Buldoza
JF-Expert Member
- May 2, 2013
- 2,307
- 986
Rais kama binadamu mwingine, kuugua kwake si jambo la ajabu. Tumeshuhudia mara mbili rais akianguka kwenye mikutano ya hadhara ni zaidi ya miaka tisa sasa hata baada ya hapo hatujawahi kitangaziwa ni ugonjwa gani unaomsumbua rais wetu.
Imekuwaje leo, amefanyiwa upasuaji kwenye sehemu za siri za mwili wake ndipo waibuke watu na kuutangazia umma ugonjwa huo? Je hii si kumdhalilisha kiongozi?
Kama nia ilikuwa ni ku-divert attention ya watu toka wizi wa Escrow na kuhamia kujadili rais alikuwa na Tezidume, basi huo mpango umefeli vibaya sana.
Je waliobuni wazo hilo hawakujua kwamba hili suala la Escrow limeshavuka mipaka na kwamba linafuatiliwa na mataifa makubwa sasa na si rahisi kulizima kwa michezo ya kitoto kama huo?
Je imekuwaje rais nae akubali kujitoa kafara ya faragha yake ili kulinda ufedhuli wa Escrow kama hausiki binafsi au mwanafamilia wake?
Hii ni aibu. Rais kwa hili naye inampasa ajipime.
Imekuwaje leo, amefanyiwa upasuaji kwenye sehemu za siri za mwili wake ndipo waibuke watu na kuutangazia umma ugonjwa huo? Je hii si kumdhalilisha kiongozi?
Kama nia ilikuwa ni ku-divert attention ya watu toka wizi wa Escrow na kuhamia kujadili rais alikuwa na Tezidume, basi huo mpango umefeli vibaya sana.
Je waliobuni wazo hilo hawakujua kwamba hili suala la Escrow limeshavuka mipaka na kwamba linafuatiliwa na mataifa makubwa sasa na si rahisi kulizima kwa michezo ya kitoto kama huo?
Je imekuwaje rais nae akubali kujitoa kafara ya faragha yake ili kulinda ufedhuli wa Escrow kama hausiki binafsi au mwanafamilia wake?
Hii ni aibu. Rais kwa hili naye inampasa ajipime.