Mlipuko wa ugonjwa usiofahamika mkoani Geita

Mlipuko wa ugonjwa usiofahamika mkoani Geita

MC44

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2019
Posts
2,168
Reaction score
3,306
Habari,

Nipo Geita kumekuwa na hali ambayo inatia shaka kidogo.

Kumekuwa na ka mlipuko ka ugonjwa ambao unatembelea kila familia na kila mtu.

Dalili kubwa ni homa...mafua na kikohozi.

Ukienda kupima unaambiwa ni malaria au UTI unapewa na dawa za kikohozi na mafua.

Ni takribani mwezi sasa hii hali nimeiona na familia yangu mwenyewe imetukumba.

Ni familia nyingi sana zimekumbwa na hii hali.

Nimejaribu kupita katk vituo vya afya (zahanati) wagonjwa ni wengi...shuleni nako ruhusa za wagonjwa ni nyingi sana

Kwenye maduka ya dawa mauzo yamepanda sana kutoka 20,000 kwa siku hadi 50,000-70,000 kwa siku.
Ila hakuna vifo vilivyo ripotiwa.

Naomba mamlaka husika iangalie hili swala isijekuwa tumevamiwa kirusi kipya.


Nimepokea ushauri wa kuweka location.

Wilaya ya geita
Kata ya Kaseme

Hiii kata ndio imeathirika
 
1. Kuleni malimao na machungwa kwa wingi
2. Tumieni Detto kunawia
3. Kaeni maeneo yenye joto/jua inavyosemekana virusi vipya havienei sana kwenye joto
4. Epukeni kula vyakula visivyoiva hasa maziwa na nyama
5. Katika hali kama hiyo kamwe msile vibudu au mifugo yenye ugonjwa
6. Hamasishaneni kunawa mara kwa mara kwa kutumia maji na sabuni
7. Watu wanaopelekewa vituo vya afya waeleze homa ilivyowapata na maeneo waliyotembelea mara ya mwisho
8. Watu wanapokohoa/kupenga watumie karatasi/tissue wazitupe baada ya matumizi kuzuia kueneza ugonjwa
9. Watu waepuke kugusa pua macho na mdomo na kushikana mikono
10.Hakikisheni mamlaka husika kwenye maeneo yenu zinapata ujumbe huu
Hala hala msilianzishe Wajameni........
 
1. Kuleni malimao na machungwa kwa wingi
2. Tumieni Detto kunawia
3. Kaeni maeneo yenye joto/jua inavyosemekana virusi vipya havienei sana kwenye joto
4. Epukeni kula vyakula visivyoiva hasa maziwa na nyama
5. Katika hali kama hiyo kamwe msile vibudu au mifugo yenye ugonjwa
6. Hamasishaneni kunawa mara kwa mara kwa kutumia maji na sabuni
7. Watu wanaopelekewa vituo vya afya waeleze homa ilivyowapata na maeneo waliyotembelea mara ya mwisho
8. Watu wanapokohoa/kupenga watumie karatasi/tissue wazitupe baada ya matumizi kuzuia kueneza ugonjwa
9. Watu waepuke kugusa pua macho na mdomo na kushikana mikono
10.Hakikisheni mamlaka husika kwenye maeneo yenu zinapata ujumbe huu
Hala hala msilianzishe Wajameni........
Nashukuru kwa ushauri wako ndugu.
 
Nashukuru kwa ushauri wako ndugu.
Karibu sana pia tunashukuru kwa taarifa usisite kuleta updates ya nini kinachojiri lakini kunawa mikono mara kwa mara kwa sabuni na maji na au (alcohol based hand rub yenye alcohol kuanzia asilimia 60) kama upo eneo lisilo na maji au sabuni pia kukohoa na kupenga au kupiga chafya kwa kujifunika na kitu hata kama si lile gari basi mtakuwa mmetekeleza kanuni bora tu za afya unaeza kukuta africa ikaja Nissan covid 22 nikukaa tu kikomando maana huwezi jua

Detto za maji ni muhimu sana ni vyema kuwa nazo majumbani hasa kipindi hiki.
 
Hali bado inakuwa tete na hakuna wa kuzungumzia
 
watu kama wanne nmekutana nao juzi kabla ya kuondoka walikuwa

wanakohoa mpaka sauti zinapotea
 
Back
Top Bottom