MKUYUNI, Mwanza: Mamba aliyekula watu 8 na mifugo auawa kwa mtego wa ndoano

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
413bbea9f209dfb3ab09333ae37b6d89.jpg

Mamba anayesadikiwa kula zaidi ya watu wanane na kuendelea kutishia maisha ya binadamu na mifugo kandokando ya Ziwa Victoria katika Kata ya Mkuyuni jijini Mwanza kwa muda mrefu. Hatimaye ameuawa baada ya kunaswa na ndoano iliyotegwa na wananchi kwa siku tatu mfululizo

Mamba huyo ameokotwa na wavuvi hii leo majira ya Alfajiri akiwa amekufa huku akielea juu ya maji katika mwalo la Butimba uliopo mtaa wa Kang'ata kata ya Mkuyuni jijini Mwanza

Kunaswa na kuuawa kwa mamba huyo kumeibua furaha kwa wakazi wa eneo hilo ambao kwa miaka mitatu iliyopita walilazimika kuchukua tahadhari kila wanapofanya shughuli zao kwenye mwalo huo

Katibu wa Kitengo cha Kudhibiti na kuzuia Uvuvi Haramu na Utunzaji wa Mazingira ya Ziwa Victoria (BMU), Robert Charles alisema mamba huyo alinaswa baada ya kuwekewa mtego wa ndoano eneo la Butimba

Mamba huyo ambaye hakujulikana kama ni dume au jike, anakisiwa kuwa na urefu wa futi 18, sawa na mita tano na nusu

Mwenyekiti wa BMU kata ya Mkuyuni, Lornard Mpemba amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mamba huyo alikuwa akifika eneo hilo akitokea eneo la Saanane, umbali wa kilometa mbili kutoka eneo mamba alikouliwa.

Chanzo : ITV channel
 
413bbea9f209dfb3ab09333ae37b6d89.jpg


Mamba anayesadikiwa kula zaidi ya watu wanane na kuendelea kutishia maisha ya binadamu na mifugo kandokando ya Ziwa Victoria katika Kata ya Mkuyuni jijini Mwanza kwa muda mrefu, hatimaye ameuawa baada ya kunaswa na ndoano iliyotegwa na wananchi kwa siku tatu mfululizo

Mamba huyo ameokotwa na wavuvi hii leo majira ya Alfajiri akiwa amekufa huku akielea juu ya maji katika mwalo wa mswahili uliopo mtaa wa Kang'ata kata ya Mkuyuni jijini Mwanza

Mamba huyo ambaye hakujulikana kama ni dume au jike, anakisiwa kuwa na urefu wa futi 18, sawa na mita tano na nusu.

Huyu mamba manka namfahamu sana kwa jinsi alivyokua anamnyanyasa BwasheeChanzo : ITV channel
 
Aiseee bonge la dude...
Mbona huyo alikuwa bado mdogo sana
413bbea9f209dfb3ab09333ae37b6d89.jpg


Mamba anayesadikiwa kula zaidi ya watu wanane na kuendelea kutishia maisha ya binadamu na mifugo kandokando ya Ziwa Victoria katika Kata ya Mkuyuni jijini Mwanza kwa muda mrefu, hatimaye ameuawa baada ya kunaswa na ndoano iliyotegwa na wananchi kwa siku tatu mfululizo

Mamba huyo ameokotwa na wavuvi hii leo majira ya Alfajiri akiwa amekufa huku akielea juu ya maji katika mwalo wa mswahili uliopo mtaa wa Kang'ata kata ya Mkuyuni jijini Mwanza

Mamba huyo ambaye hakujulikana kama ni dume au jike, anakisiwa kuwa na urefu wa futi 18, sawa na mita tano na nusu.

Chanzo : ITV channel
 
413bbea9f209dfb3ab09333ae37b6d89.jpg


Mamba anayesadikiwa kula zaidi ya watu wanane na kuendelea kutishia maisha ya binadamu na mifugo kandokando ya Ziwa Victoria katika Kata ya Mkuyuni jijini Mwanza kwa muda mrefu, hatimaye ameuawa baada ya kunaswa na ndoano iliyotegwa na wananchi kwa siku tatu mfululizo

Mamba huyo ameokotwa na wavuvi hii leo majira ya Alfajiri akiwa amekufa huku akielea juu ya maji katika mwalo wa mswahili uliopo mtaa wa Kang'ata kata ya Mkuyuni jijini Mwanza

Mamba huyo ambaye hakujulikana kama ni dume au jike, anakisiwa kuwa na urefu wa futi 18, sawa na mita tano na nusu.

Chanzo : ITV channel
Mkuu kumbe.
Nilipita asubuhi nikakuta watu kibao nikadhani ni ajali labda. Hata hivyo sikuona dalili za ajali kama vile magari yaliyohusika ama vyombo vingine. Nilibaki najiuliza bila majibu.
Asante kwa taarifa.
 
Back
Top Bottom