Mkuu wa mkoa wa Tanga nae atangaza vita dhidi ya dawa za kulevya

Baba Munah

Member
Feb 7, 2017
19
49
Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigella ametangaza rasmi vita dhidi ya dawa za kulevya kwa kuwataka wenyeji wa maeneo ya mpakani kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa ya kuwafichua na uhalifu huo.

Kauli hiyo ameitoa wakati akizindua zoezi la uandikishaji wa wa wahamiaji walowezi mkoani hapa. Amesema viongozi wa vijiji watakaobainika kushirikiana na wauzaji wa dawa za kulevya hususan mirungi ambayo inatoka nchi jirani watashughulikiwa.

Aidha shigella amewaasa wananchi kuacha uvuvi haramu pamoja na biashara za magendo na kubainisha kuwa serikali ya mko imeunda kikosi maalum ambacho kitashugulikia wanajihusisha na uhalifu huo.

Mkoa wa Ruvuma umeingia makubaliano ya ushirikiano wa kibiashara na uchumi kati ya wilaya tatu za nchini Malawi Chitipa,Nkatabei na Kalonga zinazopakana na mikoa ya Ruvuma na Mbeya nchini Tanzania makubaliano ambayo yatawapa fursa wafanyabiashara wa nchini Malawi kutumia bandari ya Mtwara kupitia Ruvuma na kuvuka ziwa Nyasa badala ya kutumia bandari ya Beila ya nchini Msumbiji.Geofrey Nilahi anataarifa Zaidi.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake katibu tawala wa mkoa wa Ruvuma Hasan Bendeyeko amesema kuwa hivi karibuni timu ya viongozi wa mkoa wa Ruvuma pamoja na viongozi wa wizara ya mambo ya nje walikuwa na kikao cha pamoja cha ushirikiano wa kudumu kuimarisha mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Malawi wafanyabiashara waangalie namna wanavyoweza kuitumia fulsa hiyo kwa maendeleo yao na taifa.

Naye afisa biashara mkoa wa Ruvuma Nehemia James amesema kuwa kufunguka kwa barabara ya Mtwara Cordal Malawi itakuwa ni sehemu ya soko la bidhaa za Tanzania.


8f0775b43a8f942a8a98fa577f786283.jpg
 
Safi sana .
Nilidhani nchi hii ina mkuu wa mkoa mmoja tu anayemwakilisha rais na kutekeleza sera za kupambana na uhalifu.
Nilijua ni Makonda peke yake.
Ni jambo la kushukuru Mungu kuwa ametokea mkuu wa mkoa mwingine kuendeleza hii vita.
Naona mawaziri husika wamekaa kimya.

Nilidhani waziri wa afya na ustawi wa jamii naye angekuja na tamko la kuwapima damu wale waliotajwa ili kubaini ukweli.


Hii vita wakiachiwa watu wachache itashindikana kwani inaonekana kuwa ina mtandao mrefu sana .

Sheria ibadilishwe ili wanaothibitishwa wauwawe mara moja kwa kunyongwa adharani.

Watu waovu wakichekewa na kupewa heshima kubwa watageuka na kuwadhuru watu wema.
Tatizo ni kuwa watu waovu wanatoa hongo sana ndio maana wanapata watetezi kila kona .
Matokeo yake jamii inajaa watu waovu na wema wanaangamizwa.
 
Safi sana ...... Hongera sana sana RC Tanga.... Mwisho itafikia hakuna pa kukimbilia.... Big UP!
 
Makonda ni Messi ana uwezo mkubwa wa kudribo na ball control kitu ambacho bwana Shigella Diego Costa hawezi.


Halafu watu wa Tanga ukicheza nao lazima wakuzawadie Bushaaa
 
Makonda ni Messi ana uwezo mkubwa wa kudribo na ball control kitu ambacho bwana Shigella Diego Costa hawezi.


Halafu watu wa Tanga ukicheza nao lazima wakuzawadie Bushaaa
Acha kumfananisha Messi na vitu vya kijinga
 
Back
Top Bottom