Mliopangiwa Bulombola Kigoma

Mliopangiwa Bulombola Kigoma

Kilangi masanja

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
4,598
Reaction score
5,187
Wadau za Jamii Forum,

Natumaini mu wazima na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku .

Baada ya mchakato mrefu wa usaili hatimaye nimekuwa miongoni mwa watu 100 Tuliochaguliwa kujiunga na jeshi la kujenga taifa na nimepangwa kambi tajwa hapo juu, kama kuna mwana jamii mwingne aliyepangwa kambi hiyo au aliyekwsha pitia kambi hiyo atujuze detailz za kambi hiyo
 
we iyo kambi ni mwisho kama we ni legelege huna bahat na ufikishi mienzi wezio 2liena 150 2karudi 90 wengine walitoroka chamaana ukaze buti
 
Sio una bahati sema nilifanikiwa kushikwa mkono,ila ujue depo kugumu kweli ndugu yangu
 
821 KJ ukaze buti pia ujue ikiwa hauko makini hata kutoroka unaweza usiweze kamwe.
Nenda ukiwa na mawazo kuwa nitapiga depo na kumaliza salama ikiwa utajituma vizuri

Sijui uko mkoa gani lakini ikiwa mfano uko Dar kwenda Bulombora(Simbo) nauli ya basi ni 60000/- sasa hutaweza toroka na mabasi ni Sumry,Adventure,Saratoga,Mvullah,Ya Alli,Kazuge,Nbs,Sasebosa,


Nakutakia depo liwe zuri nikiamini hutakimbia
 
Tarehe ya kuripoti siijui lakini nenda kwa Mshauri wa Mgamba aliyejirani nawe huyo lazima aijue tarehe yenyewe.

Kama upo Mkoani/Wilayani
 
821 kj ukaze buti pia ujue ikiwa hauko makini hata kutoroka unaweza usiweze kamwe.
Nenda ukiwa na mawazo kuwa nitapiga depo na kumaliza salama ikiwa utajituma vizuri

sijui uko mkoa gani lakini ikiwa mfano uko dar kwenda bulombora(simbo) nauli ya basi ni 60000/- sasa hutaweza toroka na mabasi ni sumry,adventure,saratoga,mvullah,ya alli,kazuge,nbs,sasebosa,


nakutakia depo liwe zuri nikiamini hutakimbia

mtwara kaka hiyo
 
nisaidien tareh ya kuripot

swala la kuripot cdhani kama ni moja nadhani mafunzo ndo mtaanza rasmi pamoja baada ya mwezi wa usafi...jamaa angu kanambia tareh 2/3 anatakiwa kambini...kila la kheri wazee, muwe wazarendo zaidi sio kimaslai zaidi
 
Hongera sana kaka kwa nafasi adhimu uliyoipata,kambi ipo nje kidogo ya mkoa wa kigoma katika ufukwe wa ziwa Tanganyika na ndio kikosi senior miongoni mwa vikosi vya j.k.t nchini.Mafunzo sio magumu sana to the extent that hayawezi kufanyika.Vitu viwili vya msingi vya kuzingatia ni uvumilivu na morali.Ukumbuke kazi ya kumbadili RAIA kuwa ASKARI sio lelemama,so utapigwa mzigo wa maana,kero nyingi na maovyoovyo ya kutosha ili uwe askari kweli.Mengine mengi utayajua huko huko na believe me ukiwa mvumilivu na una morali utadumu chomboni.Kama alivyosema mdau hapo,sitegemei pia utoroke maana hakuna sababu ya kufanya hivyo.Najua mmeshaambiwa kwenda na trunk(soldier box),nguo chache za kiraia(usiende na nyeupe,kuna udongo mwekundu Kigoma),napendekeza tracksuit nyepesi,uende na viatu vigumu vya ngozi maana zile sare zao huwa zinachelewa sometimes.Uende na dawa baadhi za magonjwa madogo madogo ambayo huwa yanakusumbua mara kwa mara koz kule unatibiwa kijeshi pia.Mahitaji madogo madogo kama dawa ya meno,mafuta ya mgando(haya ni muhimu sana kutibia fangasi na kuapply kwenye nyayo),mswaki,nguo za ndani,nyembe za kunyolea para na usisahau fedha maana huwa kuna dharura zinatokea na simu huwa zinakusanywa.Kwa sasa niishie hapa ila kwa mwenye swali atauliza hapa
 
Hongera sana kaka kwa nafasi adhimu uliyoipata,kambi ipo nje kidogo ya mkoa wa kigoma katika ufukwe wa ziwa Tanganyika na ndio kikosi senior miongoni mwa vikosi vya j.k.t nchini.Mafunzo sio magumu sana to the extent that hayawezi kufanyika.Vitu viwili vya msingi vya kuzingatia ni uvumilivu na morali.Ukumbuke kazi ya kumbadili RAIA kuwa ASKARI sio lelemama,so utapigwa mzigo wa maana,kero nyingi na maovyoovyo ya kutosha ili uwe askari kweli.Mengine mengi utayajua huko huko na believe me ukiwa mvumilivu na una morali utadumu chomboni.Kama alivyosema mdau hapo,sitegemei pia utoroke maana hakuna sababu ya kufanya hivyo.Najua mmeshaambiwa kwenda na trunk(soldier box),nguo chache za kiraia(usiende na nyeupe,kuna udongo mwekundu Kigoma),napendekeza tracksuit nyepesi,uende na viatu vigumu vya ngozi maana zile sare zao huwa zinachelewa sometimes.Uende na dawa baadhi za magonjwa madogo madogo ambayo huwa yanakusumbua mara kwa mara koz kule unatibiwa kijeshi pia.Mahitaji madogo madogo kama dawa ya meno,mafuta ya mgando(haya ni muhimu sana kutibia fangasi na kuapply kwenye nyayo),mswaki,nguo za ndani,nyembe za kunyolea para na usisahau fedha maana huwa kuna dharura zinatokea na simu huwa zinakusanywa.Kwa sasa niishie hapa ila kwa mwenye swali atauliza hapa

Mkuu ze heby sidhani kama ana swali mana you have explain well isipokuwa jambo moja umesahau ni nidhamu na uvumilivu ni muhimu jeshini
 
"Mzalendo" ndo cheo chako kuanzia sasa. Hongera mzalendo
 
We unataka kujua detail za kambi ili ugundue nini? We kama umependa kwenda kujitolea JKT huna haja ya kuhofia huko KGM coz wapo watu wengi wamepita Na wamesavaivu. Komaa
 
Daah hongera mkuu. mimi nimepangiwa kuripoti kambi ya Kanembo, Ze Heby unaweza kunisaidia kidogo topography ya huko?
 
Last edited by a moderator:
Wa 821 kj karbuni
uzalendon raha 2pu kuru2 wa mungu mpka s/m o s/g utapitia meng la muhimu ni
OPEN THE MOYO
 
Back
Top Bottom