Mkuu wa Mkoa Dar, Jipime kuhusu Taka zilizorundikana Barabarani

sasa kwanini usingejitolea kwenda mamlaka usika ku report wakautoe..? umekuja ku report JF ?

Mimi hili suala huwa silipendi hata kidogo. Watu wa mazingira ni kazi yao na wanalipwa sio kusafisha na kuzoa taka tu, bali hata kuvumbua mbinu kupunguza uchafu kusambaa. Wao hawalipwi kukaa ofisini na kusubiri simu tuwaarifu uchafu uko wapi. Ikiwa mimi mkaazi au mpita njia nauona uchafu ama chanzo cha uchafu, inatakiwa yeye awe keshauona na keshautafutia ufumbuzi. Iwe nikitokezea kupiga simu basi jawabu lake liwe tushapata taarifa hiyo na tuko njiani kutatuwa hilo tatizo.

La muhimu kuwe na sheria ya wananchi kuweza kuwashitaki hawa watu kama wanvyotushitaki sisi. Kiweko kitengo maalumu kinachojitegemea katika halmashauri ambapo mwananchi anakwenda kutoa mashitaka yake, na kama hichi kitengo wataona kuna mashiko juu ya haya malalamiko ya wananchi basi hawa mazingira washitakiwe na watoleshwe fine au hata kifungo cha jela. Hapo tunaweza kukaa sawa. Lakini hii ya kwa sasa kuwa wanatushitaki sisi tu, ni uonevu mtupu. There are always two sides of a coin

Kuhusu huyu ku report hapa JF, namuunga mkono, kwani anajuwa habari kwa kupitia JF zitawafika walengwa na mabosi wao kwa haraka zaidi kuliko ku report kwao.
 
Ni WAKATI SASA SERIKALI ZA UKAWA KATIKA MANISPAA ZA DAR WAFANYE KWELI KUSHUGULIKIA HILI JAMBO LA UCHAFU TUONE KWELI WAMEDHAMIRIA KUWATUMIKIA WANANCHI NA PO POTE WALIPO WASIKAE KULALAMIKA TU NA KUKOSOA MPIRA UPO ENEO LAP
 
Nimepitia manyanya nikaingia mpaka kwa pinda nikatokeA mkwajuni...nikarudi na bararbara nikaingia ujiji ndani, nikarud mwananyamal ...nikazama kutokea mahakama ya kinondoni mpaka Biafra mitaa yote inanuka vibaya kwa uozo wa taka.
Studio unaitwa uchafu wa magufuli ila uku mwananyamala wanauita uchafu wa Uhuru!!
Kwa kweli nahisi kuna njama za uongozi wa mikoa na wilaya wa kumkamisha rais ili ionekane order yake ilifeli efficiently!!!
 
Kwani huki ulikojaa uchafu si pengine serikali za mitaa ni ukawa ama wao wanahisi ni sawa ?

kwingine walizoa taka wakachoma sasa nyie mumezoa mukazitupa barabarani, haya halmashauri iko chini yenu leteni magari ya taka sio kulalama tu.
 
Mimi hili suala huwa silipendi hata kidogo. Watu wa mazingira ni kazi yao na wanalipwa sio kusafisha na kuzoa taka tu, bali hata kuvumbua mbinu kupunguza uchafu kusambaa. Wao hawalipwi kukaa ofisini na kusubiri simu tuwaarifu uchafu uko wapi. Ikiwa mimi mkaazi au mpita njia nauona uchafu ama chanzo cha uchafu, inatakiwa yeye awe keshauona na keshautafutia ufumbuzi. Iwe nikitokezea kupiga simu basi jawabu lake liwe tushapata taarifa hiyo na tuko njiani kutatuwa hilo tatizo.

La muhimu kuwe na sheria ya wananchi kuweza kuwashitaki hawa watu kama wanvyotushitaki sisi. Kiweko kitengo maalumu kinachojitegemea katika halmashauri ambapo mwananchi anakwenda kutoa mashitaka yake, na kama hichi kitengo wataona kuna mashiko juu ya haya malalamiko ya wananchi basi hawa mazingira washitakiwe na watoleshwe fine au hata kifungo cha jela. Hapo tunaweza kukaa sawa. Lakini hii ya kwa sasa kuwa wanatushitaki sisi tu, ni uonevu mtupu. There are always two sides of a coin

Kuhusu huyu ku report hapa JF, namuunga mkono, kwani anajuwa habari kwa kupitia JF zitawafika walengwa na mabosi wao kwa haraka zaidi kuliko ku report kwao.

kazi ya kuzoa taka ni kazi ya halmashauri na majiji yote yako chini ya ukawa haya fanyeni kazi basi, mameya mumeshachagua fanyeni kazi au munasubiri semina elekezi?
 
Rais alionyesha mfano wa nini kinachotakiwa na kufanywa na wananchi wote. Kubeza kiongozi wa sasa ambaye ameonesha kwa vitendo kinachotakiwa kufanyika ni utovu ufinyu wa kufikiri. Utashi wa viongozi wetu na watendaji ni mdogo ndio maana hali iko hivyo na wamekosa ubunifu. Rais hawezi kukuambia kila kitu cha kufanya wakati unapokea mshahara kila mwezi
 
Huyo Mkuu wa Mkoa wa Dar alishashindwa kazi, mtakumbuka aliyekuwa waziri wa Mazingira wakati ule Dr. Huvisa alianzisha utaratibu wa kufanya usafi kila jumamosi ya kwanzan ya mwezi na siku ya usinduzi wa kampeni hiyo Makamu wa Rais Mstaafu Dr Bilal alifagia. Kilichotokea baada ya hapo ni wafanyakazi na wanajeshi ndo walikuwa wanafagia maeneo mbalimbali baada ya muda mfupi zoezi likakoma. Nakumbuka kuna siku Clous walizungumza nao hewani kuwa Dar ni chafu na ile kampeni yakufagia imeeishia wapi. Waziri alisema ameshindwa baada ya kukwamishwa na watendaji, na Mkuu wa Mkoa huyuhuyu alisema Dar ni jiji Kubwa na linawatu wengi na ni ngumu kulinganisha na Mji wa Moshi au Kigali Rwanda ambako kunawatu wachache. Nilimwona amefilisika kwa fikra kwasabau kuna majiji Duniani yana watu ambao ni nusu ya watanzania wote mill 45 lakini ukipita mitaani hukuti aina yoyote ya uchafu, mfano Jiji la Osaka Japan lina watu milioni 37.83, Shanghai milioni 22.99, Osaka-Japan 20.12, New york Marekani watu milionin 18.59, Beijing China watu milioni 19.52, Cairo Misri watu milioni 18. 41 lakini ukipita mitaani ni kusafi utazani hakuna watu. Sasa Dar watu Milioni 4 tu watu visingizio kibao ooh watu wengi n.k inamaana ukipelekwa uwe Osaka hufai kupewa hata uongozi wa mtaa maana hao milioni 4 na ushee wa Dar ni mtaa tu Osaka. Hawawezi kwenda na kasi ya Magufuli ushauri wa bure ni kuachia ngazi tu wawaachie wenye uwezo wafanye kazi. Nadhani hata hizo nafasi za ukuu wa mikoa na wilaya wapigiwe kura ili wakishindwa wapigwe chini tu. Katiba Mpya
 
Lema hawezi kupita ubunge mie ndo nakwambia...

kwa maana hiyo wewe ndio unaechagua? sasa hivi tumetoka kupiga kura katika mstari tuliokuwa tumesimama tulikuwa watu kama Ishirini hivi kati ya hao kumi na saba wote tulikuwa watu wa upande wa Lema, labda kama mnamikakati ya wizi unaoujua wewe
 
Hili zoezi lilikuwa na malengo mazuri na wote tulipenda lifanikiwe na liwe endelevu lakini inaonekana liliendeshwa pasipo mikakati na malengo maalumu.Labda kama kulikuwa na malengo ya PR ya kisiasa.Kwa nini wasingetenga mafungu kiasi toka pesa zilizo okolewa kutoka gharama za sherehe za uhuru kwa ajili ya kukodi agari ya kuzoa hizo taka?Kwa jinsi mambo yanavyoenda napata mashaka makubwa muda ukifika mipango ya kutoa elimu bure itakuwa na kasheshe la aina yake,only time will tell.

Maeneo mengi kuna watu wanakula tenda za kusafisha na kuzoa taka.

Labda wamekasirika hakuna ulaji wanaogopa wamezoea kutokusafisha na kula pesa na hawanunuhi vifaa wala kuajiri ipasavyo

Kweli inasikitisha kusoma taka bado zipo barabarani

Mkuu wa mkoa,asipojipanga akapumzike
 
Wakuu wa mikoa nao wakuwafanyia sub, maana wanaonyesha wazi kabisa wanahujumu jitihada za magufuli kama anavyofanya huyu wa Dar!

Ampige chini, amteue mwingine!
 
Rais alitangaza tarehe 09.12.2015 ni sikukuu ya uhuru itakayoadhimishwa kwa kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni mbinu ya kupambana na kipindupindu.

Nchi nzima ikiwemo Dsm watu walijitokeza na kufanya usafi kisha kulundika taka ktk maeneo fulani.

Cha kushangaza hadi leo baadhi ya maeneo tska hazijazolewa na Mkuu wa mkoa bado anacheka na watendaji wake.

Nataka nimkumbushe kuwa kutozolewa kwa taka hizo tafsiri yake kwa wananchi mnataka kasi ya utendaji wa serikali ya awamu ya tano ionekane ni nguvu ya soda.

Mkuu wa mkoa punguza maneno walime barua wakurugenzi vinginevyo wewe mwenyewe jipime ktk nafasi yako kama unataka kuendelea kuwa nayo.
 
Wasaidizi wa Mheshimiwa Rais wapaswa wafanye tathmini waone miji, mitaa na vitongoji vitavyokuwa bado vimerundika uchafu ndani ya wiki moja baada ya sherehe ya uhuru. Wazembe wpte wawajibishwe: fukuza, funga au weka ndani!!!
 
Nimeenda Soko la Kisutu kuna lundo la Uchafu linatoa harufu kupita maelezo khah!
 
Miaka 54 ya uhuru hakuna ufumo thabiti wa ukusanyaji na utupaji takataka ngumu mijini; hakuna mfumo thabiti wa afya ya jamii (public health system); hakuna mifumo ya maji taka (sewarage systems) mijini (iliyopo kidogo ni ile iliyoachwa na wakoloni); na hakuna maji safi ya bomba. Barabara mijini hazina mitaro ya maji ya nvua na zile chache zilizonayo mitaro imeziba kutokana na kutokufanyiwa maintenance. Moja ya sababu ya kuwepo serikali na wananchi kulipa kodi ni ili hizi huduma ziwepo kikamilifu. Kukosekana kwa hizi huduma ndicho chanzo hasa cha maisha duni ya wananchi mijini na maradhi kama kipindupindu. Hiyo kampeni ya Magufuli ya 'kufanya usafi' ni usanii, kejeli na kutafuta umaarufu wa kisiasa wa reja reja. Matatizo yako pale pale na wala hakuyagusia na hatayagusia!

Well said mkuu!!!
 
Nimefanikiwa leo kusafiri kwa pikipiki maeneo mbali mbali ya Jiji la DAR. Nimetokea ubungo hadi Mabobo nikaelekea Mwananchi CL. Nilichokiona huko service road ni uchafu umerundikwa hauna mzoaji.

Nimeshangaa sana pale dereva bodaboda alipo niambia wanauita uchafu wa magufuli, Nilipo toka Mwananchi nikaelekea maeneo ya Buguruni jamani ni shiiiiida. Naaamini bila shaka viongozi wetu, Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya, wenye tender za usafi, Madiwani, Watendaji wa kata, wenyeviti wa mitaa, mabwnana/bibi afya na wadau mbali mbali mumo humu. Saidieni hizi juhudi za wananchi mtawavunja moyo siku nyingine, maana wataona haina maana.

Tafadharini sana fanyeni hima kabla mvua kubwa haijanyesha, Huo uchafu utatapakaa kila sehemu na utaziba mitalo, Hatari ya magonjwa ya milipuko ni kubwa.

Asanteni na Hongereni kwa kuwa viongozi wa jiji la Dar.

Asante kaka kwa taarifa hii,Yaani haya ndio matatizo ya kukurupuka,matatizo ya kutaka sifa,matatizo ya kuamua bila ushauri......Kwanini pesa alizozikusanya za shere za uhuru asikodishe gari za kukusanya hizo taka,,,
 
Miji na vijiji vingi havijatenga maeneo ya dampo, hakuna mipango, hakuna mikakati. Mbele hatua moja nyuma nne. Je tutafika?
 
Back
Top Bottom