Sisi kama wananchi wazalendo; Ni lazma tuchangie kwa uwezo wetu wote kuhakikisha watu wanaohatarisha usalama wa nchi yetu kipenzi wanakamatwa na kudhibitiwa.Kufuatia suala la Arusha; tunatakiwa tuunganishe nguvu zetu, uwezo wetu kifikra,wasaa wa kimazingira, ueledi na kila kiwezekanacho kuhakikisha wahusika wanapatikana.Tujitahidi kuepuka na ushabiki wa kisiasa katika hili ili tuweze kupata nadharia za kitaalam ambazo zinaweza kutupa pa kuanzia.Katika hili inabidi tuwe wakweli 100% hata pale mmoja wetu atakapoguswa.
Serikali imeahidi mill 100 kwa atakaesaidia kubainika kwa mtandao wa uhalifu uliohusika ila usalama wa nchi yetu ni zaidi hata ya million 100.Tushirikianeni mawazo ili tupate pa kuanzia na hatimae tuinusuru nchi.
Kwa kuanzia nizitete kwenu nadhadhia zinazoweza kutupa muongozo wa pakuanzia na vielelezo vilivyopo.
(1)Ni nadharia kwamba wahusika watakuwa ni mtandao ndani ya CCM
(2)Ni nadharika kwamba wahusika watakuwa ni CHADEMA wenyewe.
(3)Ni nadharika kwamba zitakuwa ni hujuma za makundi ya kisiasa toka nje ya nchi
(4) ni nadharia kwamba yatakuwa ni makundi yenye ufungamano na Al-qaeda/Al-shabaab.
Nitoe vielelezo vilivyopo kwa kila nadharia kisha alie na ziada atuongezee ili tupate muelekeo.
1.NADHARIA KWAMBA NI CCM.
Hoja ni kwamba CCM watakuwa wamezidiwa nguvu sasa wameamua watumie mbinu za kimafia na za kutisha.
Muunganikano wa matukio kwa hoja hii;
(a)
MweziMarch 2013; Kinana alikutana na Kiongozi wa CHAMA CHA KIKOMUNISTI cha NchiniChina.(walifanya mazungumzo).
Katibu Mkuu wa CCM
Tunapounganisha hayo matukio tunapata wazo juu ya nadharia ya kwanza.
Naendelea kuleta nadharia zingine;
= = = = = = = = = = = = = = = = = = = = = =