Mkutano wa Askofu Gwajima Mbezi Luis 25/09/2016

Mkutano wa Askofu Gwajima Mbezi Luis 25/09/2016

Hapa niko Mortuary naandaa kuleta Maiti ifufuliwe, nifanyie booking kabisa
Yaani wewe umenikumbusha MAREHEM Much Mtikila alivyojitolea kumsaidia yule kijana aliyedhulimiwa laki zake sita . Wana Jf mnakumbuka lakini?
 
Karibu katika mkutano wa ishara na miujiza uliokwisha kuanza hapa viwanja vya mbezi luis, unaoongozwa na Bishop Josephat Gwajima njoo ushuhudie wafu wakifufuliwa na misukule ikirudishwa kwa Jina la Yesu.
 
Nipo uwanjani wakuu naiona Chopa hapa Gwajima katua muda huu
 
Gwajima asituchoshe aende pale muhimbili wamfungilie majokofu ya maiti afufue watu hii biashara ya kuandaa mizuka kwenye mikutano yake ni usanii usiovumilika. Serikali pigeni marufuku mambo kama haya yanachangia kuturudisha nyuma sana.
 
Wanabodi hapa mbezi kuna mkutano mkubwa wa Injili wa Askofu Gwajima ametua na chopa jamaa huku hammer zake mbili zikija na watu wengine
Ameruhusu afisa mwanamke kutoka TRA anatoa elimu ya kodi na namna ya kudai risiti
Kwangu mm nimehesabu kama kitendo cha kizalendo katika nchi hii kwani nimeona ni uzalendo.
Serikali imetumia halaiki hii ya mkutano kutoa taarifa zao.
 
Alichikula msikule sasa anasema alipelekw Gamboshi kijiji kina itwa mwadila shinyanga
 
Ni kweli wajinga ndio waliwao! unakuta mtu na akili zake anaenda kwa waganga wa kienyeji wanakula pesa zake wakati kwa Yesu uponyaji ni bureeeeee!
Unakuta mtu mzima mvaa suruali wa asili lakini anapoteza pesa zake kwa makahaba na hiyo tamaa ya uzinzi haipungui ndo inazidi kuongezeka mwishowe anakufa kwa ukimwi au anatelekeza familia wakati kwa Yesu angesamehewa dhambi zake na kufunguliwa kwenye vifungo vya uzinzi!
Unakuta mtu mzima anamalizia pesa kwenye ulevi mpaka anashindwa kutimizia familia yake mahitaji muhimu kama ya chakula , shule na mavazi wakati kwa Yesu angeokolewa! Kwa kweli wajinga ndio waliwao!
Ni kweli kwa Yesu uponyaji ni bure, lakini kwa "watumishi hawa wa siku za mwisho" ni ghali kuliko hata kwa waganga wa kienyeji. Kwa mfano, kuna huyu anayejiita Suguye yuko Kivule Matembele kumwona tu kueleza tatizo lako ni laki unusu, na baada ya hicho kiasi kwa ajili ya usajili, unapaswa pia kuorodheshwa kama "TV Partner" unaweka commitment ya kulipia gharama za uanzishwaji na uendeshaji wa tv yake, kila mwezi unatakiwa kulipia kiasi kisichopungua laki moja. Na ujue mtu kuacha uzinzi au ulevi sio lazima aende kwa "hawa watumishi wa siku za mwisho" Yesu wa kweli ndiye anayemgusa mtu na kumwondoa katika ukahaba, uzinzi; nakadhalika, na haijalishi uko kwa Gwajima au uko bar wakati huo. Yesu akikutaka anakufuata kokote uliko. Hii inaweza kuhitaji ufafanuzi mrefu kidogo, lakini ili uelewe kuwa huu ndio ukweli ndio maana huko huko kwa "watumishi wa siku za mwisho" waumini wanaziniana wao kwa wao, na "watumishi" nao wanazini na waumini! Simameni imara msiyumbishwe na lugha tamu tamu za "wahubiri wa siku za mwisho"!
 
1474814713500.jpg
1474814781704.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom