Mlinzi mpya wa Dr. Slaa


Polisi mmeshindwa.
 
Huyu kijana anahitaji mafunzo yapo ya wiki moja tu ili ajue ABC ya kazi yake. Angalia jinsi miguu yake ilivyo hapo, anaweza kuanguka. Jinsi alivyosimama haonekani kumpa cover nzuri boss wake.
 
Jamaani huu si ndio ubwanyenye Nyerere alioupiga vita. Hata gari ufunguliwe mpango?
 
pause yake inakaa poa kumlima ngwala na akadondoka mithili ya kifurushi
 
Inaonekana hajui kazi yake maana mpaka bosi wake anafungua mlango yeye ndo anarukia kuufungua!

Halafu mkao huo wa ufunguaji kibaka pale akitaka kumpiga nondo ya kichwa au ngwala slaa wala hamna kipingamizi.Nilishasema Kazi za ulinzi ni fani watu wanasomea sio kila baunsa kilabu cha mbege kwa mbowe anakuwa mlinzi.Huyo mlinzi atakuwa mchaga tu.
 
frema120

===> Kumbe hawa walinzi huwa wanaokotwa tu? Wanapata wapi mafunzo ya ulinzi hasa ya kulinda viongozi?

===> Na yeye ni bei gani? i.e thamani yake, kilo na nusu au dau lake litaongezeka kidogo?

Kajaribu kumsogelea Dr.Slaa ndiyo utamjua FBI ni nani!!!
 
Halafu mkao huo wa ufunguaji kibaka pale akitaka kumpiga nondo ya kichwa au ngwala slaa wala hamna kipingamizi.Nilishasema Kazi za ulinzi ni fani watu wanasomea sio kila baunsa kilabu cha mbege kwa mbowe anakuwa mlinzi.Huyo mlinzi atakuwa mchaga tu.


Duh uongo wako umekuwa mkubwa sanaa bhanaa,jionee aibu wewe mwenyewe,mkubwa mzima kusema uongo!!!!
 
Hapana huyu kijana, ana mafunzo ya ulinzi kayapata nchi tatu yupo vizuri, tumtie moyo.

Hizo nchi tatu ni zipi? Na alikwenda kupata mafunzo kwa ridhaa ya chama au aliwahi kuwa mtumishi wa mojawapo wa vyombo vya ulinzi&usalama?
 
Mlinzi gani huyu mdebwedo kofi moja tu huyu ana dondoka chini hata ngumi hajui kwanza mwili mwenye hana amechoka
 
Hapana huyu kijana, ana mafunzo ya ulinzi kayapata nchi tatu yupo vizuri, tumtie moyo.



Tazama hiyo picha uone makosa ya kiulinzi, kwa mtu aliyesomea "ulinzi" nchi tatu hawezi kufanya makosa namna hiyo hata chembe. Na kama ni kweli kasomea nchi tatu, basi hayupo vizuri.
 
Mlinzi hana mafunzo yoyote ya kiu salama hajui hata code za ulinzi wewe mwangalie anavyo fungua mlango hayuko makini kabisa.

Mnaokota watu vijiweni mnawaita walinzi hana hata element moja yakuwa mlinzi semeni CCM wakupeni vijana ile front line ya Mkuu wa nchi usipime hata kidogo vijana wapo fit wale ndio walinzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…