KWELI Mlevi wa kupindukia akisitisha ghalfa unywaji wa Pombe anaweza kupoteza Maisha

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Mdau mmoja wa JamiiForums ameelezea kuwa watu wanaokunywa pombe kupita kiasi (Ulevi uliopindukia) wakiacha ghafla matumizi ya pombe wanaweza kufa.

istockphoto-1179962667-612x612.jpg
Mdau huyu anaeleza kuwa pombe hupunguza utendaji wa akili kama yalivyo madawa mengine ya kulevya, pia huleta uraibu na utegemezi.

Amewashauri walevi sugu kuacha pombe taratibu ili wasipatwe na athari kubwa kwenye afya, ikiwemo kifo kutokana na kifafa.

Madai haya ni sahihi?
 
Tunachokijua
Kama ilivyo kwa aina nyingine za uraibu, unywaji wa pombe uliopindukia husababisha mabadiliko ya kemikali kwenye ubongo ambayo huleta utegemezi kwa mhusika. Ubongo unapotengeneza uraibu na utegemezi wa pombe, inakuwa karibu haiwezekani kwa mtumiaji kufanya kazi bila pombe.

Kwa mlevi, kunywa pombe kunaweza kuonekana kuwa muhimu kwa maisha yake ya kila siku kuliko kitu kingine chochote. Kusitisha ghafla unywaji huathiri ubongo kwa kusababisha dalili zenye maudhi madogo yanayovumilika au makali kiasi cha kuua.

Baadhi ya dalili za kujiondoa kwenye matumizi ya pombe (Alcohol Withdrawal Symptoms) ni kutetemeka, kukosa usingizi, kichefuchefu na kutapika, kukosa hamu ya kula, kuweweseka na maumivu makali ya kichwa. Kwa mujibu wa tafiti, 3% ya watu wanaositisha ghafla matumizi ya pombe hupatwa na aina kali ya kifafa inayoweza kuwa hatari kwa afya, hata kuua.

Kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya kuaminika, ikiwemo taasisi ya IARC, JamiiForums imebaini kuwa usitishaji wa ghafla wa matumizi ya pombe kwa walevi wa kupindukia unaweza kuwaletea changamoto nyingi kwa afya, ikiwemo kifo, kutokana na kifafa kisichotibika kirahisi.

Katika hatua za kusitisha matumizi ya pombe, wataalam wa afya hushauri jambo hili lifanyie taratibu ili kuepusha maudhi na dalili kubwa zinazoweza kutokea.

Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa na Vyakula ya Marekani (FDA) imepitisha matumizi ya dawa tatu zinazoweza kumsaidia mtu kusitisha matumizi ya pombe;
  • Acamprosate husaidia kupunguza ukubwa wa maudhi baada ya kusitisha matumizi.
  • Disulfiram husababisha maudhi kwa mhusika hasa kiungulia na kutapika ikiwa atakunywa pombe au hata kusikia harufu yake. Hii humfanya aanze kuiepuka.
  • Naltrexone husaidia kupunguza hamu ya kunywa.
Pia, dawa zinazopatikana kwenye kundi kubwa la Benzodiazepines kama vile diazepam, lorazepam na chlordiazepoxide husaidia kupunguza maudhi yanayoweza kumpata mhusika anapokuwa kwenye zoezi la kusitisha matumizi ya pombe.
Ila odds za basketball huwezi acha 😂😂😂
Hahaha! Umenifurahisha mkuu... Umenifanya nicheke! Na sikuwa na mpango wa kucheka kabisa mzee hii wiki mzima!

Nimekuwa verry disappointed! Odd 10, odds 50 hadi odds 300 mzee najikunja kufanya vetting... ng'ombe Moja ya mwisho inakuja niharibia mwishoni kabisa! Nahisi nna mkosi! Mara 3 mfululizo!? Why me!? Nimeamua nikae pembeni kidogo mzee ..
 
Hakuna cha kufa wala nini. Kinachotokea ni kupata mfadhaiko wa hisia sababu ya kusosa kilevi. Pombe ina uraibu kama ule anaokutana nao mvuta bangi, sigara, au mpiga punyeto.

Pombe haina faida mwilini zaidi ya kuchosha viungo muhimu kama Ini, figo,moyo na kongosho.
 
Wewe ulikuwa ni moderate drunk tu. Acha kwa waliofikia level ya asipokunywa mikono inatetemeka mpaka kuongea vizuri anashindwa.
Una uhakika na unachokiongea!? Nimemaliza mwaka bado tatizo la vibration lipo na halijaisha! Ingawa limepungua kama KWA asilimia 25 hadi 30 tu.... Nilikuwa mlevi mzee! Nisipokunywa naweweseka usiku kucha..HADI kupiga kelele usiku kama nimepandwa na malaria kichaa!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom