Mlioko Uingereza, msaidieni huyu mama kufahamu wanawe walipo

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,246
4,467
MSAADA TUTANI: OMBI LA KUWASILIANA NA WATOTO WALIOPO UINGEREZA KWA ZAIDI YA MIAKA 22 SASA.

87a7dba21b625a50ae6f47a140659a2c.jpg


Picha za awali za wahusika wa waraka huu ikiwa ni pamoja na watoto Amina na Seleman Kichawela na Bw. Mahmud Hassan Mihile aliyewachukua miaka 22 iliyopita ili kuwasaidia masomo huko Uingereza.

Kutokana na kichwa cha habari hapo juu mimi AZAMA ABBASI KICHAWELE ambae kwa sasa ni mjane, mwenye namba ya simu +255 784 697319 na mkazi wa Majengo Arusha, Tanzania, na ambae ni mama wa nyumbani, nachukua nafasi hii kukutaarifu kama ifuatavyo.

Mume wangu kwa majina ABBASI ALLY KICHAWELE ambaye kwa sasa ni marehemu alikua na rafiki wake wa karibu kwa majina MAHMUD HASSAN MIHILE aliekuwa akitumia namba ya simu +441332270462 wakati huo mwenye asili ya Kisomali na uraia wa Uingereza na Tanzania walikubaliana awachukue watoto wetu ambao ni:

SELEMAN ABBASI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka kumi na AMINA JABIRI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka saba aende nao Uingereza kwa ajili ya kuwasomesha.

Siku ya kuondoka watoto hawa ilikuwa ni mwaka 1994 na waliondoka na mke wa huyo Msomali kwa majina RAHMA MIHILE.

Mji wa kwanza walioshukia huko UINGEREZA unaitwa LEICESTER.

Baada ya hapo mawasiliano yaliendelea kuwepo kati ya mzazi wa kiume wa watoto na Msomali.

NB: Katika hawa watoto huyu wa kike, Amina Jabiri alikuwa ni wa mdogo wake mume wangu yaani shemeji yangu.

Kwa bahati mbaya mume wangu, aliugua maradhi ya cancer na ilipofika mwaka 1998, nikampoteza (alitangulia mbele ya haki).

Baada ya kifo cha mume wangu hakukua na mawasiliano yoyote kati yangu na huyu bwana aliyechukua watoto wangu.

Alikata mawasiliano kabisa na wala hakutaka watoto wajue kuwa baba yao hayupo tena Duniani.

Kwa bahati mbaya sikua na mtu mwingine mbadala wa kuweza kuniunganisha na huyu bwana ikizingatiwa pia mimi ni mama wa nyumbani sikuwa na PR kubwa. Leo hii ninapoandika barua hii, huu ni mwaka wa ishirini na mbili (22) toka nitengane na watoto wangu. Sisi pamoja na wanafamilia tutaendelea kutoa shukrani zetu kwa serikali ya Uingereza iwapo watoto hawa wapo salama na kwenye ajira zao. Kwetu hilo sio tatizo.

Jambo kubwa linaloniumiza ni kutokua na MAWASILIANO na watoto wangu kwa miaka ishirini na mbili sasa. Wakati mwingine najenga wasiwasi kwamba je, wako hai? Na hali hii nitaendelea nayo mpaka lini?

Huyu bwana Mahamudu (msomali) nini kimemsukuma kuwa na ujasiri wa kuwaficha watoto wangu hata nisiwe na mawasiliano nao? Ana dhamira gain?

Kutokana na maelezo mafupi hapo juu nimefikia hatua ya kuiomba ofisi yako tukufu kunisaidia kupata namna ya kuwasiliana na watoto wangu wapendwa huko waliko.

Jambo hili likifanikiwa litaleta faraja sana kwangu na kwa wana familia kwa ujumla.

Pia itakuwa ni fursa kwa watoto kutambua kuwa baba yao mpendwa alishafariki lakini mimi mama yao bado nipo hai, taarifa ambazo tuna hakika hawajazipata.

Naambatanisha picha za watoto ambazo walipigwa wakati wanakaribia kuondoka mwaka 1994.

Pia naambatinisha na picha ya Mahmud Hassan Mihile (Msomali) ya wakati huo aliyewachukua watoto kwa makubaliano na mume wangu.

NB: Kwa mawasiliano tumia namba hizi za barua pepe
hasatathuman@gmail.com
Au Athuman Rashid Mfinanga
Box 2614, - Arusha Tanzania
Ph: 0754375602/0784375602

Wako,
Katika ujenzi wa Taifa
Azama Abbasi Kichawele


Chanzo: Michuzi blog

============================
======================================
UPDATES kuhusu kupatikana kwa watoto

Kwa mujibu ya maoni ya wachangiaji (comments) kule blogi ya michuzi ilipotoka habari hiii hawa vijana wamekwisha patikana tayari wakiwa wazima na salama. Maoni hayo hapo 'sosi' ikiwa blogi ya ankal Michuzi.


January 26, 2017


blank.gif
Ok said...
Kwa taarifa za awali hawa wanaotafutwa walikabidhiwa social care walipo kua bado ni watoto.hawakuelewana kimalezi na huyo aliye wachukua. Ndugu yangu fahmi kama upo karibu na mji wa leicester jaribu kuulizia social care ya hapo pengine utapata mwangaza wapo wapi kwa sasa .itabidi ujieleze vizuri si unajua mambo ya europe hiyo ni private issue
All the best

January 27, 2017


blank.gif
Grace said...
JAMANI MIMI NI GRACE NAISHI HOLLAND. ASANTENI SANA WATOTO WAMEPATIKANA.

January 27, 2017


blank.gif
Grace said...
JAMANI MIMI NI GRACE NAISHI HOLLAND. ASANTENI SANA WATOTO WAMEPATIKANA.

January 27, 2017


blank.gif
Grace said...
JAMANI MIMI NI GRACE NAISHI HOLLAND. ASANTENI SANA WATOTO WAMEPATIKANA.

January 27, 2017


blank.gif
Abu Fahmi said...
Ndugu Hijambi na wadau wengine habari nilizopata mpk sasa watoto wamepatikana wakiwa wazima na afya njema.

Tumshukuru Mungu mkarimu kwa kuliwezesha hili Zoezi.

Alhamdulillah Rabb l aalamiin.

Mbarikiwe sana wote mlioshiriki ktk Zoezi hili.
Na km kuna Mzazi au wazazi wengine out there waliopoteza watoto wao walete habari zao hapa tuone namna gani tunaweza kusaidiana. Wasikate tamaa hata kidogo.
Ukimtegemea Mungu Hakuna kinachoshindikana.

Ndugu yenu Abu Fahmi.
United Kingdom.
 
Nimeisoma hii habari nimekumbuka mbali sana.Pole sana Mama...Tunaamini kwa umri huo wa miaka 07 na 10 bila shaka watakuwa na kumbukumbu ya mbali juu ya taswira ya Wazazi wao.

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya "Upendo" wa Wazazi na "Uono"(Sight).Ndio maana wazungu walisema "Out of Sight,Out of Mind".

Hata kama leo watakutana,lakini hakutakuwa na ile "bondism" ya Mama na Watoto,sbb kile kipindi cha kutengeneza hiyo bondism kilishapita.

Hii kwa wale wafuatiliaji wa mpira watakuwa wameiona kwa Mario Baloteli,wazazi wake walimpa Mzee Baloteli raia wa Italia kumlea Mario akiwa bado mtoto mdogo sana,kiasi Mario ana upendo wa kweli kwa baba wa kufikia kuliko kwa "Biological Parents" wake.

Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kukutana na jamaa aliyelelewa na Watawa wa Kikatoliki huko Dodoma,baada ya Wazazi wake kuwa na umasikini kiasi alikuwa na utapiamlo,alikuja kuwaona Wazazi akiwa na miaka 20.Siku alipokufa mmoja wa Wazazi wake,hakulia kama alivyolia na kugalagala kama siku aliyokufa Mtawa aliyemlea.

Tumuombee Mama Kichawele awapate watoto wake,tuombe wawe wazima...Na sisi tukumbuke kujinyima na kufanya lolote kwa ajili ya kuwekeza kwa watoto...Hujawahi kwenda kwenye msiba wa mzazi wa mwenzako na ukakuta jamaa ana-behave kama aliyefariki ni jirani na si mzazi??Ni kwa sbb wakati wa umri wa "bondism",ile bond haikushimana vilivyo.
 
Wewe ni mke wa marehemu Abbas wa Bondeni Arusha....????
Huyo Msomali Mahmood kwao ni Ngarnaro .....???
Nauliza hivyo ili nasi tuanze kukusaidia kupitia ndugu na jamaa wa Mahmood
Kama unaweza mpigie simu uongee naye vizuri, nafikiri ndiyo sababu kaweka simu.

Tunaambiwa hii habari imetolewa Michuzi kwa hiyo inawezekana aliyeandika hasomi hapa, lakini unaweza kumpata kwa simu.
 
Nimeisoma hii habari nimekumbuka mbali sana.Pole sana Mama...Tunaamini kwa umri huo wa miaka 07 na 10 bila shaka watakuwa na kumbukumbu ya mbali juu ya taswira ya Wazazi wao.

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya "Upendo" wa Wazazi na "Uono"(Sight).Ndio maana wazungu walisema "Out of Sight,Out of Mind".

Hata kama leo watakutana,lakini hakutakuwa na ile "bondism" ya Mama na Watoto,sbb kile kipindi cha kutengeneza hiyo bondism kilishapita.

Hii kwa wale wafuatiliaji wa mpira watakuwa wameiona kwa Mario Baloteli,wazazi wake walimpa Mzee Baloteli raia wa Italia kumlea Mario akiwa bado mtoto mdogo sana,kiasi Mario ana upendo wa kweli kwa baba wa kufikia kuliko kwa "Biological Parents" wake.

Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kukutana na jamaa aliyelelewa na Watawa wa Kikatoliki huko Dodoma,baada ya Wazazi wake kuwa na umasikini kiasi alikuwa na utapiamlo,alikuja kuwaona Wazazi akiwa na miaka 20.Siku alipokufa mmoja wa Wazazi wake,hakulia kama alivyolia na kugalagala kama siku aliyokufa Mtawa aliyemlea.

Tumuombee Mama Kichawele awapate watoto wake,tuombe wawe wazima...Na sisi tukumbuke kujinyima na kufanya lolote kwa ajili ya kuwekeza kwa watoto...Hujawahi kwenda kwenye msiba wa mzazi wa mwenzako na ukakuta jamaa ana-behave kama aliyefariki ni jirani na si mzazi??Ni kwa sbb wakati wa umri wa "bondism",ile bond haikushimana vilivyo.


Mkuu barafu, heshima kwako mzee wangu.

Naomba kufahamu... ni UMRI upi haswa (kwa mtoto) wa kucreate na kustrengthen hiyo "bondism" ? you have just notified kwamba AGE hiyo ishapita kwa hao watoto, ila hukuutaja huo umri wenyewe.

Umetoa maelezo mazuri sana... useful to vijana wote kama mimi ambao tunaelekea kuwa wazazi or walezi.

-Kaveli-
 
Pole mama kwa Hili unalopitia tumwombe Mungu watoto wawe salama , hakika tunapaswa kujitahidi kujinyima na kulea watoto Wetu katika Hali yoyote tunayopitia haijalishi kipato wala Hali zetu kumpa MTU watoto ni risk kubwa sana na tunapoteza nafasi ya kujenga upendo
 
Wewe ni mke wa marehemu Abbas wa Bondeni Arusha....????
Huyo Msomali Mahmood kwao ni Ngarnaro .....???
Nauliza hivyo ili nasi tuanze kukusaidia kupitia ndugu na jamaa wa Mahmood

Watanzania wengi tuna akili nzito sana.

Hapo juu mleta mada kaweka wazi kabisa kuwa TANGAZO hili kaliCOPY from MICHUZI blog. Halafu wewe unaanza kuuliza maswali, unamuuliza mleta mada?

Chukua hizo namba za simu wasiliana na huyo mama direct, coz yawezekana huyo mama sio member wa JF, ndo maana kaweka contacts zake.

-Kaveli-
 
Yaani mtu ukisikia uingereza au Nchi za Nje unaona ndio maisha sasa huko akifanikiwa atakujali na wakati ulikimbia majukumu na shemeji katengeneza choyo na wakwangu nae aende! Yaani doooo !vumilia tu atarudi!
 
Shukran kwa ushauri mzuri saana.Nilikurupuka kwani huyo Abbas ni kijana wetu...Ahsante
Pole
Watanzania wengi tuna akili nzito sana.

Hapo juu mleta mada kaweka wazi kabisa kuwa TANGAZO hili kaliCOPY from MICHUZI blog. Halafu wewe unaanza kuuliza maswali, unamuuliza mleta mada?

Chukua hizo namba za simu wasiliana na huyo mama direct, coz yawezekana huyo mama sio member wa JF, ndo maana kaweka contacts zake.

-Kaveli-
Haku dhamiria....
 
Copied from MICHUZI BLOG: MSAADA TUTANI: OMBI LA KUWASILIANA NA WATOTO WALIOPO UINGEREZA KWA ZAIDI YA MIAKA 22 SASA.

MSAADA TUTANI: OMBI LA KUWASILIANA NA WATOTO WALIOPO UINGEREZA KWA ZAIDI YA MIAKA 22 SASA.

87a7dba21b625a50ae6f47a140659a2c.jpg


Picha za awali za wahusika wa waraka huu ikiwa ni pamoja na watoto Amina na Seleman Kichawela na Bw. Mahmud Hassan Mihile aliyewachukua miaka 22 iliyopita ili kuwasaidia masomo huko Uingereza.

Kutokana na kichwa cha habari hapo juu mimi AZAMA ABBASI KICHAWELE ambae kwa sasa ni mjane, mwenye namba ya simu +255 784 697319 na mkazi wa Majengo Arusha, Tanzania, na ambae ni mama wa nyumbani, nachukua nafasi hii kukutaarifu kama ifuatavyo.

Mume wangu kwa majina ABBASI ALLY KICHAWELE ambaye kwa sasa ni marehemu alikua na rafiki wake wa karibu kwa majina MAHMUD HASSAN MIHILE aliekuwa akitumia namba ya simu +441332270462 wakati huo mwenye asili ya Kisomali na uraia wa Uingereza na Tanzania walikubaliana awachukue watoto wetu ambao ni: SELEMAN ABBASI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka kumi na AMINA JABIRI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka saba aende nao Uingereza kwa ajili ya kuwasomesha.

Siku ya kuondoka watoto hawa ilikuwa ni mwaka 1994 na waliondoka na mke wa huyo Msomali kwa majina RAHMA MIHILE.

Mji wa kwanza walioshukia huko UINGEREZA unaitwa LEICESTER.
Baada ya hapo mawasiliano yaliendelea kuwepo kati ya mzazi wa kiume wa watoto na Msomali.

NB: Katika hawa watoto huyu wa kike, Amina Jabiri alikuwa ni wa mdogo wake mume wangu yaani shemeji yangu.

Kwa bahati mbaya mume wangu, aliugua maradhi ya cancer na ilipofika mwaka 1998, nikampoteza (alitangulia mbele ya haki).

Baada ya kifo cha mume wangu hakukua na mawasiliano yoyote kati yangu na huyu bwana aliyechukua watoto wangu. Alikata mawasiliano kabisa na wala hakutaka watoto wajue kuwa baba yao hayupo tena Duniani.

Kwa bahati mbaya sikua na mtu mwingine mbadala wa kuweza kuniunganisha na huyu bwana ikizingatiwa pia mimi ni mama wa nyumbani sikuwa na PR kubwa.

Leo hii ninapoandika barua hii, huu ni mwaka wa ishirini na mbili (22) toka nitengane na watoto wangu. Sisi pamoja na wanafamilia tutaendelea kutoa shukrani zetu kwa serikali ya Uingereza iwapo watoto hawa wapo salama na kwenye ajira zao. Kwetu hilo sio tatizo.

Jambo kubwa linaloniumiza ni kutokua na MAWASILIANO na watoto wangu kwa miaka ishirini na mbili sasa. Wakati mwingine najenga wasiwasi kwamba je, wako hai? Na hali hii nitaendelea nayo mpaka lini?

Huyu bwana Mahamudu (msomali) nini kimemsukuma kuwa na ujasiri wa kuwaficha watoto wangu hata nisiwe na mawasiliano nao? Ana dhamira gain?

Kutokana na maelezo mafupi hapo juu nimefikia hatua ya kuiomba ofisi yako tukufu kunisaidia kupata namna ya kuwasiliana na watoto wangu wapendwa huko waliko. Jambo hili likifanikiwa litaleta faraja sana kwangu na kwa wana familia kwa ujumla.

Pia itakuwa ni fursa kwa watoto kutambua kuwa baba yao mpendwa alishafariki lakini mimi mama yao bado nipo hai, taarifa ambazo tuna hakika hawajazipata. Naambatanisha picha za watoto ambazo walipigwa wakati wanakaribia kuondoka mwaka 1994.

Pia naambatinisha na picha ya Mahmud Hassan Mihile (Msomali) ya wakati huo aliyewachukua watoto kwa makubaliano na mume wangu.

NB: Kwa mawasiliano tumia namba hizi za barua pepe
hasatathuman@gmail.com
Au Athuman Rashid Mfinanga
Box 2614, - Arusha Tanzania
Ph: 0754375602/0784375602

Wako,
Katika ujenzi wa Taifa
Azama Abbasi Kichawele
Mama kama angekuwa na kopi ya paspoti za hao watoto angeenda ubalozini kutoa taarifa ingalikuwa ni rahisi zaidi kusaidiwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom