mkafrend
JF-Expert Member
- May 12, 2014
- 3,045
- 1,503
WanaJF, Salaam!
Nilikuwa natazama chanzo kimoja cha televisheni mchana saa nane 18/12/2015 katika habari hiyo nimemsikia akitamka kwamba kuanzia sasa hataki kuona wala kusikia habari za ulipaji wa posho za vikao kwa watumishi.
Habari hii imenishtua kidogo kwa kuwa kimsingi fedha zinazotekeleza shughuli hizo zilishaidhinishwa na kuzitumia kwa kazi nyingine bila kibali cha Wizara ya Fedha kinatoa nafasi kwa CAG kutoridhishwa matumizi ya fedha hizo.
Aidha, binafsi nadhani kilichotakiwa kufanyika ni kuanza na maandalizi ya bajeti hii kwa Makatibu Wakuu wa Wizara kuainisha maeneo ambayo katika bajeti ijayo si lazima kuzingatiwa ili fedha zake zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo au kwingineko panapostahili.
Najiuliza maswali mengi nikitilia mashaka ya baadhi ya viongozi kutomwelewa vizuri Mhe. JPM na kuanzisha vitu vitakavyoleta chuki miongoni mwa jamii hasa itakapotokea wana habari kuripoti juu ya matumizi yasiyo sahihi ya fedha za serikali kutokana na kubadilishiwa matumizi.
Tusikurupuke, tujuwe nn tunapaswa kukifanya na matokeo yake baadae
Ushauri tu!
Nilikuwa natazama chanzo kimoja cha televisheni mchana saa nane 18/12/2015 katika habari hiyo nimemsikia akitamka kwamba kuanzia sasa hataki kuona wala kusikia habari za ulipaji wa posho za vikao kwa watumishi.
Habari hii imenishtua kidogo kwa kuwa kimsingi fedha zinazotekeleza shughuli hizo zilishaidhinishwa na kuzitumia kwa kazi nyingine bila kibali cha Wizara ya Fedha kinatoa nafasi kwa CAG kutoridhishwa matumizi ya fedha hizo.
Aidha, binafsi nadhani kilichotakiwa kufanyika ni kuanza na maandalizi ya bajeti hii kwa Makatibu Wakuu wa Wizara kuainisha maeneo ambayo katika bajeti ijayo si lazima kuzingatiwa ili fedha zake zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo au kwingineko panapostahili.
Najiuliza maswali mengi nikitilia mashaka ya baadhi ya viongozi kutomwelewa vizuri Mhe. JPM na kuanzisha vitu vitakavyoleta chuki miongoni mwa jamii hasa itakapotokea wana habari kuripoti juu ya matumizi yasiyo sahihi ya fedha za serikali kutokana na kubadilishiwa matumizi.
Tusikurupuke, tujuwe nn tunapaswa kukifanya na matokeo yake baadae
Ushauri tu!