20PROFF
JF-Expert Member
- Nov 5, 2013
- 8,217
- 7,255
Habari wanajamvi,
Natumai ni wazima kabisa. Wale wanaofunga nawapa pole na hongera, makobe badilikeni lakini nyote tumieni mfungo na kipindi kufanya yaliomema na acting ziishe. Leo nimeona niwaletee mkusanyiko wa matukio kadhaa yalioyowahi nitokea, kushuhudia au kusimuliwa na wahusika hii ni sehmu ya fasihi tu, so maudhui ya fasihi nadhani yanatambulika. Ngoja nianze kama ifuatavyo.
Nusura jumba bovu liniangukie: Nakumbuka ilikuwa usiku kama saa tano kuelekea saa sita. Tulikuwa tunapiga pindi na washkaji zangu wa chuo kipindi hiko. Geto letu lilikuwa karibu na Jeshini kabisa, so mpaka uliotenganisha jeshi na uraini ilikuwa ni miti iliyopandwa kama ishara ya mipaka.
Tulisikia kilio cha maumivu makali ambacho kilitupa tasfira kuwa kinatoka kwa binti. Alikuwa akilia kwa uchungu sana na uomba msaada kwa yeyote anayeweza muokoa, kwa haraka haraka nikajua labda anabakwa ama kukabwa na wahuni (maana wahuni hutegaga mara kadhaa kuvizia hapo na wengi wao ni watoto wa kota).
Nilishtua washkaji zangu tonde tukaone yanayojiri. Kutoka nje na kufika eneo la tukio maana kulikuwa hakuna umbali ni hatua kadhaa tu. Nakuta watu wamezunguka kiasi wakiangalia bila kutoa msaada kuhofia kugeuziwa kibao. Kumbe walikuwa wajeda wawili wakitembeza kichapo kwa dada mmoja.
Nilikuta amelala hawezi kusimama, anagalagala kutaka kujitoa katika katika mikono ya wale askari wenye hasira sana, mithiri ya simba alieporwa watoto wake. Kipigo kiliendelea bila wao kuhofu polisi kuja au watu kuingilia maana walimzusha kwewnye ule mpaka wa jeshi (hakuna fensi) na mpaka kufika kwenye geti la jeshi ambapo ndipo walinzi hukaa kuna ka umbali. Huyu dada alipigwa nikaanza kuona akotoka damu puani, pia naye alikuwa hakitamka mbavu zinamuua na mengine mengi. Wajeda walikuwa kimya sana na mara moja moja walikuwa wakiongea kuwa leo tutakua wewe.
Hasira, huruma zote zilinifika kuona hata mmoja wa watu katika kundi lile kashndwa kumpa msaada yule dada, maana hata kama kosa liwe la namna hakushtahili kwa kweli. Nikiwa na washkaji tumekaa karibu na kuangalia nikasema guys Tumsaidie huyu binti, wote walijitoa aisee. Nikasema its oky, let me try to get her out of there ( kipindi hiko nikiwa nimekulia na kuishi kota za jeshi muda mrefu sana so ikabida nitumie akili niijuayo kumsaidia huyu dada ).
Nina mwili na apearnce ya askari kama ukiwa hunifahamu. Kwa haraka haraka nikajua fika kuwa wale lazima watakuwa ni private tu, hakuna ataye zidi SGT. Ikabidi nivae ujasiri na kutoa kauli ya mari kwa wale askari, " nikasema private stand down". Wale jamaa mmoja wao ikibidi ageuke uangalia ni nani anaongea, mwenzie akiwa hajasikia neo kutokana na jazba. Nikarudia wewe kokapu husikiii amri yangu? Jamaa nilichogundua walikuwa maji pia ingawa hawayumbi yumbi, vinywa vyao vilikuwa na harufu ya pombe. Nikaanza zungumza nao na kuuliza nani kawapa kibali cha kupiga raia.
Wakataka nijitamburishe nami nilifanya hivyo, wakijua mimi ni Luteni (ilikuwa usiku, kucheki muonekano wa mwili wangu, na ujasiri na ukali ikabida wajifocre kutulia). Ikabidi waanze kunieleza kwanini wanampiga yule dada, huku yule dada akaanza kuningangania nimuokoe baada ya kuona jamaa wameweza tulia kwa kauli yangu. wakasema makosa ya yule dada kama yafuatayo Jamaa mmoja wapo alianza uhusiano na yule dada, baadae alienda likizo fupi kwao, yule binti aliachiwa pesa na alikuwa anatumiwa pesa na jamaaa kila atakapo au mshahara kutoka.
Pia jamaa alisema yeye ndie alimpangishia chumba na kumnunulia vitu vyote vya ndani. Lakini huyubinti nimerudi huku, nakuta chumba kina mpangaji mwingine nayeye kasema alipata matatizo ikabidi vitu vichukuliwe na kuuzwa alikuwa na madeni so akaamua kurudi kwao. Jamaa kwao hapajui wamekutana mjini, ila anawajua baadhi ya wadada wa huyu binti. Kumbe binti anamzingua jamaa, kapata bwana mwingine lakini mshikaji anapewa kalenda na kujibiwa hovyo sometimes.
Jamaa akasema alimpenda sanmsichana akasamehe yote hayo. Msichana akachana na yule mchepuko karudi kwa jamaa mapenzi yakaendelea, sasa huyu jamaa wa pili yeye ni rafiki wa karibu na huyu mwenzie, alikuwa kikosi kingine na alikutana na huyu binti akiwa na wenzake hapa hapa Dar. Jamaa naye akaingiza chiombezo msicha akalipokea sio wote wawili wakawa wanahudumia, msichana anachanganya wanaume.
Siku imetokea jamaa wakatembeleana kukumbushana mabo yao ya zamani na story za wasichana wa depo, ndipo likaja swala la kunyweshana pumziko lao jipya. Picha zikatolewa kwa simu kutambiana ndipo hapo ikagundulika wanashare, maana wote wakatoa picha zao punde walizopiga na msichana.
Hapo ndipo wakaamua kuweka mtego wamnasebinti, Jamaa akampigia simu msichana aje wanywe na kula nyama jioni, achukue usafiri atalipa, binti alifanya hivyo huku akitoa taarifa za uongo kwa huyu mwingine. Wakaenda bar za uraiani Baada ya vinywaji na maogezi ya hapa na hapa na pale huku mwingine akisubiri sms ya njoo tumalize mchezo akiwa anachoramchezo nzima kwa mbali. Ndipo hapo akatiwa nguvuni na kwenda kuchapiwa hapo mpakani. Wakati hayo maongezi yakifanyika binti alikuwa anasota miguuni mwangu na kulia nimuokoe.
Nilichowambia kuwa hapa kuna haja ya kuumuuliza binti, nikimuuliza jibu ni moja tu napewa, kaka naomba niokoe. Nikajua fika huyu binti ni mkosaji, ila inabidi nimsaidie maana uhai wa mtu ni ghali sana. Nikasema sasa yatosha, mmempiga vya kutosha mwacheni aende la sivyo nitawachukulia sheria, sawa! Wakajibu sawa afande. Hilo jibu lilinipa ujasiri kuwa hawa wameamini mimi ni mkuu wao.
Jamaa mmoja akasema basi naomba nimpeleke kwa dada zake napajua, huyu hawezi kufika mwenyewe. Nikasema huwezi nizidi akili, kumpiga kule kote sasa hivi hasira zimeisha? Au mwataka kwenda kumuua? Ooh huyu hana hela kaangusha pochi huko kwenye mtaro, nikasema pesa mtatoa nyie ya bajaji. Nikawataka wasaidiane kuchanag wenyewe wakatoa pesa, nikaomba baadhi ya watu wasaidie kuita bajaji ikaitwa.
Binti unapakumbuka kwao? Ndio unaweza mulekeza bajaji akafika ndio? Nikasema sawa, bajaji mpeleke chukua namba zangu hzi ukimfikisha kwao nibipu nuiongee na wenyeji wa pale. Binti alifka salama hadi leo hii huwa anasalimia sana na kujiluina hali.Nikasema wangejua mimi sio mjeda ningepotea
Nitaendelea na tukio jingine.......
Natumai ni wazima kabisa. Wale wanaofunga nawapa pole na hongera, makobe badilikeni lakini nyote tumieni mfungo na kipindi kufanya yaliomema na acting ziishe. Leo nimeona niwaletee mkusanyiko wa matukio kadhaa yalioyowahi nitokea, kushuhudia au kusimuliwa na wahusika hii ni sehmu ya fasihi tu, so maudhui ya fasihi nadhani yanatambulika. Ngoja nianze kama ifuatavyo.
Nusura jumba bovu liniangukie: Nakumbuka ilikuwa usiku kama saa tano kuelekea saa sita. Tulikuwa tunapiga pindi na washkaji zangu wa chuo kipindi hiko. Geto letu lilikuwa karibu na Jeshini kabisa, so mpaka uliotenganisha jeshi na uraini ilikuwa ni miti iliyopandwa kama ishara ya mipaka.
Tulisikia kilio cha maumivu makali ambacho kilitupa tasfira kuwa kinatoka kwa binti. Alikuwa akilia kwa uchungu sana na uomba msaada kwa yeyote anayeweza muokoa, kwa haraka haraka nikajua labda anabakwa ama kukabwa na wahuni (maana wahuni hutegaga mara kadhaa kuvizia hapo na wengi wao ni watoto wa kota).
Nilishtua washkaji zangu tonde tukaone yanayojiri. Kutoka nje na kufika eneo la tukio maana kulikuwa hakuna umbali ni hatua kadhaa tu. Nakuta watu wamezunguka kiasi wakiangalia bila kutoa msaada kuhofia kugeuziwa kibao. Kumbe walikuwa wajeda wawili wakitembeza kichapo kwa dada mmoja.
Nilikuta amelala hawezi kusimama, anagalagala kutaka kujitoa katika katika mikono ya wale askari wenye hasira sana, mithiri ya simba alieporwa watoto wake. Kipigo kiliendelea bila wao kuhofu polisi kuja au watu kuingilia maana walimzusha kwewnye ule mpaka wa jeshi (hakuna fensi) na mpaka kufika kwenye geti la jeshi ambapo ndipo walinzi hukaa kuna ka umbali. Huyu dada alipigwa nikaanza kuona akotoka damu puani, pia naye alikuwa hakitamka mbavu zinamuua na mengine mengi. Wajeda walikuwa kimya sana na mara moja moja walikuwa wakiongea kuwa leo tutakua wewe.
Hasira, huruma zote zilinifika kuona hata mmoja wa watu katika kundi lile kashndwa kumpa msaada yule dada, maana hata kama kosa liwe la namna hakushtahili kwa kweli. Nikiwa na washkaji tumekaa karibu na kuangalia nikasema guys Tumsaidie huyu binti, wote walijitoa aisee. Nikasema its oky, let me try to get her out of there ( kipindi hiko nikiwa nimekulia na kuishi kota za jeshi muda mrefu sana so ikabida nitumie akili niijuayo kumsaidia huyu dada ).
Nina mwili na apearnce ya askari kama ukiwa hunifahamu. Kwa haraka haraka nikajua fika kuwa wale lazima watakuwa ni private tu, hakuna ataye zidi SGT. Ikabidi nivae ujasiri na kutoa kauli ya mari kwa wale askari, " nikasema private stand down". Wale jamaa mmoja wao ikibidi ageuke uangalia ni nani anaongea, mwenzie akiwa hajasikia neo kutokana na jazba. Nikarudia wewe kokapu husikiii amri yangu? Jamaa nilichogundua walikuwa maji pia ingawa hawayumbi yumbi, vinywa vyao vilikuwa na harufu ya pombe. Nikaanza zungumza nao na kuuliza nani kawapa kibali cha kupiga raia.
Wakataka nijitamburishe nami nilifanya hivyo, wakijua mimi ni Luteni (ilikuwa usiku, kucheki muonekano wa mwili wangu, na ujasiri na ukali ikabida wajifocre kutulia). Ikabidi waanze kunieleza kwanini wanampiga yule dada, huku yule dada akaanza kuningangania nimuokoe baada ya kuona jamaa wameweza tulia kwa kauli yangu. wakasema makosa ya yule dada kama yafuatayo Jamaa mmoja wapo alianza uhusiano na yule dada, baadae alienda likizo fupi kwao, yule binti aliachiwa pesa na alikuwa anatumiwa pesa na jamaaa kila atakapo au mshahara kutoka.
Pia jamaa alisema yeye ndie alimpangishia chumba na kumnunulia vitu vyote vya ndani. Lakini huyubinti nimerudi huku, nakuta chumba kina mpangaji mwingine nayeye kasema alipata matatizo ikabidi vitu vichukuliwe na kuuzwa alikuwa na madeni so akaamua kurudi kwao. Jamaa kwao hapajui wamekutana mjini, ila anawajua baadhi ya wadada wa huyu binti. Kumbe binti anamzingua jamaa, kapata bwana mwingine lakini mshikaji anapewa kalenda na kujibiwa hovyo sometimes.
Jamaa akasema alimpenda sanmsichana akasamehe yote hayo. Msichana akachana na yule mchepuko karudi kwa jamaa mapenzi yakaendelea, sasa huyu jamaa wa pili yeye ni rafiki wa karibu na huyu mwenzie, alikuwa kikosi kingine na alikutana na huyu binti akiwa na wenzake hapa hapa Dar. Jamaa naye akaingiza chiombezo msicha akalipokea sio wote wawili wakawa wanahudumia, msichana anachanganya wanaume.
Siku imetokea jamaa wakatembeleana kukumbushana mabo yao ya zamani na story za wasichana wa depo, ndipo likaja swala la kunyweshana pumziko lao jipya. Picha zikatolewa kwa simu kutambiana ndipo hapo ikagundulika wanashare, maana wote wakatoa picha zao punde walizopiga na msichana.
Hapo ndipo wakaamua kuweka mtego wamnasebinti, Jamaa akampigia simu msichana aje wanywe na kula nyama jioni, achukue usafiri atalipa, binti alifanya hivyo huku akitoa taarifa za uongo kwa huyu mwingine. Wakaenda bar za uraiani Baada ya vinywaji na maogezi ya hapa na hapa na pale huku mwingine akisubiri sms ya njoo tumalize mchezo akiwa anachoramchezo nzima kwa mbali. Ndipo hapo akatiwa nguvuni na kwenda kuchapiwa hapo mpakani. Wakati hayo maongezi yakifanyika binti alikuwa anasota miguuni mwangu na kulia nimuokoe.
Nilichowambia kuwa hapa kuna haja ya kuumuuliza binti, nikimuuliza jibu ni moja tu napewa, kaka naomba niokoe. Nikajua fika huyu binti ni mkosaji, ila inabidi nimsaidie maana uhai wa mtu ni ghali sana. Nikasema sasa yatosha, mmempiga vya kutosha mwacheni aende la sivyo nitawachukulia sheria, sawa! Wakajibu sawa afande. Hilo jibu lilinipa ujasiri kuwa hawa wameamini mimi ni mkuu wao.
Jamaa mmoja akasema basi naomba nimpeleke kwa dada zake napajua, huyu hawezi kufika mwenyewe. Nikasema huwezi nizidi akili, kumpiga kule kote sasa hivi hasira zimeisha? Au mwataka kwenda kumuua? Ooh huyu hana hela kaangusha pochi huko kwenye mtaro, nikasema pesa mtatoa nyie ya bajaji. Nikawataka wasaidiane kuchanag wenyewe wakatoa pesa, nikaomba baadhi ya watu wasaidie kuita bajaji ikaitwa.
Binti unapakumbuka kwao? Ndio unaweza mulekeza bajaji akafika ndio? Nikasema sawa, bajaji mpeleke chukua namba zangu hzi ukimfikisha kwao nibipu nuiongee na wenyeji wa pale. Binti alifka salama hadi leo hii huwa anasalimia sana na kujiluina hali.Nikasema wangejua mimi sio mjeda ningepotea
Nitaendelea na tukio jingine.......