi.

Ukienda kupima unaambiwa ni malaria au UTI unapewa na dawa za kikohozi na mafua.

Ni takribani mwezi sasa hii hali nimeiona na familia yangu mwenyewe imetukumba.

Ni familia nyingi sana zimekumbwa na hii hali.

Nimejaribu kupita katk vituo vya afya (zahanati) wagonjwa ni wengi...shuleni nako ruhusa za wagonjwa ni nyingi sana

Kwenye maduka ya dawa mauzo yamepanda sana kutoka 20,000 kwa siku hadi 50,000-70,000 kwa siku.
Ila hakuna vifo vilivyo ripotiwa.

Naomba mamlaka husika iangalie hili swala isijekuwa tumevamiwa kirusi kipya.
SERIOUSLY...! Team ya wizara ya Afya itimbe mapema huko dalili za COVID-19 zote..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Kuleni malimao na machungwa kwa wingi
2. Tumieni Detto kunawia
3. Kaeni maeneo yenye joto/jua inavyosemekana virusi vipya havienei sana kwenye joto
4. Epukeni kula vyakula visivyoiva hasa maziwa na nyama
5. Katika hali kama hiyo kamwe msile vibudu au mifugo yenye ugonjwa
6. Hamasishaneni kunawa mara kwa mara kwa kutumia maji na sabuni
7. Watu wanaopelekewa vituo vya afya waeleze homa ilivyowapata na maeneo waliyotembelea mara ya mwisho
8. Watu wanapokohoa/kupenga watumie karatasi/tissue wazitupe baada ya matumizi kuzuia kueneza ugonjwa
9. Watu waepuke kugusa pua macho na mdomo na kushikana mikono
10.Hakikisheni mamlaka husika kwenye maeneo yenu zinapata ujumbe huu
Hala hala msilianzishe Wajameni........
Vaeni maski pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ni msimu wa mvua, ni majira ya baridi kuanza taratibu. Hii ni kawaida sana kunapotokea mabadiliko ya hali ya hewa kutokea kwa mafua na kikohozi.

Ingawa mamlaka husika ziantakiwa kujiridhisha
 
ukute corona....sema uzuri ni kua wabongo immune kubwa
 
Asante kugutuka na kuhisi huenda kukawa na tatizo nyuma ya haya. Lakini, zaidi ya kuandika humu kwenye JF ingekuwa na maana zaidi kama utalifikisha suala hili kwenye vyombo husika; ikiwemo ofisi ya Mkuu wa Wilaya au kwingineko ili walifuatilie kwa undani zaidi. Haitoshi kuomba vyombo husika vifuatilie. Kwani una uhakika watu wa kwenye vyombo husika pia wamo humu kwenye JF? Kuna malalamiko mingine huwa yanaandikwa mitandaoni kwamba uhalifu fulani unaendelea mahali fulani na polisi hawachukui hatua. Sasa polisi watachukuaje hatua kama hawajaarifiwa? Ni juu yetu wananchi tukiona kitu tutoe taarifa panapohusika. Vivyo hivyo ni suala hili la ugonjwa. Wewe una ushahidi wa ndugu zako kadhaa waliodhurika. Ukitoa ushahidi huo uchunguzi utafanyika kuanzia na ndugu zako na labda watu zaidi watagundulika na tatizo kuthibitiwa. Hivi sasa wahusika hata kama waameiona mada yako hawaezi wala kujua waanzie wapi kwani hukujitambulisha.
Nashukuru kwa maoni .
Naweka location
 
Hilo ni onyo kwa wanaokula vibudu na mifugo yenye ugonjwa msisitizo kuepusha hatari

Onyo kwa wanaokula vibudu na mifugo migonjwa KATIKA HALI YA SASA!

KWA HIYO, hali ikirudi kawaida turudi kula vibudu na wanyama magonjwa?
 
Back
Top Bottom