Mkutano Mkuu UTPC; Mtihani Mkubwa kwa Press Clubs

MtuHabari

JF-Expert Member
Oct 16, 2020
321
1,019
Nikiri kuwa Mimi ni mwanachama wa moja ya Press Club za mkoa ulio mashariki mwa nchi hii lakini pia miaka ya nyuma nilikuwa pia mwanachama wa Mwanza Press Club hadi miaka ya karibuni nilipohamia kwenye chombo cha habari chenye makao makuu yake huku Mikoa ya Pwani.

Hizi Press Clubs ni vyama muhimu sana kwa maslahi ya moja kwa moja kwa waandishi ambao ndio mwanachama wake.

Clubs hizi ziliunda (au kiukweli waliundiwa) chombo wakakiita mwamvuli wao nacho ni UTPC (Union of Tanzania Press Clubs) na ndio hapo misaada na ufadhili mbalimbali toka kwa wahisani inakopitia na kuratibiwa kabla haijafika kwenye Clubs au kwa waandishi wanachama moja kwa moja.

Sasa mwezi huu huko Morogoro utafanyika uchaguzi wa Rais mpya wa UTPC na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi.

Je, wajumbe wa mkutano mkuu huo kutoka kila Press club ambao ni Mwenyekiti, Katibu mkuu na Mweka hazina wanaelewa wanakwenda kufanya nini na umuhimu wa jambo hilo?

Je, wajumbe hao wanafahamu kuwa kwenye nafasi ya Urais kuna waliojipanga kugombea kwa mbinu Kali ya kujinufaisha na tayari wanajinadi kuwa mambo yote sawasawa?

Nini kifanyike kuinusuru UTPC isiingie mikononi mwa matapeli ambao wana historia ya ujanja ujanja na wanaotaka kuhakikisha mambo yote ya UTPC yananufaisha hao walioko huko makao makuu ambako ni Mwanza?
 
Nani anajua historia ya huyu mgombea katika utendaji wake ndani ya hii field ya habari?

Kesho nitashuka na full details ambazo wajumbe wengi wa mikoa wa zamani wanaweza kuzijua Ila itakuwa msaada kwa wasio mfahamu.

Tahadhari ni bora kuliko kusubiri ajali.
IMG-20201102-WA0000.jpg
 
Waandishi wa siku hizi utopolo kulamba viatu vya lumumba na jiwe.njaa zitawaua ,heshima yenu imeshuka sana siku hizi mnashindwa hata kuripoti mambo kwa woga wa kuminywa na jiwe,shame on you
 
Siku hizi hakuna waandishi
Sio hivyo mkuu, waandishi wapo tena mahiri tuu. Shida ni kuruhusu matapeli wachumia tumbo kuingia kwenye uongozi.
Mfano huyo anayepigiwa chapuo ili awe kiongozi mkuu wa Union ya Clubs za waandishi hana rekodi nzuri hata kidogo katika uaminifu.
Ametumikia Mwanza Press kama Mratibu kwa kipindi kirefu hadi alipo toa notice ya kuacha kazi kwa uongozi uliopita baada ya tuhuma nyingi za kutafuna hata michango ya rambirambi.
Akaja kuanzisha eti chama cha Waandishi wapinga madawa ya kulevya ili apige pesa akakwama.
Kifupi ni mpambanaji lakini katika nyanja ya "opportunistic". Kila mahali aonapo kuna mpunga safi atafanya lobbying aingie na apige mpunga.
Katika hali kama hiyo waandishi mahiri watainukia wapi?
Haiwezekani ndani ya mwaka mmoja Huyu Soko aweze kuhakikisha ana pata uenyekiti wa mkoa then achukue na Urais wa UTPC kama sio kuwa alilenga nafasi hiyo au amesukwa na Mkurugenzi yule Mhindi ambaye pia yuko huko Mwanza wahakikishe hiyo nafasi inabaki Mwanza sio kwa maslahi ya Clubs za TZ bali binafsi.
 
Kuna nguvu kubwa sana inatumika huko Mwanza kumnadi mgombea wao mzee wa ujanja ujanja kuna Nini hapo?
Wajumbe wa mkutano mkuu wa UTPC wangejiuliza huyu Soko ana mahusiano gani na yule mtu wa Human right defenders ana itwa Ole Ngurumwa? Jee ni kweli kuwa wanapiga pesa za kesi za kubumba kupitia mawakili wao wanao waweka? Yaani 10-20% zinapitishiwa humo humo katika hela za wafadhili?
Clubs zetu zitapona kweli kuziweka mikononi mwa mtu huyu?
 
Sasa kweli uchaguzi umefika. Nilisema yule mgombea mjanja mjanja na tapeli sasa anasambaza ujumbe kupitia wapambe wake huko kwao Mwanza kumchafua mgombea mwenzie bw. Nsokoro kuwa ni mtoa rushwa.
Oneni ujumbe wanao sambaza hao wajumbe baada ya kuona yeye yuko kimya akisubiri kujieleza mbele ya.mkutano mkuu.
UJUMBE UKO HIVI;

URAIS UTPC NA RUSHWA YA T-SHIRTS!

Tangu kipenga cha kuwania urais wa UTPC kilipopulizwa, tumeshuhudia mgombea mmoja tu wa nafasi ya uras Edwin Soko ndiye amekuwa akinadi sera zake na kutangaza ilani yake ya uchaguzi.

Baadhi yetu tulidhani ni mgombea mmoja pekee ndiye aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo.

Hata hivyo kwa yale yanayoendelea kwenye mitandao ya kijamii yametuamsha usingizini na kubaini kwamba kumbe Deo Nsokolo, rais anayemaliza muda wake naye anagombea kutetea kiti hicho!

Kwa akili ya kawaida kabisa tumekuwa tunajiuliza inawezekana vipi mtu anayegombea ashindwe kutangaza ilani yake ilhali mpinzani wake amefanya hivyo?!

Nadhani sote tunafahamu kwamba katika uchaguzi wowote wagombea hupimwa kwa kusoma au kusikia sera/ilani zao, ndipo wapiga kura huwa kwenye nafasi nzuri ya kujua mgombea wanayekwenda kumchagua atawafanyia nini.

Wataalam wa masuala ya uchaguzi wamekuwa wakijiuliza kulikoni hadi zimebaki siku tatu uchaguzi ufanyike lakini Deo Nsokolo hajatangaza ilani yake?!

Wanasema ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni!
Habari za kiintelejensia zinaonesha kwamba kumbe huyu Deo silaha yake kubwa kwenye uchaguzi ni rushwa!

Inaaminika uchaguzi uliopita pamoja na mambo mengine aligawa vitenge kwa wapiga kura!

Habari zaidi za kiintelejensia zinasema kwamba katika uchaguzi wa mwaka huu Deo Nsokolo amechapisha T-shirts ambazo atazigawa kwa wajumbe!

Kumbe wakati mgombea mwenzake anapambana kunadi sera na kutangaza ilani, yeye (Deo) ameona ilani yake ni kugawa T-shirts kwa wajumbe!

Swali la kujiuliza atazirudishaje fedha zote hizo alizotumia ku-print T-shirts za kuwatosheleza wajumbe wa mkutano mkuu wa UTPC?!

Kuna biashara gani pale UTPC kwamba mtu anaweza kutumia pesa zake za mfukoni kwa ajili ya kutengeneza T-shirts za wajumbe?!

Na kama hakuna ajenda yoyote ya siri kuhusu urais wa UTPC, kwa nini suala hili lilifanywa siri hadi lilipodukuliwa na intelejensia?!

Au ndiyo sababu wapambe wa Deo Nsokolo wamekuwa na ujasiri wa kutangaza kwamba atashinda tu iwe isiwe, kwa vile wanajua kinachoendelea nyuma ya pazia!

TAHADHARI!
Katika zama hizi za utawala wa JPM, rushwa ya aina yoyote mahali popote ni kosa linalopewa uzito mkubwa katika kulishughulikia.

Nsokolo na timu yako mjiandae kuishia kwenye mikono ya Jenerali Mbungo.

MWISHO WA KUNUKUU**"

Jee yeye huyo ameweka wazi kale kakampuni kake ka kukopesha akina mama ntilie na kuwadhurumu riba hadi kuishia kuwa anawanyang'anya masufuria na vyombo?
Ujanja janja wake kujipatia kipato akiuingiza ndani ya Union yetu itasalimika kweli? Au ndio mwisho tuje kukorofishana na wahisani wetu mfano SIDA nk kwa migogoro atakayo leta?
Habari nilizoletewa za uhakika toka huko Mwanza ni kuwa alipopewa Uenyekiti wa muda mwaka Jana katikati baada ya kuukimbia Uratibu alihakikisha viongozi wenzake wote alio kuwa nao na hawakuwa wanaridhishwa na mbinu zake za siri za uongozi wanakosa nafasi ya kurudi katika uchaguzi halisi January mwaka huu.
Huyu malengo yake kumbe yalikuwa urais UTPC ili akawavuruge watendaji humo hasa pale watakapo kuwa hawakubaliani naye.
Viongozi wa Clubs za mikoa ambao ndio wenye maamuzi ya mwisho kwenye uchaguzi sidhani kama ni wajinga kiasi hawawezi ona nia ovu inayokwenda kutokea na kuleta kutoelewana.
EDWARD SOKO NI SUMU NA HAIONJWI, TUIPONYE UTPC YETU
 
Uchaguzi umeisha na nashukuru wajumbe wameelewa na kuogopa Union kuiweka mikononi mwa Tapeli Edwin Soko aliyeambulia 13% ya kura pamoja na mbwembwe zote na kumchafua Nsokoro aliyeibuka mshindi.
Sasa majungu na fitina zake azirudishe huko kwao Mwanza anako wadanganya kila siku kuwa ni mtetezi wao kumbe ni upigaji tuu.
 
Back
Top Bottom