Mkuu wa Wilaya ya Mkalama amemfukuza kazi Afisa Afya wa Wilaya kwa makosa ya Ubadhirifu

RUCCI

JF-Expert Member
Oct 6, 2011
1,701
1,714
attachment.php


Mkuu wa wilaya ya Mkalama mkoani Singida, Christopher Ngubiangai, amemsimamisha kazi Afisa Afya wa Wilaya hiyo, bwana James Ndembo, kwa muda usiojulikana kufuatia wizi wa zaidi ya shilingi milioni 19.

Ngubiangai amemtuhumu Ndembo kwa wizi wa fedha hizo zilizotengwa ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya magonjwa yasioambukizwa. Amedai kuwa Ndembo alitoa fedha kiasi cha shilingi 25,151,430 benki na kuzihifadhi kwa mweka hazina wa Manispaa ambapo amekuwa akichukua kiasi cha pesa katika nyakati tofauti kwa ajili ya matumizi binafsi.

Ndembo alijaribu kukimbia lakini amekamatwa na sasa yuko chini ya ulinzi.

Ngubiangai ameonya watumishi wa umma dhidi ya wizi wa fedha za umma, tabia ambayo inakwamisha maendeleo. Amesema watakaobainika kufanya hivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.
 

Attachments

  • 7584.jpg
    7584.jpg
    18.5 KB · Views: 9,025
Hizi hasira hizi hivi baadaye kukiwa na kesi na ikaonekana tofauti nani atakayekuwa anairipia hasira hizi au tuanzishe gachacha
 
Mamlaka ya nidhamu ya Afisa afya si mkuu wa wilaya hata kidogo naona hii serekali ya Magufuli ikiparaganyika kwa kushindwa kufuata sheria,kanuni na taratibu.
 
Mamlaka ya nidhamu ya Afisa afya si mkuu wa wilaya hata kidogo naona hii serekali ya Magufuli ikiparaganyika kwa kushindwa kufuata sheria,kanuni na taratibu.

Kama hujui vitu ni bora ukae kimya tu kuliko kuanika upumbavu wako hapa.
 
Kama hujui vitu ni bora ukae kimya tu kuliko kuanika upumbavu wako hapa.

Kujifanya unajua kila kitu, ndio kunakufanya kuwa mbumbumbu wa mambo.

Mamlaka ya kinidhamu wa Afisa afya ni Mkuu wa Wilaya? Yeye alipaswa kutoa ushauri kwa Mkurugenzi wa Wilaya uli afanye uchunguzi na kutoa maamuzi juu ya mtumishi huyu.

Naamini Mkurugenzi atafuata sheria na sio kupelekeshwa tu na mijitu isiyojua utawala wa sheria kama hamy B
 
Kujifanya unajua kila kitu, ndio kunakufanya kuwa mbumbumbu wa mambo.

Mamlaka ya kinidhamu wa Afisa afya ni Mkuu wa Wilaya? Yeye alipaswa kutoa ushauri kwa Mkurugenzi wa Wilaya uli afanye uchunguzi na kutoa maamuzi juu ya mtumishi huyu.

Naamini Mkurugenzi atafuata sheria na sio kupelekeshwa tu na mijitu isiyojua utawala wa sheria kama hamy B

Mkurugenzi wa wilaya ndio nini!?
 
Kwanini hakuambiwa kuzirudisha kama wale wa EPA, ESCROW au hawa waliokwepa kodi bandarini?

Nchii hii umeanza kuwa ya watanzania wa daraja LA juu ambao sheria haziwahusu na makabwela ambao wakifanya hivyo huozea jela,
 
Huyo inapaswa apigwe ndoo za kutosha ajifunze tatzo anakamatwa baada ya muda anaonekana mtaani afu anahamishwa kazi
 
Kujifanya unajua kila kitu, ndio kunakufanya kuwa mbumbumbu wa mambo.

Mamlaka ya kinidhamu wa Afisa afya ni Mkuu wa Wilaya? Yeye alipaswa kutoa ushauri kwa Mkurugenzi wa Wilaya uli afanye uchunguzi na kutoa maamuzi juu ya mtumishi huyu.

Naamini Mkurugenzi atafuata sheria na sio kupelekeshwa tu na mijitu isiyojua utawala wa sheria kama hamy B

Huyo ndivyo alivyo
 
We nae vipi bana? Mkurugenzi wa halmashauri

Sasa mkurugenzi wa halmashauri na mkuu wa wilaya nani mkubwa? Ni sawasawa na kusema rais hana mamlaka, ila katibu mkuu kiongozi ndio anayo. Acheni upumbavu wa kuzungusha mikono...fanyeni utafiti...wakuu wa mikoa na wilaya ni watu wazito sana TAMISEMI. Hivyo ishu yoyote inayohusu watumishi wa umma katika wilaya au mkoa...ipo chini ya mamlaka ya wakuu wa wilaya na mikoa respectively. Wakuu wa wilaya ndio wawakilishi wa rais katika wilaya husika. Sio nafasi ndogo hii.

Kinacho wakera wengi ni kuona kuwa wakuu hao wa wilaya na mikoa ni makada wa CCM...mmesahau kuwa hata rais wa nchi nae ni kada wa CCM...hahahaha
 
Sasa mkurugenzi wa halmashauri na mkuu wa wilaya nani mkubwa? Ni sawasawa na kusema rais hana mamlaka, ila katibu mkuu kiongozi ndio anayo. Acheni upumbavu wa kuzungusha mikono...fanyeni utafiti...wakuu wa mikoa na wilaya ni watu wazito sana TAMISEMI. Hivyo ishu yoyote inayohusu watumishi wa umma katika wilaya au mkoa...ipo chini ya mamlaka ya wakuu wa wilaya na mikoa respectively. Wakuu wa wilaya ndio wawakilishi wa rais katika wilaya husika. Sio nafasi ndogo hii.

Kinacho wakera wengi ni kuona kuwa wakuu hao wa wilaya na mikoa ni makada wa CCM...mmesahau kuwa hata rais wa nchi nae ni kada wa CCM...hahahaha


Acha uwongo Wewe.
Mbona wakuu wengine wa mikoa hutoa mapendekezo kwa mkurugenzi ili hatua zichukuliwe?

Mkuu wa mkoa au mkuu wa wilaya hana mamlaka ya kumsimamisha kazi hata mwalimu.
 
Mkuu huyo jamaa anaitwa James Ndimbo ni Ktibu wa Afya,

nzi hizo Mzumbe tulikuwa tunamwita mzee wa totoz naona yamemkuta
 
Kwa issue za wizi na ushahidi ukiwepo NDIO MKUU wa Wilaya anakufukuza kazi na kifungo juu...sasa wewe mtu kahamisha fedha ya kuelimisha wananchi juu ya afya...halafu unaona sawa?...Penye ukweli kuweni na uwazi...
 
Back
Top Bottom