Mkutano wa Askofu Gwajima Mbezi Luis 25/09/2016

Mkutano wa Askofu Gwajima Mbezi Luis 25/09/2016

malkiamrembo

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2015
Posts
386
Reaction score
231
Wakuu habari za jioni..Napenda kufahamisha kuwa naanzisha Uzi ambao utakuwa nawapa Updates za kila kinachotokea kwa Mkutano Wa Askofu Gwajima ambao unafanyika pale mbezi Luis mkabala na Stand ya magari.

Mkutano huo utaanza Tar. 25.09.2016 (kesho kutwa) mpaka Tar.02.10.2016 katika uwanja wa Mbezi luis pale kuanzia SAA Tisa Alasiri..ukihudhuliwa na Waimbaji mbali mbali kama;

Atosha kisava, John lisu, Masanja Mkandamizaji, Bahati Bukuku, Mercy Masika, Angle Bernard, Glorious celebratio, Mwanamapinduzi, Catheline Mkoma, Madam Flora na wengine...

Askofu Gwajima pamoja na maelfu ya watenda kazi watakuwepo kuwasaidia wote walioonewa na ibilisi.

Kama una ndugu ambae ni mgonjwa au Hospitali hawaoni ugonjwa, na wenye mapepo na mashetani usisite kumleta Mkutanoni Yesu Kristo atamsaidia na atakuwa sawa.

Mungu akubariki sana Mtu wa Mungu.

Amen.
 
Wagonjwa watasaidiwa na yesu au gwajima,mbona hueleweki? Maana umesema gwajima ndio anafanya mkutano
Bila shaka wewe ndiye hueleweki. Sasa kama umeona mwandishi anasema Gwajima anafanya Mkutano, iweje usijue kuwa anayeponya ni Yesu kupitia kwa mtumishi wake Gwajima. ?
 
Tulio karibu hapa hatutolala kwa amani kwa hizo systems mnazofunga ni hatari

Ila mi ntakuja kushuhudia endapo tu misukule itafufuliwa live
 
Mkuu Masanja atakuja na Crew nzima ya Comedy au peke yake,maana kama watakuja wote sitaki kukosa hiyo show.naomba jibu .Ahsante
 
utanambia siku joyous celebration watakayoimba nije
 
Wajinga ndio waliwao
Ni kweli wajinga ndio waliwao! unakuta mtu na akili zake anaenda kwa waganga wa kienyeji wanakula pesa zake wakati kwa Yesu uponyaji ni bureeeeee!
Unakuta mtu mzima mvaa suruali wa asili lakini anapoteza pesa zake kwa makahaba na hiyo tamaa ya uzinzi haipungui ndo inazidi kuongezeka mwishowe anakufa kwa ukimwi au anatelekeza familia wakati kwa Yesu angesamehewa dhambi zake na kufunguliwa kwenye vifungo vya uzinzi!
Unakuta mtu mzima anamalizia pesa kwenye ulevi mpaka anashindwa kutimizia familia yake mahitaji muhimu kama ya chakula , shule na mavazi wakati kwa Yesu angeokolewa! Kwa kweli wajinga ndio waliwao!
 
Aisee nimepita jioni hii pale mbezi Luis, ile system ya maspika ile aisee ni kiboko. Kwa mandalizi haya, mimi sitakosa nataka nishuhudie kwa macho yangu
 
Ni kweli wajinga ndio waliwao! unakuta mtu na akili zake anaenda kwa waganga wa kienyeji wanakula pesa zake wakati kwa Yesu uponyaji ni bureeeeee!
Unakuta mtu mzima mvaa suruali wa asili lakini anapoteza pesa zake kwa makahaba na hiyo tamaa ya uzinzi haipungui ndo inazidi kuongezeka mwishowe anakufa kwa ukimwi au anatelekeza familia wakati kwa Yesu angesamehewa dhambi zake na kufunguliwa kwenye vifungo vya uzinzi!
Unakuta mtu mzima anamalizia pesa kwenye ulevi mpaka anashindwa kutimizia familia yake mahitaji muhimu kama ya chakula , shule na mavazi wakati kwa Yesu angeokolewa! Kwa kweli wajinga ndio waliwao!

We unaelewa maana ya neno "bure" au ni sawa na voda kutuma msg nunua kifurushi cha shilingi mia 500 na upate dk 10 bureeeeeeeee
 
Huwaga natatizika sana kusikia Masanja mkandamizaji naye eti Muubiri...
Kuna njia nyingi sana za kujipatia kipato lakin sio kwa kumdhihaki Mola
 
Huwaga natatizika sana kusikia Masanja mkandamizaji naye eti Muubiri...
Kuna njia nyingi sana za kujipatia kipato lakin sio kwa kumdhihaki Mola
Si bora hata masanja kuliko huyo Gwajima mara 1000
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom