Kiranga,Uhuru kaja kama Deputy PM according to the caption.
Kwa hiyo ni sawa hata wakikutana publicly kwa sababu hajaja kama mgombea, bali kama kiongozi.
Hata Obama akifanya ziara nje sasa hivi anapokewa rasmi, watu hawawezi kusema "tusimpokee rasmi kwa sababu uchaguzi uko karibu" kwa sababu kwa sasa ndiye rais, kama alivyo Uhuru kwa sasa Deputy PM.
Swali hapa labda liwe reciprocity, kwa nini tusione PM Pinda akimpokea Deputy PM WA Kenya na badala yake tunaona rais? Lbda washapokelewa na Pinda wanaenda ku pay a homage visit kwa rais na sio kwamba wanapokelewa rasmi na rais.Labda, maana Tanzania haina itifaki, hata meya wa Nairobi anaweza kupokelewa na rais wa Tanzania kama ana deal la kuvutia.
Hayo mambo ya deals na "stake holders mapping" tushayafanya tangu enzi za Mugabe anaishi Four flats Upanga anaendesha ki Volkswagen, Mondlane anaishi Kinondoni, Kabila anaishi Msasani, Museveni na Tito Okello wanaishi Upanga Mindu St, John Garang anaishi Upanga Mathuradas et cetera, et cetera, kwa hiyo Kikwete anayajua ukizingatia kashakaa Foreign Affairs miaka kumi akifundwa na Che Nkapa.
Hata angekuwa deputy secreatry wa commerce kutoka Marekani nakuhakikishia Kikwete angekutana naye. Anapenda sana kujionyesha kuwa yeye ni internationalist.