Feedback
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 7,988
- 4,507
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imemshtaki katika Mahakama Kuu ya Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BP, Engelbert Kongolo ikiiomba aeleze kwa nini asifungwe kwa kukataa kufuata amri ya utii (Compliance Order) iliyotolewa na mamlaka hiyo.
Ewura ilifungua jana kesi hiyo namba 130 ya mwaka huu, huku mamlaka hiyo ikiomba mkurugenzi huyo alipe gharama za kesi hiyo.Kesi hiyo ilifunguliwa na Ewura kupitia wakili James Kabakama wa kampuni ya GRK Advocates.
Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam hivi karibuni, Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu alisema Katika uamuzi wake wa Bodi ya Wakurugenzi uliofikiwa Agosti 9 mwaka huu, Imeagiza mkurugenzi mkuu na mwenyekiti wa BP kufikishwa mahakamani kwa kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai (DPP).
Kabla ya kufikia hatua hiyo ya kuishtaki BP, Ewura ilikuwa imetoa amri kwa kampuni nne zinazosambaza mafuta kurejesha huduma hiyo mara moja huku ikizitaka kujieleza, kwa nini zisichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kushindwa kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa leseni zao za biashara. Ziligoma zikipinga punguzo la bei ya bidhaa hiyo iliyokuwa imetangazwa na mamlaka hiyo.
Kampuni hizo ni pamoja na BP ambayo Serikali inamiliki nusu ya hisa pamoja na Engen, Oil Com na Camel. Tatu zilitii lakini BP ilikaidi kitendo ambacho kiliifanya Ewura kusitisha leseni yake ya biashara kwa miezi mitatu.
Katika uamuzi huo wa kusitisha leseni, vituo vyote vya rejareja vyenye nembo ya BP viliruhusiwa kuuza mafuta kwa kununua bidhaa hiyo kwa wafanyabiashara wengine wa jumla.
Source: Mwananchi
Ewura ilifungua jana kesi hiyo namba 130 ya mwaka huu, huku mamlaka hiyo ikiomba mkurugenzi huyo alipe gharama za kesi hiyo.Kesi hiyo ilifunguliwa na Ewura kupitia wakili James Kabakama wa kampuni ya GRK Advocates.
Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam hivi karibuni, Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu alisema Katika uamuzi wake wa Bodi ya Wakurugenzi uliofikiwa Agosti 9 mwaka huu, Imeagiza mkurugenzi mkuu na mwenyekiti wa BP kufikishwa mahakamani kwa kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai (DPP).
Kabla ya kufikia hatua hiyo ya kuishtaki BP, Ewura ilikuwa imetoa amri kwa kampuni nne zinazosambaza mafuta kurejesha huduma hiyo mara moja huku ikizitaka kujieleza, kwa nini zisichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kushindwa kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa leseni zao za biashara. Ziligoma zikipinga punguzo la bei ya bidhaa hiyo iliyokuwa imetangazwa na mamlaka hiyo.
Kampuni hizo ni pamoja na BP ambayo Serikali inamiliki nusu ya hisa pamoja na Engen, Oil Com na Camel. Tatu zilitii lakini BP ilikaidi kitendo ambacho kiliifanya Ewura kusitisha leseni yake ya biashara kwa miezi mitatu.
Katika uamuzi huo wa kusitisha leseni, vituo vyote vya rejareja vyenye nembo ya BP viliruhusiwa kuuza mafuta kwa kununua bidhaa hiyo kwa wafanyabiashara wengine wa jumla.
Source: Mwananchi