Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,412
Umeingia ofisini saa 2 asubuhi, ukakuta hakuna umeme umekaa siku nzima ukisuniri umeme.
Unaamua kuondoka saa 11 jioni, ukijifariji kwamba utaukuta umeme nyumbani angalau ufanye kazi za wateja wako.
Unafika nyumbani saa 1 kasoro unakuta hakuna umeme wanakuambia wamekata saa 12 jioni. Unajaribu kuusubiri umeme Hadi saa 6 usiku, hakuna umeme.
Unaamua kwenda kulala, kitandani una mtoto wa miezi 10 unakuta anahangaika joto usiku mzima analia. Unashindwa hata kulala. Huku ukiwa na stress za kazi za watu.
Mwisho wa siku muendelee kusema Vijana wa Tanzania ni wavivu, hawajitumi, uzembe mwingi. Asubuhi nitaamka, unakuta sms za TRA wanakusubiri Kodi zao za ajabu za kubambikiwa, Jiji na leseni zao wanaakusubiri tozo nyingi nyingi... Daaahhh!
Anyway mnaopush agenda[CHAWA], na hashtags ni MAJASIRI sana, Mungu awasaidie kuona MAISHA HALISI kuliko kuona Pesa. Sijui mnaishije wenzetu, sijui mko Tanzania ya wapi wenzetu Tunajitekenya wenyewe tunacheka wenyewe.
Tujifunze kupendana Kwanza na tujifunze kujaliana. Pia tujifunze kuambizana ukweli. UBINAFSI unarudisha Maendeleo. Na ubinafsi wa watu kadhaa umekwamisha Taifa kufika kwenye malengo.
SIASA TOO MUCH IS HURTFUL AND HURTFUL
crdt : Lusaj0
Unaamua kuondoka saa 11 jioni, ukijifariji kwamba utaukuta umeme nyumbani angalau ufanye kazi za wateja wako.
Unafika nyumbani saa 1 kasoro unakuta hakuna umeme wanakuambia wamekata saa 12 jioni. Unajaribu kuusubiri umeme Hadi saa 6 usiku, hakuna umeme.
Unaamua kwenda kulala, kitandani una mtoto wa miezi 10 unakuta anahangaika joto usiku mzima analia. Unashindwa hata kulala. Huku ukiwa na stress za kazi za watu.
Mwisho wa siku muendelee kusema Vijana wa Tanzania ni wavivu, hawajitumi, uzembe mwingi. Asubuhi nitaamka, unakuta sms za TRA wanakusubiri Kodi zao za ajabu za kubambikiwa, Jiji na leseni zao wanaakusubiri tozo nyingi nyingi... Daaahhh!
Anyway mnaopush agenda[CHAWA], na hashtags ni MAJASIRI sana, Mungu awasaidie kuona MAISHA HALISI kuliko kuona Pesa. Sijui mnaishije wenzetu, sijui mko Tanzania ya wapi wenzetu Tunajitekenya wenyewe tunacheka wenyewe.
Tujifunze kupendana Kwanza na tujifunze kujaliana. Pia tujifunze kuambizana ukweli. UBINAFSI unarudisha Maendeleo. Na ubinafsi wa watu kadhaa umekwamisha Taifa kufika kwenye malengo.
SIASA TOO MUCH IS HURTFUL AND HURTFUL
crdt : Lusaj0