Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini akibeba Boksi

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini akibeba Boksi

Huyu Richard kasesera aka dibo ni mtu wa sifa,kimbelembele tu....hata huo ukuu wa wilaya sjui mkoa kaupata kwa akili ya sifa ....
Na bado mtaona mengi kutoka kwake...
 
View attachment 333126
Mkuu wetu wa wilaya ya Iringa akiwa amebeba box huku akitizama camera...


Huku sasa ni kuwa Juha Kalulu ..nafikri watu hawajaelewa Dhana ya hapa kazi tu.......kila mtu anatakiwa kuwajibika kwa kazi yake

Kama DC au watawala wafanye kwa makini kwa bidii Yale yote yaliyo kwenye Job description ...zao
Kama ni mesenja pia ..Kama mfagiaji ..au kuli wa kupakia mizigo

Sasa sidhani Kama tutapima utendaji wa Mkuu wa wilaya kwa kuangalia uwezo wake wa kubeba box

Au kumpima waziri kwa uwezo wake wa kufagia...........

Anaweza kufanya kwenye matukio Maalum Kama siku ya usafi na kadhalika ....lakini sio ndio iwe utaratibu.....

Kwenye Tukio la ajali DC ataangaliwa namna anavyoweza kuratibu...mambo yakaenda na sio kukimbilia kupiga picha
 
Ikumbukwe kuna kipindi wakati wa kuomba kura za
ubunge,huwa kuna vituko vinajitokeza kama vile
watu kuwapigia magoti wapiga kura,kuongea kilugha kwenye kampeni
kuamkia watoto wadogo shikamoo n.k.
sasa sijui kama uteuzi wa wakuu wa wilaya umeishapita au bado.
ila ninachokumbuka ni msemo mmoja maarufu "Hapa kazi tu"
 
bila shaka alimkabidhi mtu kisimu chake cha Kichina ili akitoka tu amfotoe.chezeya kutafuta kick kwa magu nyie.
 
Huyu jamaa hasalimiki maana anafanya mambo ya kijipu jipu tu
 
Back
Top Bottom