Mkwawa: Shujaa au muonezi

Mkwawa: Shujaa au muonezi

AFRIKAN GUY

Member
Joined
Jun 26, 2015
Posts
67
Reaction score
74
harakati za mkwawa zilikua ni kukamata himaya moja baada ya nyingine na kuifanya yake. na alizikamata kwa nguvu. inshort alikua mkoloni na na yeye kwa makabila ya jirani. Hakupanga kuacha, mpaka alipokutana na mjerumani.

Tunapozungumzia Mkwawa, mara nyingi tunamwona kama shujaa wa kitaifa kwa sababu ya ujasiri wake katika kupinga Wajerumani.

mkwawa alikua anapigana na wajerumani ili kulinda himaya zake, na sio kulinda taifa. Infact makabila aliyo yaonea, walikua wanafurahia kuona mkwawa anapigana vita inayomgharimu sana, waliomba apigwe. ili wawe huru.

Historia ya Mkwawa inatufundisha kuwa shujaa wa kitaifa si lazima awe mzalendo kwa wote. Wakati mwingine, tunapojivunia mashujaa wetu, tunapaswa kutambua kwamba hadithi yao ina nyuso nyingi, na baadhi ya nyuso hizo zinaweza kuwa za udhalimu na ukandamizaji kwa wengine. Hii ni changamoto kubwa kwa namna tunavyoiandika historia yetu.

Watu waliompa Mkwawa sifa ya ushujaa wa taifa, walimpa baada ya wao kushuhudia ukatili wa mjerumani dhidi yetu. kwa kufanya hivyo, walituaminisha kwamba mkwawa alikua anapigana kumtimua mjerumani tanganyika. kumbe sio. Mkwawa alikua busy kumpiga mjerumani ili aendeleze harakati zake za kuteka himaya moja baada ya nyingine kwa mabavu.
 
harakati za mkwawa zilikua ni kukamata himaya moja baada ya nyingine na kuifanya yake. na alizikamata kwa nguvu. inshort alikua mkoloni na na yeye kwa makabila ya jirani. Hakupanga kuacha, mpaka alipokutana na mjerumani.

Tunapozungumzia Mkwawa, mara nyingi tunamwona kama shujaa wa kitaifa kwa sababu ya ujasiri wake katika kupinga Wajerumani.

mkwawa alikua anapigana na wajerumani ili kulinda himaya zake, na sio kulinda taifa. Infact makabila aliyo yaonea, walikua wanafurahia kuona mkwawa anapigana vita inayomgharimu sana, waliomba apigwe. ili wawe huru.

Historia ya Mkwawa inatufundisha kuwa shujaa wa kitaifa si lazima awe mzalendo kwa wote. Wakati mwingine, tunapojivunia mashujaa wetu, tunapaswa kutambua kwamba hadithi yao ina nyuso nyingi, na baadhi ya nyuso hizo zinaweza kuwa za udhalimu na ukandamizaji kwa wengine. Hii ni changamoto kubwa kwa namna tunavyoiandika historia yetu.

Watu waliompa Mkwawa sifa ya ushujaa wa taifa, walimpa baada ya wao kushuhudia ukatili wa mjerumani dhidi yetu. kwa kufanya hivyo, walituaminisha kwamba mkwawa alikua anapigana kumtimua mjerumani tanganyika. kumbe sio. Mkwawa alikua busy kumpiga mjerumani ili aendeleze harakati zake za kuteka himaya moja baada ya nyingine kwa mabavu.
Swali zuri sana hili na linaonyesha namna historia inaweza kuangaliwa kwa mitazamo tofauti.

Mutwa Mkwavinyika alikuwa chifu wa Wahehe, na jina lake limebaki kwenye kumbukumbu za historia kwa sababu ya vita kali alivyopigana dhidi ya Wajerumani mwishoni mwa karne ya 19. Sasa, hoja yako ina sura mbili:

1. Mkwawa kama Shujaa
Mkwawa aliongoza upinzani mkali dhidi ya ukoloni wa Kijerumani. Wakati Wajerumani walipojaribu kuteka ardhi ya Wahehe, Mkwawa na askari wake waliwapiga vita kwa uhodari. Vita kama ile ya Lugalo mwaka 1891, ambako Wahehe waliwaua mamia ya askari Wajerumani, ilionyesha ushujaa wake wa kulinda ardhi, watu na uhuru wa kabila lake dhidi ya wakoloni.

Katika muktadha huu, kupigana na Wajerumani ni ushujaa — kwa sababu ilikuwa vita ya kujitetea dhidi ya uvamizi wa mgeni aliyeleta unyonyaji, dhuluma na uvunjaji wa mila za Kiafrika.

2. Mkwawa kama Muonezi
Lakini kabla ya ujio wa Wajerumani, Mkwawa alikuwa akipanua himaya ya Wahehe kwa kuvamia na kuteka maeneo ya makabila mengine kama Wabena, Wakinga, na Wanyakyusa. Alikuwa na jeshi kubwa na aliwatawala walioshindwa kwa mkono wa chuma. Hapa, anaweza kuchukuliwa kama muonezi, kwa sababu alitumia nguvu kutawala na kupanua himaya yake — kama ilivyokuwa kawaida kwa machifu wengi wa Kiafrika wa wakati huo.

Kulinda Himaya au Kulinda Taifa?
Wakati alipopigana na Wajerumani, lengo lake lilikuwa zaidi kulinda himaya yake na mamlaka yake kama chifu wa Wahehe, lakini kwa namna isiyo ya moja kwa moja, alichangia pia katika mapambano ya kitaifa dhidi ya ukoloni — jambo ambalo linampa hadhi ya kishujaa kwa historia ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Hitimisho
Mkwawa alikuwa shujaa na muonezi kwa nyakati tofauti — kama tunavyoona kwa viongozi wengi wa kijadi duniani. Ushujaa wake mkubwa unaonekana zaidi katika mapambano dhidi ya Wajerumani, ambapo alisimama kama kiongozi wa mapambano ya kiafrika dhidi ya ukoloni.

Karibu sana Kalenga uje ufaidi ulasi,ugimbi bagia na mishikaki.Nyama ya Mbwa walitusingizia tu hatuli.
 
Dunia ndio iko hivyo... Mbabe na wanyonge, kila himaya itahitaji kujitanua zaidi na zaidi kwa sababu tofauti, iwe kuongeza eneo lenye rutuba, madini etc,
 
Wakati alipopigana na Wajerumani, lengo lake lilikuwa zaidi kulinda himaya yake na mamlaka yake kama chifu wa Wahehe, lakini kwa namna isiyo ya moja kwa moja, alichangia pia katika mapambano ya kitaifa dhidi ya ukoloni — jambo ambalo linampa hadhi ya kishujaa kwa historia ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Hii ina make sense. Kwamba MKWAWA alikua hana habari kabisa swala utaifa na ukoloni. mjerumani kwake alikua kama adui mtu mwingine tu! aliesimama katikati ya harakati zake za kutawala kila ardhi anayo iona mbele yake.
 
Hitimisho
Mkwawa alikuwa shujaa na muonezi kwa nyakati tofauti
Mkwawa alikua muonezi Tu mwenye majivuno. na swala la yeye kujiua linathibitisha kiwango cha majivuno alionayo.

pengine aliwaza moyoni mwake, kuhusu uonezi alio ufanya kwa makabila mengine ya karibu. watamuonaje, na makabila hayo watamfanya nini. ndipo sa akaamua kuutoa uhai wake.
 
Hii ina make sense. Kwamba MKWAWA alikua hana habari kabisa swala utaifa na ukoloni. mjerumani kwake alikua kama adui mtu mwingine tu! aliesimama katikati ya harakati zake za kutawala kila ardhi anayo iona mbele yake.
Enzi hizo kila chief alikuwa na eneo lake la utawala .
 
harakati za mkwawa zilikua ni kukamata himaya moja baada ya nyingine na kuifanya yake. na alizikamata kwa nguvu. inshort alikua mkoloni na na yeye kwa makabila ya jirani. Hakupanga kuacha, mpaka alipokutana na mjerumani.

Tunapozungumzia Mkwawa, mara nyingi tunamwona kama shujaa wa kitaifa kwa sababu ya ujasiri wake katika kupinga Wajerumani.

mkwawa alikua anapigana na wajerumani ili kulinda himaya zake, na sio kulinda taifa. Infact makabila aliyo yaonea, walikua wanafurahia kuona mkwawa anapigana vita inayomgharimu sana, waliomba apigwe. ili wawe huru.

Historia ya Mkwawa inatufundisha kuwa shujaa wa kitaifa si lazima awe mzalendo kwa wote. Wakati mwingine, tunapojivunia mashujaa wetu, tunapaswa kutambua kwamba hadithi yao ina nyuso nyingi, na baadhi ya nyuso hizo zinaweza kuwa za udhalimu na ukandamizaji kwa wengine. Hii ni changamoto kubwa kwa namna tunavyoiandika historia yetu.

Watu waliompa Mkwawa sifa ya ushujaa wa taifa, walimpa baada ya wao kushuhudia ukatili wa mjerumani dhidi yetu. kwa kufanya hivyo, walituaminisha kwamba mkwawa alikua anapigana kumtimua mjerumani tanganyika. kumbe sio. Mkwawa alikua busy kumpiga mjerumani ili aendeleze harakati zake za kuteka himaya moja baada ya nyingine kwa mabavu.
Mambo haya ni kama kugeuza shilingi tu

Mfano pale CDM leo kuna kundi linaona linaonewa na utawala unawapuuza kwa kuwaita majina mabaya mabaya unadhani hawakufurahia lililomkuta mwenyekiti
 
Tena Mkwawa alikuwa katili kuliko Wajerumani. Watu wa nyanda za juu kusini wakisikia Wahehe walikuwa wanatetemeka kwa uoga. Wajerumani wakati wanachunguza koloni loa waliambaa na mto Ruvuma, wakafika ziwa Nyasa, wakasafiri hadi Kyela. Wakawa wanapanda kwenda Usangu. Eneo lote kuanzia Kyela walikuta watu wanatetemeka sababu ya Wahehe. Alipofika Usangu Chief wao akataka sana wamsaidie kuwapiga Wahehe, lakini wakakataa, wakisema wamekuja kupandisha bendera yao.

Wasangu kuonewa na Wahehe ilikuwa kama kisasi, huko nyuma kulikuwa na Wasangu waliojiita Warori. Walikuwa wanatembea eneo lote la nyanda za juu na kati, ikiwemo uhehe, wakipora na kuua kila wapitapo.
 
Hii ina make sense. Kwamba MKWAWA alikua hana habari kabisa swala utaifa na ukoloni. mjerumani kwake alikua kama adui mtu mwingine tu! aliesimama katikati ya harakati zake za kutawala kila ardhi anayo iona mbele yake.
Utaifa unakuja kwa. Sababu alipigana na mgeni ambae alikuwa anataka kuteka na kutawala ardhi ya Tanzania iliyopo kwenye eneo la Iringa hivyo dhana taifa lazima iwepo hapa.
 
Utaifa unakuja kwa. Sababu alipigana na mgeni ambae alikuwa anataka kuteka na kutawala ardhi ya Tanzania iliyopo kwenye eneo la Iringa hivyo dhana taifa lazima iwepo hapa.
lakini tatizo linakuja pale ambapo ukijua kwamba, kipindi hicho kulikua hakuna kitu kinaitwa utaifa, wala tanganyika wala tanzania.

kipindi hiko kulikua na makabila tu, na kabila lolote lenye nguvu lilikua linataka kutanua ardhi ya kabila lake.
 
Bora Mkwawa kuliko Mangungo wa Msowero.
 
lakini tatizo linakuja pale ambapo ukijua kwamba, kipindi hicho kulikua hakuna kitu kinaitwa utaifa, wala tanganyika wala tanzania.

kipindi hiko kulikua na makabila tu, na kabila lolote lenye nguvu lilikua linataka kutanua ardhi ya kabila lake.
Na kuitazama mfumo unavyoendelea kwa dunia ya sasa ni badiliko la mfumo tu.Angalia ukraine,gazza sirria na kwingineko hali ni ile ile.KWA hiyo neno taifa linabadilishwa na mazingira tu.
 
Na kuitazama mfumo unavyoendelea kwa dunia ya sasa ni badiliko la mfumo tu.Angalia ukraine,gazza sirria na kwingineko hali ni ile ile.KWA hiyo neno taifa linabadilishwa na mazingira tu.
mkwawa anatoka taifa la wahehe, alikua anapita akikama na kupora ardhi za mataifa mengine kama wabena wakinga etc.

lakini kamwe hakuwahi kupigania taifa linaloitwa tanzania au tanganyika.
 
mkwawa anatoka taifa la wahehe, alikua anapita akikama na kupora ardhi za mataifa mengine kama wabena wakinga etc.

lakini kamwe hakuwahi kupigania taifa linaloitwa tanzania au tanganyika.
Ni sawa hata taifa Tanzania halikuwepo pia sasa angepigania Tanzania ipi mkuu.?
 
Back
Top Bottom