Mlipuko Arusha na nadharia Pasua Kichwa!

Tuwaachie vyombo vya dola/JWTZ vinavyohusika na uchunguzi wa maswala ya milipuko wafanye kazi yao kwa kuzingatia weledi na maadili ya kazi zao ili tupate mwarobaini wa hii milipuko ya kila kukicha!

Angalizo kwa wataalam walioko field wakiendelea na uchunguzi wao, ni vema wasikubali hata kidogo kazi yao kuingiliwa na wanasiasa!

Mkikubali kuingiliwa na wanasiasa ni dhahiri haya mambo ya milipuko yataendelea na Taifa kuendelea kupoteza nguvu kazi!
 
Mtoa mada ameonesha udhaifu mkubwa sana ktk kudadabua hoja yake. 1. Anasema mlipuko Arusha ni nadharia pasua kichwa. Ninavyofahamu mimi kitu kinakuwa pasua kichwa kama kinakosa majibu au majibu yanatatanisha. Kwa maelezo yake utata uko wapi? wakati anaonesha dhahiri kuwa ccm wanahusika (kwa ushahidi wa mazingira). 2. Mtoa mada anaonekana ushabiki wa kisiasa unamtawala kuliko ukweli (reality). Mfano, kachambua vizuri mazingira yanayoweza kudhaniwa ccm na cdm wanahusika, lakini cha ajabu ametoa udhafu wa kuihusisha cdm TU na mlipuko kana kwamba hoja za kuihusisha ccm hazina udhaifu. Hapa ndipo umakini na ueledi wa mtoa hoja unapokuwa mashakani.
Mkuu hapa hatudili ukamilifu na udhaifu wa mtoa mada.Elewa kuwa mtoa mada ni mtu tu kama wewe kwa hiyo unachotakiwa kukifanya ni kusaidia unakoona kuna mapungufu badala ya kumlaumu mwenzako.
 
Kofia ya kikominist ndo inamfanya mtu awe gaidi akiivaa kwa sababu tu ni ya wachina?
Kwani huko china hicho chama cha kikomunist kinaua watu.
Grunet la kisasa likoje na lisilo la kisasa likoje?maana grunet liko la aina moja tu tangu vita vya pili hakuna Advanced medium range grunet.
Risasi zilizozaa hayo maganda ni za polisi wakati wakijihami baada ya wanachadema kuwashambulia kwa mawe.kwahiyo nadharia hii iko debunked.
Swali la kujiuliza hapa,nani aliwaamuru raia waanze kuwaponda mawe polisi?kwasababu logic haikubali kuwa bomu limelipuka halafu watu badala ya kukimbia kujiokoa waanze mapambano na polisi lazima kuna watu waliorganise ili mtupa bomu ajichanganye na kupotea.
Yeyote alieanza kuwambia watu wawapige polisi pia alitaka polisi waact ili idadi ya maafa iwe kubwa kuvuta huruma ya hadi jumuia za kimataifa.
 
Yaani wewe unauliza na kujijibu mwenyewe! Kwa nini unataka ku-manage mawazo ya watu? Hiyo nadharia ya CCM umeipamba wakati ya CHADEMA yenye ushahidi mwingi umeifinya na kukanusha hapo hapo!

Ndio maana nchi hii ni masikini kwa sababu wajinga wanadhani wana akili!

Hapo kwenye red panamuhusu Mwigulu..
 
Yaani wewe unauliza na kujijibu mwenyewe! Kwa nini unataka ku-manage mawazo ya watu? Hiyo nadharia ya CCM umeipamba wakati ya CHADEMA yenye ushahidi mwingi umeifinya na kukanusha hapo hapo!

Ndio maana nchi hii ni masikini kwa sababu wajinga wanadhani wana akili!

Na wewe ndiye mwalimu wa hao wajinga wa Tanzania ,vitu viko wazi havihitaji kupambwa'
 
how i wish through serial numbers za vitu kama silaa za hatari kama hizi zingekuwa zinaambatana na taarifa za mnunuzi ambazo zingeambatanishwa kwenye records za serial number yenyewe.. sijui wataalam labda mtuambie more abt this as its not a local made
Kama umenunua kwa taratibu za kawaida taarifa zitakuwepo tu!
 
Nakusoma kiongozi unavyomiminika.

Well, hakuna pa kujificha kwa wauaji, majambazi, waongo na wanafiki ambao muda huu wanatuchukulia wananchi kama vile soli ya kiatu.
 
Nawaogoppa sana CCM kwa sasa!ila wanajiharibia wenyewe tena sana!wajue hao mabalozi wa nchi za magharibi wana source zao kujua ukweli woote!usishangae Obama akakatisha ziara yake!aibu sana kuua ili kutisha wapiga kura kuchagua majambazi na mafisadi
 
Kama umenunua kwa taratibu za kawaida taarifa zitakuwepo tu!

sidhani kama mchina anaweka kwenye intanet record ya silaha anazouza.na taarifa kupatikana kwenye search engine yeyote mfano google ,yahoo etc ni mpaka habari ziwekwe kwenye mtandao.
 
sidhani kama mchina anaweka kwenye intanet record ya silaha anazouza.na taarifa kupatikana kwenye search engine yeyote mfano google ,yahoo etc ni mpaka habari ziwekwe kwenye mtandao.

Ninacho maanisha ni kuwa "serikali ifuatilie kiwanda kili produce na kuuza hizo silaha itajulikana imeuzwa lini imesafirishwa vipi wanunuzi ni kampuni ,"chama" au watu gani.
japokuwa naamini kabisa "sirikali" WOULD'NT DARE DO THAT!
 
Sisi kama wananchi wazalendo; Ni lazma tuchangie kwa uwezo wetu wote kuhakikisha watu wanaohatarisha usalama wa nchi yetu kipenzi wanakamatwa na kudhibitiwa.Kufuatia suala la Arusha; tunatakiwa tuunganishe nguvu zetu, uwezo wetu kifikra,wasaa wa kimazingira, ueledi na kila kiwezekanacho kuhakikisha wahusika wanapatikana.Tujitahidi kuepuka na ushabiki wa kisiasa katika hili ili tuweze kupata nadharia za kitaalam ambazo zinaweza kutupa pa kuanzia.Katika hili inabidi tuwe wakweli 100% hata pale mmoja wetu atakapoguswa.

Serikali imeahidi mill 100 kwa atakaesaidia kubainika kwa mtandao wa uhalifu uliohusika ila usalama wa nchi yetu ni zaidi hata ya million 100.Tushirikianeni mawazo ili tupate pa kuanzia na hatimae tuinusuru nchi.


Kwa kuanzia nizitete kwenu nadhadhia zinazoweza kutupa muongozo wa pakuanzia na vielelezo vilivyopo.

(1)Ni nadharia kwamba wahusika watakuwa ni mtandao ndani ya CCM

(2)Ni nadharika kwamba wahusika watakuwa ni CHADEMA wenyewe.

(3)Ni nadharika kwamba zitakuwa ni hujuma za makundi ya kisiasa toka nje ya nchi

(4) ni nadharia kwamba yatakuwa ni makundi yenye ufungamano na Al-qaeda/Al-shabaab.

Nitoe vielelezo vilivyopo kwa kila nadharia kisha alie na ziada atuongezee ili tupate muelekeo.

1.NADHARIA KWAMBA NI CCM.

Hoja ni kwamba CCM watakuwa wamezidiwa nguvu sasa wameamua watumie mbinu za kimafia na za kutisha.

Muunganikano wa matukio kwa hoja hii;

(a)MweziMarch 2013; Kinana alikutana na Kiongozi wa CHAMA CHA KIKOMUNISTI cha NchiniChina.(walifanya mazungumzo).

Katibu Mkuu wa CCM
, Abdulrahman Kinana, akiwakatika mazungumzo na Mjumbe wa Tume ya Uongozi wa Taifa wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), Liu Yunshan, kwenye Ofisi za chama hicho mjini Beijing China



(b) Kofia inayoonekana hapo chini; ni kofia inayovaliwa na makamanda wa chama cha Kikomunisti cha China.
.


chinese-red-army-hat-people-s-liberation-army-cap-0db2a.JPG

(c)Mwigulu akiwa na kofia hii
nchemba.JPG



(d)Mwigulu nchemba akisema watakaoipinga CCM watakufa


(e) hapo awali Mwigulu alishawahi kusema;

Pia alishawahi kusema;



Kuna taarifa kwamba kwa uchunguzi wa awali uliofanyka kwenye mabaki ya mabomu; na risasi, zinaonekana ni za kichina tena za model za kisasa.






Tunapounganisha hayo matukio tunapata wazo juu ya nadharia ya kwanza.

Naendelea kuleta nadharia zingine;
= = = = = = = = = = = = = = = = = = = = = =


  • Kwenye kesi inayoendelea katika mahakama kuu Singida kuhusu mauaji ya raia mmoja kwenye mkutano wa CDM. Imeelezwa na mashahidi upande wa mashitaka kwamba wahusika walikodiwa na Mwigulu kwenda kufanya vurugu (hence Mauaji) kwenye mkutano wa CDM. Pamoja na kutajwa kwenye ushahidi, Mwigulu hajaitwa kutoa maelezo ya kuhusika kwake katika mauaji hayo.
  • Pia, Mwigulu, Nape na Riziwan walishatoa taarifa kwa nyakati tofauti kuelezea njama za kupanga mauaji za viongozi wa CDM kabla ya video yao kutoka "You Tube".
  • Nape akiwa katika mmoja wa mikutano yao huko Njombe mwezi uliopita alisikika akiwaasa wananchi wasishiriki katika mikutano ya vyama vya upinzani wanaweza kuuawa bure!(upinzani kwa Nape maana yake CDM).
  • Naibu Waziri Mwanry, Mwigulu, Nape wamenukuriwa kwa nyakati tofauti wakisema kwa gharama zozote(hata kwa kumwaga damu) meya wa Arusha hang'ooki hadi uchaguzi wa 2015.(ili kulinda maslahi yao.) Hata hivyo, maslahi hayo yana mwisho tu, yako wapi maslahi ya Sani Abbacha (Nigeria), yako wapi maslahi ya Mobutu Seseseko (Zaire) Gadafi (Libya) etc.
 
Last edited by a moderator:
Ndiyo maana Philip Malmo aliondolewa haraka nchini China mwanzo wa mwezi huu wa June 2013 kama balozi na nafasi yake ikachukuliwa na Liutenant General Abdulrahman Shimbo, mtaalaamu wa vita anayejua vifaa bora vya kijeshi na mwezi huu wa June Mwigulu naye akaenda China kwa mambo yasiyofahamika, ila kwenye bandiko lake anaelezea ziara yake nchini China ilikuwa na mafanikio ambayo hakuyaeleza.
 
Mtoa mada ameonesha udhaifu mkubwa sana ktk kudadabua hoja yake. 1. Anasema mlipuko Arusha ni nadharia pasua kichwa. Ninavyofahamu mimi kitu kinakuwa pasua kichwa kama kinakosa majibu au majibu yanatatanisha. Kwa maelezo yake utata uko wapi? wakati anaonesha dhahiri kuwa ccm wanahusika (kwa ushahidi wa mazingira). 2. Mtoa mada anaonekana ushabiki wa kisiasa unamtawala kuliko ukweli (reality). Mfano, kachambua vizuri mazingira yanayoweza kudhaniwa ccm na cdm wanahusika, lakini cha ajabu ametoa udhafu wa kuihusisha cdm TU na mlipuko kana kwamba hoja za kuihusisha ccm hazina udhaifu. Hapa ndipo umakini na ueledi wa mtoa hoja unapokuwa mashakani.
hili liko wazi na ndo maana Mwigulu ameshindwa hata kutuma salamu za pole kwa CHADEMA akiwa ndiye katibu wa Bara na Nape ametoa matusi badala ya kuwapa Wenzake pole. Hapa hata mimi mwenye Elimu ya Gumbaru nimeiona wazi kabisa kuhusika kwa CCM.
 
kwa mtazamo usiokwepeka huachi kumfikiria mwigulu na kofia yake kama ndiye mnunuzi wa hizo bidhaa.. nikiitazama hiyo kofia naona kama ni bonus baada ya kununua bidhaa mfano wa mnunuzi wa sim anapopewa na pochi ama cover kama bonus.. zaidi mtu waweza pata wazo kuwa ni mwaka huu huu ambao mwigulu ametoka china tena very recently kiasi ambacho wasambazaji na wauzaji wa bidhaa hizo hapa kwetu wasingeweza kuzipata na kuziingiza nchini this soon. Zingetoka uingereza ama ujerumani haraka ningeanza kufikiria na uwezekano wa nadharia ya kuihusisha CHADEMA otherwise not tht simple
Kununua bomu moja la kurusha?, halafu upewe zawadi ya kofia? Kaka mbona unalazimisha fikra sahihi za mwenyekiti, ingawa hazimake sense?
Silaha nyingi zinazotumiwa na magaidi ni za kutengeneza wenyewe au kutoka nchi kama China, Croatia, Ukraine .... ambapo unaweza kuzipata kimtaamtaa tu. Siyo lazima utume ujumbe wa viongozi wa juu wa nchi kwenda China kupata silaha, unaweza kuletewa mpaka mlangoni kwa kutumia mitandao ya Mafia like Russian Mafia, Triads, etc.... Kwa hiyo hapo ziara ya Kinana na Mwigulu zilikuwa siyo necessary ili kupata mabomu.

Pia, aina nyingi za silaha zinazotumiwa Africa na Central Asia, au hata Maghreb ni counterfeit weapons ambazo hata serial numbers zake zinaweza kuwa misleading. Mfano mzuri ni viwanda vya Pakistan na Philipines ambavyo ni SIDO tu za mtaani na vinatengeneza mpaka rocket launchers za kirusi, kichina, n.k

Kwa kundi binafsi lisilofungamana na Chama chochote, uwezekano wa kupata silaha toka China si mdogo. Na kwanini iwe CCM tu? Hivi Zanzibar hakujawahi lipuliwa bomu?Au kuwa na tishio la kigaidi kutoka chama fulani? Na kwanini walijitokeza sana Arusha ilhali wanajua si rahisi kupata kura? ... I'm just saying .... try to scratch your head a lil bit ..... no, the top one!!
 
Ndiyo maana Philip Malmo aliondolewa haraka nchini China mwanzo wa mwezi huu wa June 2013 kama balozi na nafasi yake ikachukuliwa na Liutenant General Abdulrahman Shimbo, mtaalaamu wa vita anayejua vifaa bora vya kijeshi na mwezi huu wa June Mwigulu naye akaenda China kwa mambo yasiyofahamika, ila kwenye bandiko lake anaelezea ziara yake nchini China ilikuwa na mafanikio ambayo hakuyaeleza.
Fikra zangu zinaanzia kwenye hoja hii!!!
 
Back
Top Bottom