Dah! nakumbuka Tabora! Enzi nacheza kama centre forward , kwenye kombe la kuku, na udhamini wa kupata tango kutoka kwa diwani Lugembe Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
Walewale akina Bujibuji!
Hii kitu ya Mwanjelwa, opposite na soko kuu linalojengwa. Tulikuwa tukichezea hapo, kabla yule jamaa hajaweka kituo cha mafuta (BP).
Walewale akina Bujibuji!
Hii kitu ya Mwanjelwa, opposite na soko kuu linalojengwa. Tulikuwa tukichezea hapo, kabla yule jamaa hajaweka kituo cha mafuta (BP).
Bwahahahahhh!
We chiboko, hats off!
Hapo pekundu, umeniacha hoi, Nadhani ni miaka ile ambapo pale kwenye kilima (juu kidogo ya transfoma) palikuwa na kokoto na kakipande ka lami kidogo upande mmoja, possibly mpaka mitaa ya shule ya Maanga. Kile kilima kimeua na kujeruhi sana vijana, hasa wakiwa wameziachia baiskeli zao kutoka Makunguru.
Thanks Bujibuji kwa kumbukumbu hii muhimu.
Bwahahahahhh.
Walewwale. Mnachukua sukani za magari mnapigilia kwa misumari kwenye beringi zenu ili muendeshe kwa urahisi kwenye kona, often without brakes! Ni mteremko upi unaongelea wewe, ule wa kuja Uwanja wa Sokoine (kutoka Isanga) ama ule wa kwenda Makunguru (kutoka Isanga).
Watu bwana, kumbe mmeficha vipaji namna hii?
Mpira wa madaso, miaka ya 80 hadi 90 nikiwa nasoma Kiloleli, Masanza kona nimecheza sana. Nilikuwa kipa mkali mno, nisipocheza timu inafungwa mvua ya magoli