Swagatwende
Member
- Mar 1, 2012
- 38
- 9
Acha utani , tujuze vizuri ina maana hata walimu wameshtuka !!R.I.P CCM,
Acha utani , tujuze vizuri ina maana hata walimu wameshtuka !!R.I.P CCM,
Upepo wa kisiasa unaelekea kukiendea kombo chama cha CCM kwani kwa taarifa nilizopata kwa mmoja wa washiriki kwamba mkutano uliofanyika jana kata ya Kikatiti ulikosa watu sana sana wanafunzi wa shule tu. Hali hiyo inasemekana kufanana na ilivyotokea kata ya Songoro alikotokea Nassari kwani walikosa watu kiasi cha kuahirisha mkutano.Hali hii ilisabisha makada wa CCM kukasirika na kuporomosha matusi.
Kama kuna mwenye taarifa zaidi atujuze.
we nani kakwambia kuna mtu hamwogopi Mungu hapa. Kama yaliyoletwa ni uongo basi ulete ukwelijamani acheni uongo muogopeni mungu
Upepo wa kisiasa unaelekea kukiendea kombo chama cha CCM kwani kwa taarifa nilizopata kwa mmoja wa washiriki kwamba mkutano uliofanyika jana kata ya Kikatiti ulikosa watu sana sana wanafunzi wa shule tu. Hali hiyo inasemekana kufanana na ilivyotokea kata ya Songoro alikotokea Nassari kwani walikosa watu kiasi cha kuahirisha mkutano.Hali hii ilisabisha makada wa CCM kukasirika na kuporomosha matusi.
Kama kuna mwenye taarifa zaidi atujuze.
Mwigulu Nchemba
Ndivyo mnavyojidanganya kuwa ccm mambo yanawaendea kombo, hivi nyie mpo dunia ya wapi? dunia iliyo mbali na uhalisia wa mambo? subirini kipigo mtakachokipata sijui kama mtaongea nini tena!!! nilikuwa nabisha lakini kumbe ni kweli CHADOMO
SISI NI CCM DAMU: wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Kikatiti wakishadadia CCM wakati wa mkutano wa kampeni za CCM Kata ya Kikatiti
Msanii wa TOT anayekwenda kwa jina la Juakali, akihamasisha watu, baada ya mgombea wa CCM Arumeru Mashariki, Sioi Sumari na Mratibu kampeni za CCM Mwigulu Nchemba (kulia) kupanda jukwaani katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo Kata ya Kikatiti A Town.
Sioi akikasalimia katoto kwenye mkutano huo
Mgombea ubunge wa CCM jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari akiwasalimia wapigakura wake, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kijiji cha Mikandini jimboni humo. Kulia ni Mratibu wa kampeni za CCM jimboni humo, Mwigulu Nchemba.
NI CCM TU: Kina mama na kina baba wa kijiji cha Mikandini wakishangilia kwenye mkutano uliofanyika katika kijiji hicho.
Hii ni siku ile ya ufunguzi ambapo tulienda kumsikiliza Mh. Rais mstaafu Mkapa akaishia kututukana na kuelezea koo za watu. Kuanzia siku ile tumekoma kabisa kwenda kuwasikiliza hawa watu. Mbaya zaidi tumeikia eti siku ile alikuwa anatania, kumbe kampeni zao ni kuja kutuelezea utani badala ya kunadi sera ili tuzipime na kuchagua zipi zitatufaa kutukomboa. Nahisi uwelewa wa DEMOKARASIA kwa wenzetu ni mdogo sana, pamoja na kuwa CCM damu nilishabadilisha maamuzi tayari. Ni demokrasia tu